TUCTA acheni unafiki!

TUCTA acheni unafiki!

CK Allan

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2013
Posts
2,781
Reaction score
6,139
TUCTA ! TUCTA! TUCTA!
Shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini Tanzania nimewaita mara tatu! Hivi kwanini ninyi ni wanafiki kiasi hiki? Kwanini yaani!

Wanabodi,

Kama mtakumbuka mara ya mwisho mishahara kupandishwa angalau kwa kiasi kikubwa ni wakati wa JK Kikwete! Mara baada ya Raisi magufuli kuingia madarakani mwaka 2015 Kila kitu kinachohusu maslahi ya wafanyakazi kilisimama!

Hakukuwa na kupanda madaraja Wala kupata hata Ile nyongeza ya Kila mwaka ya kisheria (annual increment)
Lakini Mbaya zaidi Kuna kitu TUCTA na Wana harakati hawasemi:

Kulikua na zoezi la uhakiki wa watumishi wa Uma! Katika zoezi hili wafanyakazi walio mbali na halmashauri zao walijigharamia wenyewe Nauli na gharama za kushughulikia nyaraka na chakula n.k kwa muda wote wa zoezi! Yaani zoezi la uhakiki lilikuwa la mwajiri lakini gharama ni kwa mfanyakazi!

Haya tuache hili likapita! Baadae akasema hakuna kupanda madaraja kwanza Mpaka atoe watumishi hewa! Wafanyakazi wakasubiri.

Mwishowe akasema ataongeza ila kwanza wafanyakazi waunganishe Namba zao za NIDA na mishahara aka uhakiki wa NIDA, wafanyakazi wakasubiri! Na miaka ikasonga, ikasonga ikafika SABA (7) bila bila!

Wakati haya yote yakitokea viongozi wa TUCTA hakuna aliyetokeza pua yake hadharani kulalamika Wala kukosoa! Sana Sana walituomba wafanyakazi 'tusikilizie' TU, lakini wakati sisi tunaugulia maumivu wao viongozi wa TUCTA kimya kimya walikuwa wanaenda Ikulu kwa mlango wa kufanya vikao vya majadiliano huko walikua Per DM na marupu rupu kibao, haikuishia hapo wengine wakala Teuzi za ukuu wa wilaya na ubunge!! Kama naongopa waje hapa kukanusha!! Kilio Cha wafanyakazi kikawa kilio Cha samaki mpaka pale yaliyotokea yakatokea na Mama Samia Suluhu akaingia madarakani! Jambo la kwanza kwa haraka mama akapandisha Madaraja!

Kwa haraka kabisa! Imagine mtu aliyeajiriwa mwaka 2014 alikaa miaka 7! Bila kuonja daraja, wakati mama anaendelea na Hali hii ngumu kwasasa Duniani ya Vita ya Ukraine Bado akaongeza Hiyo 23.3 kwa kima cha chini!

Kumbuka ni mwaka mmoja TU mama madarakani! Lakini tayari TUCTA washajitokeza hadharani na kujifanya wanatetea Sana wafanyakazi fyuuuuuuuuu!

Yaani yule ambaye alituweka miaka 7 bila chochote mlikaa kimya Leo anakuja mtu mwaka mmoja tu anapandisha madaraja TUCTA mnajifanya kumkosoa!

Kwanini msijtokeze hadharani kukosoa Wakati wa Magufuli kama kweli nyie ni watu wazuri? Acheni unafiki wenu mara Moja!!

Mwisho,
Ushauri wangu kwa Raisi Samia kama ikikupendeza mrudishe Mchenjerwa kwenye utumishi halafu Kuna watu hawapendi wafanyakazi waboreshewe maslahi Yao kwakuwa tayari Wana Imani na itikadi za ' previous' watu hao ikikupendeza uwatoe uwape majukumu mengine au wasirudi Tena baraza lijalo!

Kwaherini
 
TUCTA ni kama CWT tu.

Hawana la maana wanalofanya zaidi ya kushibisha matumbo yao.

Hata juzi viongozi wa juu watakuwa wamelambishwa asali ili wapotezee harakati ya kupigania watumishi wenye miaka 6 bila nyobgeza ya mishahara halafu wakaongezewa 12,000/= na wengine 20,000/=

Hao TUCTA usiwahesabie kama wapo.
 
Mbaya wetu sio Samia, wabaya tumeanza kuwajua....na Mungu yupo atashughulika nao.
Rais Samia kaingia tu kaondoa retention fee ya bodi, Ila wabaya kuna namna wakaiweka weka, mara wanasema wanaondoa retention kuanzia aliposema mama.

Rais Samia kapandisha madaraja watumishi wote walostahili....ana Baya gani?

Naamini kuna wanaomshauri vibaya Ili kumgombanisha na wapiga Kura....na huo Urais mnaoupigania hamtoupata wanga nyie.......Uongozi unatoka Kwa Mungu, Yuko wapi mwenzenu aliyetengeneza Kura feki?
Na Sisi tunaendelea kumlilia Mungu, atashughulikia tu.
 
TUCTA ! TUCTA! TUCTA!
Shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini Tanzania nimewaita mara tatu! Hivi kwanini ninyi ni wanafiki kiasi hiki? Kwanini yaani!

Wanabodi,

Kama mtakumbuka mara ya mwisho mishahara kupandishwa angalau kwa kiasi kikubwa ni wakati wa JK Kikwete! Mara baada ya Raisi magufuli kuingia madarakani mwaka 2015 Kila kitu kinachohusu maslahi ya wafanyakazi kilisimama!

Hakukuwa na kupanda madaraja Wala kupata hata Ile nyongeza ya Kila mwaka ya kisheria (annual increment)
Lakini Mbaya zaidi Kuna kitu TUCTA na Wana harakati hawasemi:

Kulikua na zoezi la uhakiki wa watumishi wa Uma! Katika zoezi hili wafanyakazi walio mbali na halmashauri zao walijigharamia wenyewe Nauli na gharama za kushughulikia nyaraka na chakula n.k kwa muda wote wa zoezi! Yaani zoezi la uhakiki lilikuwa la mwajiri lakini gharama ni kwa mfanyakazi!

Haya tuache hili likapita! Baadae akasema hakuna kupanda madaraja kwanza Mpaka atoe watumishi hewa! Wafanyakazi wakasubiri.

Mwishowe akasema ataongeza ila kwanza wafanyakazi waunganishe Namba zao za NIDA na mishahara aka uhakiki wa NIDA, wafanyakazi wakasubiri! Na miaka ikasonga, ikasonga ikafika SABA (7) bila bila!

Wakati haya yote yakitokea viongozi wa TUCTA hakuna aliyetokeza pua yake hadharani kulalamika Wala kukosoa! Sana Sana walituomba wafanyakazi 'tusikilizie' TU, lakini wakati sisi tunaugulia maumivu wao viongozi wa TUCTA kimya kimya walikuwa wanaenda Ikulu kwa mlango wa kufanya vikao vya majadiliano huko walikua Per DM na marupu rupu kibao, haikuishia hapo wengine wakala Teuzi za ukuu wa wilaya na ubunge!! Kama naongopa waje hapa kukanusha!! Kilio Cha wafanyakazi kikawa kilio Cha samaki mpaka pale yaliyotokea yakatokea na Mama Samia Suluhu akaingia madarakani! Jambo la kwanza kwa haraka mama akapandisha Madaraja!

Kwa haraka kabisa! Imagine mtu aliyeajiriwa mwaka 2014 alikaa miaka 7! Bila kuonja daraja, wakati mama anaendelea na Hali hii ngumu kwasasa Duniani ya Vita ya Ukraine Bado akaongeza Hiyo 23.3 kwa kima cha chini!

Kumbuka ni mwaka mmoja TU mama madarakani! Lakini tayari TUCTA washajitokeza hadharani na kujifanya wanatetea Sana wafanyakazi fyuuuuuuuuu!

Yaani yule ambaye alituweka miaka 7 bila chochote mlikaa kimya Leo anakuja mtu mwaka mmoja tu anapandisha madaraja TUCTA mnajifanya kumkosoa!

Kwanini msijtokeze hadharani kukosoa Wakati wa Magufuli kama kweli nyie ni watu wazuri? Acheni unafiki wenu mara Moja!!

Mwisho,
Ushauri wangu kwa Raisi Samia kama ikikupendeza mrudishe Mchenjerwa kwenye utumishi halafu Kuna watu hawapendi wafanyakazi waboreshewe maslahi Yao kwakuwa tayari Wana Imani na itikadi za ' previous' watu hao ikikupendeza uwatoe uwape majukumu mengine au wasirudi Tena baraza lijalo!

Kwaherini
Watesi wa watumishi ndio washauri wa mkuu.... Watampa takwimu za uongo kama walivyozoea... Hata chekechea hawezi elewa hiyo ya kuwapa watu 20,000/ baada ya kilio na mateso makali kwa zaidi ya miaka Saba. Bidhaa nyingi zimepanda zaidi ya 150% halafu unamwongezea mtu 0.6%
 
CHODAWU moja ya vyama shiriki vya TUCTA ilituachia sisi wafanyakazi wa hoteli za kitalii (TAHI) kanda ya kaskazini kuachishwa kazi wakati wa ubinafsishaji kwa malipo ya mshahara wa mwezi mmoja tuu, licha ya kuwachangi kwa zaidi ya miaka thelathini
Jitihada za kuwasihi wasimamie mikataba ya hiari miaka mowili kabla hawakufanya lolote
Mishara ilikuwa wastani wa 50000.- tuu
Hivi vyama vya wafanyakazi nchi hii vipo kukusanya michango na kununua t shirt za mei mosi tuu
 
Nashukuru niliishia elimu ya darasa la saba aya mateso sijawai pitia. Nachofahamu mie ni kukwepa kodi na kupambana na TRA
Dah! Ila kukwepa kodi kwa wafanyabiashara raha aisee!

Maana wale wanyonyaji wanaambulia kodi kidogo tu. Kinachobakia chote, unabeba mwenyewe.
 
Back
Top Bottom