Tuanze na mwamko wa kisiasa kabla ya kudai Katiba Mpya

Tuanze na mwamko wa kisiasa kabla ya kudai Katiba Mpya

Uncle Araali

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2014
Posts
950
Reaction score
1,262
Kwa muda mrefu,pamekuwa na jitihada na mashinikizo kutoka kwa vyama vya siasa,asasi za kiraia na wananchi wenye mapenzi mema na taifa lao la Tanzania.Harakati zote hii zimechochewa na jinsi katiba iliyopo ilivyo na walakini na dosari anuwai,ambazo wengi wanaona ni bora tuwe na katiba inayoendana na wakati huu,katiba inayowawajibisha viongozi wetu kwa maslahi ya taifa na kulinda haki na uhuru wa raia.Hili ni jambo jema kabisa.

Lakini kwa mtazamo wangu,tukiidai katiba mpya bila ya kutengeneza uelewa wa kisiasa kwa wananchi walio wengi,bado tutabaki hapahapa,licha ya kupata katiba mpya.Wananchi wengi bado wana uelewa mdogo na masuala mapana,hata yanayowagusa moja kwa moja.Hawajui kuwa kiongozi anapaswa kuwajibishwa,pale anapokwenda ndivyo sivyo.

Ninashauri kuwa,kwa sasa nguvu kubwa zaidi,pamoja na vuguvugu la kudai katiba mpya,vyama vya siasa,asasi za kiraia na raia wenye mapenzi mema wawekeze zaidi katika uelimishaji wa jamii kuhusu masuala ya kisiasa. Nawanukuu wataalamu wafuatao wa maswala ya siasa:

"Institutions alone are not enough to rein in elected autocrats. Constitutions must be defended - by political parties and organized citizens, but also by democratic norms. Without robust norms, constitutional checks and balances do not serve as the bulwarks of democracy we imagine them to be.

nstitutions become political weapons, wielded forcefully by those who control them against those who do not. This is how elected autocrats subvert democracy - packing and "weaponizing" the courts and other neutral agencies, buying off the media and private sector (or bullying them into silence) and rewriting the rules of politics to tilt the playing field against opponents"

(Steven Levitsky & Daniel Ziblatt: HOW DEMOCRACIES DIE)

Nawasilisha hoja.
 
Kama demokrasia imesimamishwa ambayo inanafasi ya kutoa elimu hiyo Kwa raia wa kawaida kwamsaada wa dola/wasimamizi wa haki na mamlaka saidizi, sasa hapa hoja yako ni ipi je sii sawa na kufukuza upepo, au kutaka kuupaka upepo rangi?
 
Chawa wa jiwe, SSH na CCM anapotoa ushauri wa namna ya kupata katiba mpya 😁😁
 
Tatizo ni mamlaka zinazohusika kuwawajibisha hawa viongozi hazitendi haki ndio maana hata pale kiongozi anapokiuka sheria bado anabebwa na wale tunawaamini wasimamie sheria zetu na kuzitekeleza, hata tukiwaelimisha wananchi na tukawa na katiba mpya pasipo kubadikisha mifumo yetu ni kazi bure, viongozi wetu hawana uzalendo wa kusimamia na kutekelileza matakwa ya kikatiba badala yake wanabebana kwa mgongo wa vyama na itikadi zake, pamoja na Elimu ya uraia au mwamko wa kisiasa, bado tunahitaji mfumo imara utakaowezesha sheria zetu kutekelezwa na kuwajibisha viongozi pasipo kujali nafasi zao ndani ya serikali.
 
Tatizo ni mamlaka zinazohusika kuwawajibisha hawa viongozi hazitendi haki ndio maana hata pale kiongozi anapokiuka sheria bado anabebwa na wale tunawaamini wasimamie sheria zetu na kuzitekeleza...
Umesema ukweli mkuu
 
Kama demokrasia imesimamishwa ambayo inanafasi ya kutoa elimu hiyo Kwa raia wa kawaida kwamsaada wa
dola/wasimamizi wa haki na mamlaka saidizi, sasa hapa hoja yako ni ipi je sii sawa na kufukuza upepo, au kutaka kuupaka upepo rangi?
Wale waliokula kiapo kupitia vitabu vitakatifu kwamba watailinda katiba ndio hao hao wanaoivunja katiba, sijui wananchi wakimbilie kwa nani
 
Wale waliokula kiapo kupitia vitabu vitakatifu kwamba watailinda katiba ndio hao hao wanaoivunja katiba, sijui wananchi wakimbilie kwa nani

Ukweli mchungu ni kuwa kwa njia zote za amani hakuna pa kukimbilia:

Machinga wanapotoa Somo, Makamanda tunakwama Wapi?

Wao ndiyo wanaotulazimisha si kwa kupenda kwetu bali shuruti zao.

Chawa wengine hawa, sad to say hawana lolote la maana.
 
Tatizo ni mamlaka zinazohusika kuwawajibisha hawa viongozi hazitendi haki ndio maana hata pale kiongozi anapokiuka sheria bado anabebwa na wale tunawaamini wasimamie sheria zetu na kuzitekeleza, hata tukiwaelimisha wananchi na tukawa na katiba mpya pasipo kubadikisha mifumo yetu ni kazi bure, viongozi wetu hawana uzalendo wa kusimamia na kutekelileza matakwa ya kikatiba badala yake wanabebana kwa mgongo wa vyama na itikadi zake, pamoja na Elimu ya uraia au mwamko wa kisiasa, bado tunahitaji mfumo imara utakaowezesha sheria zetu kutekelezwa na kuwajibisha viongozi pasipo kujali nafasi zao ndani ya serikali
Ubovu wa katiba unachangia kutowajibika/kuwajibishwa kwao mbali na ukosefu wa uadilifu, usisahau tayari wapo waliojitemgenezea Kinga ya kutoshitakiwa.
 
Wale waliokula kiapo kupitia vitabu vitakatifu kwamba watailinda katiba ndio hao hao wanaoivunja katiba, sijui wananchi wakimbilie kwa nani
Njoni kwangu nami nitawaponya
Hili swala la kwa Katiba Sasa Bado Sana kupatikana
Labda zianze movement kubwa za kisiasa na ziongozwe na vyama vya kisiasa
Na vitaanza lini
 
Back
Top Bottom