Tuendelee kutunza kumbukumbu za biashara ya utumwa?

Tuendelee kutunza kumbukumbu za biashara ya utumwa?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Biashara ya utumwa ilikuwa udhalilishaji mkubwa wa utu, kuendelea kuitunza kumbukumbu hii na kuwaonyesha watoto wetu ni sawa sawa na mzazi kuendelea kutunza chupi yenye damu ya mtoto wake aliyebakwa kikatili miaka mingi iliyopita.

Kumbukumbu hizi zinazidi kuwafanya wazungu na waarabu wazidi kuwa imara kuliko sisi, kutudharau na sisi tuzidi kuwaona wazungu ni mabwana zetu milele kwa kuwa watoto, wajukuu, watukuu na vilembwe wana tabia ya kujivunia matendo ya mababu zao.

Hata kama kumbukumbu hizi zinatunzwa kwa lengo la kutuingizia pesa kutoka kwa wazungu haohao walioendesha biashara hii pesa hizo zinatoka kwenye chanzo kisicho sahihi na haramu.

Watoto wetu wakitoka kutembelea kumbukumbu hizo huko Bagamoyo na Zanzibar huwa wanarudi nyumbani vichwa chini na kuwaona watoto wa kizungu kama watu bora kabisa (superior) na katili.
.
 
Ukweli unapaswa uwekwe wazi. Ni juu yetu kama ukweli unatunyong'onyesha au unatujenga
 
Ukweli unapaswa uwekwe wazi. Ni juu yetu kama ukweli unatunyong'onyesha au unatujenga
kwa maslahi gani? mnafikiria iko siku mtaomba fidia kwa hilo? unadhani wazungu wakiiona historia hiyo wanatuaonea huruma na kujisikia vibaya?

Mlishafanya utafiti kujua wazungu na waarabu wanajisikiaje tukiwaonyesha historia ya uovu waliofanya babu zao kwetu? wanajutia, wanaona kawaida au wanafurahia?

Hiyo ni ajira tu kwa watu kuonyesha watu namna tulivyotwezwa basi
 
Kama zilivyo kumbukumbu za holocaust ambapo Wayahudi milioni kadhaa waliuliwa, kama ilivyo mauaji ya kidini na kikabila huko Kosovo, kama ilivyo kwa maujaji ya kimbari ya Rwanda ambayo yote yako very well documented, kuna umuhimu wa kuweka kumbukumbu hizi ili kizazi cha sasa na vizazi vijavyo viseme NEVER AGAIN
 
Historia ipo kujifunza. Historia inatupa mwongozo wa tulipotoka, tulipo na tunapoelekea. Hivyo hoja yako ya kutokomeza kumbukumbu za historia kwa kigezo kwamba zinatudhalilisha ni mawazo potofu.

Bila historia usingeandika hata huu uzi, kila siku ungekuwa unajiuliza nini tofauti yako na wazungu? Kumbe tofauti inapatikana kwenye historia, wao walistarabika mapema na kututumia waafrika kwa manufaa yao na uchumi wao ulipo leo waafrika tumehusika zaidi. Hivyo tuitumie historia kurekebisha makosa yetu ya nyuma na tusiione kama kizingiti kwetu.
 
Historia ipo kujifunza. Historia inatupa mwongozo wa tulipotoka, tulipo na tunapoelekea. Hivyo hoja yako ya kutokomeza kumbukumbu za historia kwa kigezo kwamba zinatudhalilisha ni mawazo potofu.

Bila historia usingeandika hata huu uzi, kila siku ungekuwa unajiuliza nini tofauti yako na wazungu? Kumbe tofauti inapatikana kwenye historia, wao walistarabika mapema na kututumia waafrika kwa manufaa yao na uchumi wao ulipo leo waafrika tumehusika zaidi. Hivyo tuitumie historia kurekebisha makosa yetu ya nyuma na tusiione kama kizingiti kwetu.
Hauko sahihi, Wamarekani walitawaliwa na Uingereza lakini Marekani imefanya na inaendelea kufanya kila kitu ili kupoteza historia hiyo ya kidhalimu kwa kutoifunfisha shuleni, kugeuza kila kitu kitofautiane na cha Uingereza kama vile magari to keep right barabarani badala ya left. Usukani wa magari kuwa kushoto, American English and spellings, kutumia kipimo cha gallon badala ya litre, kutumia vipimo tofauti vya umeme na vifaa vya umeme. Wanafanya hivyo ili kututa aibu ya kuambiwa wametawaliwa na Uingereza. Sisi hapa tunaweka na kuhifadhi vitu vyooote vya mkoloni, shame.

Mauaji ya Rwanda nitofauti sana na biashara ya utumwa.
 
Baadae tutakuja ulizana, je tuweke wazi mikataba mibovu iliyokuwa inasainiwa na akina kikwete, mkapa, chenge, na nk kuruhusu wazungu kujichotea madini yetu? Na twiga kupanda ndege ? Ni sawa au ni aibu?
 
Baadae tutakuja ulizana, je tuweke wazi mikataba mibovu iliyokuwa inasainiwa na akina kikwete, mkapa, chenge, na nk kuruhusu wazungu kujichotea madini yetu? Na twiga kupanda ndege ? Ni sawa au ni aibu?
Kama iko faida Kwa kuiweka wazi sioni shida.

Sababu za kutunza historia ya biashara ya utumwa ni dhaifu
 
Kama iko faida Kwa kuiweka wazi sioni shida.

Sababu za kutunza historia ya biashara ya utumwa ni dhaifu

Walioleta dini ndio hao hao waliotupeleka utumwani huku pamoja na mengine wakivunja map.umbu ya mababu zetu.

Tuache tu kila kitu kiwe kama kilivyo
 
Back
Top Bottom