Tuepuke matumizi mabaya ya neno "Bilionea"

Tuepuke matumizi mabaya ya neno "Bilionea"

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kwa Tanzania hasa watu wa kanda ya Kaskazini wana matumizi mabaya sana ya neno bilionea. Ukiwa tu na uwezo wa kumiliki gari nzuri ya thamani kubwa, bus kadhaa za usafirishaji au ghorofa maeneo ya kitajiri wewe tayari umekuwa bilionea.

Tuache huu ushamba, bilionea kidunia/kimataifia ni mtu mwenye "networth"/utajiri wa dola za kimarekani bilioni moja($1b) na kuendelea, kama mtu yuko chini ya hapo huyo sio bilionea. Kwa hapa bongo bilionea anayetambulika kwa sasa ni Mo, kuna wakati Rostam Aziz pia aliingia kwenye ubilionea ila sijui kama bado yupo kwenye list.

Tanzania wengi tulio nao ni mamilionea, hawa ni watu wanaomiliki utajiri wa zaidi ya dola za kimarekani milioni 1( $1m). Tuepuke matumizi mabaya na ushamba wa neno bilionea.
 
Unakosea

Mtu mwenye utajiri wa shilingi bilioni moja za kitanzania na kuendelea, huyo nae ni bilionea

Tukitumia kigezo chako mabilionea tanzania watakuwa watatu tu

Wakati watu wenye utajiri wa $1m kuendelea wapo wengi, na hiyo inamaanisha mabilionea wapo wengi zaidi ukizingatia bilioni moja inalingana na $500k
Screenshot_20240809-102822_Chrome.jpg
 
Kwa Tanzania hasa watu wa kanda ya Kaskazini wana matumizi mabaya sana ya neno bilionea. Ukiwa tu na uwezo wa kumiliki gari nzuri ya thamani kubwa, bus kadhaa za usafirishaji au ghorofa maeneo ya kitajiri wewe tayari umekuwa bilionea.

Tuache huu ushamba, bilionea kidunia/kimataifia ni mtu mwenye "networth"/utajiri wa dola za kimarekani bilioni moja($1b) na kuendelea, kama mtu yuko chini ya hapo huyo sio bilionea. Kwa hapa bongo bilionea anayetambulika kwa sasa ni Mo, kuna wakati Rostam Aziz pia aliingia kwenye ubilionea ila sijui kama bado yupo kwenye list.

Tanzania wengi tulio nao ni mamilionea, hawa ni watu wanaomiliki utajiri wa zaidi ya dola za kimarekani milioni 1( $1m). Tuepuke matumizi mabaya na ushamba wa neno bilionea.

Kwa mwendo huu:

F9Nuw_WXYAA3qAr.jpeg


Atakuwa mbioni kurejea kama alitoka.
 
Arusha mtu akiitwa bilionea fahamu machalii wanatumia hela yao yaani shilingi
 
Kama bakhresa siyo bilionea ni milionea....mimi ni nani🤔🤔🤔
 
Kwani sisi tunatumia dola we mzee mbona unakuwa mtumwa mtumwa sana.
 
Tuambie sasa hiyo tafsiri umeitoa wapi?. Maana isije ikawa wewe ndio mshamba?. Je mtu akimiliki bilioni 4+ Tshs kwa nini asiitwe bilionea?. Sema kwa nini asiwe bilionea?.
 
Hiki ndiyo kipimo halisi cha Mtanzania aliyetumia mda wake wote kwa siku ya leo kufikiria na kuja na kitu kama hiki..

Yoda ni miyeyusho sana
 
Kwa Tanzania hasa watu wa kanda ya Kaskazini wana matumizi mabaya sana ya neno bilionea. Ukiwa tu na uwezo wa kumiliki gari nzuri ya thamani kubwa, bus kadhaa za usafirishaji au ghorofa maeneo ya kitajiri wewe tayari umekuwa bilionea.

Tuache huu ushamba, bilionea kidunia/kimataifia ni mtu mwenye "networth"/utajiri wa dola za kimarekani bilioni moja($1b) na kuendelea, kama mtu yuko chini ya hapo huyo sio bilionea. Kwa hapa bongo bilionea anayetambulika kwa sasa ni Mo, kuna wakati Rostam Aziz pia aliingia kwenye ubilionea ila sijui kama bado yupo kwenye list.

Tanzania wengi tulio nao ni mamilionea, hawa ni watu wanaomiliki utajiri wa zaidi ya dola za kimarekani milioni 1( $1m). Tuepuke matumizi mabaya na ushamba wa neno bilionea.
Mkuu kuna madhara gani wakiitana mabilionea?
 
Bilionea ni mtu mwenye ukwasi unaofikia bilioni moja kwa sarafu ya eneo husika.
Ukiwa na dollar billion moja huwezi kuitwa billionea UK ambapo hela yao (pound) ni kubwa kuliko dollar.
Nb:sishangai MPUMBAVU kama wewe kuja na mada hii.
 
Kwa Tanzania hasa watu wa kanda ya Kaskazini wana matumizi mabaya sana ya neno bilionea. Ukiwa tu na uwezo wa kumiliki gari nzuri ya thamani kubwa, bus kadhaa za usafirishaji au ghorofa maeneo ya kitajiri wewe tayari umekuwa bilionea.

Tuache huu ushamba, bilionea kidunia/kimataifia ni mtu mwenye "networth"/utajiri wa dola za kimarekani bilioni moja($1b) na kuendelea, kama mtu yuko chini ya hapo huyo sio bilionea. Kwa hapa bongo bilionea anayetambulika kwa sasa ni Mo, kuna wakati Rostam Aziz pia aliingia kwenye ubilionea ila sijui kama bado yupo kwenye list.

Tanzania wengi tulio nao ni mamilionea, hawa ni watu wanaomiliki utajiri wa zaidi ya dola za kimarekani milioni 1( $1m). Tuepuke matumizi mabaya na ushamba wa neno bilionea.
Mkuu umeanza wivu.Unamfahamu "Bilionea Asigwa"?
 
yoda haya mambo ya ubilionea waachie watu wa arusha, wewe komaa na mastori ya siasa na umafia wa mr born town
 
Kuna bilionea wa kihaya pia cjui unamjua mkuu...ila dunia hii bana ni vile unapenda iwe inakupeleka hivo hivo ..ni imani yake suku moja atakuwa bilionea na uzee ule mm ni nani nisijitabirie mema hata mm ni bilionea japo hata laki sina
 
Huku kwetu kaskazini Bilionea ni mtu yoyote mwenye nyumba za kupangisha, bar na lori la mchanga.
 
Back
Top Bottom