Tufanye nini ili kupunguza athari ya upandaji wa bei za mafuta? tulaumiane?

Tufanye nini ili kupunguza athari ya upandaji wa bei za mafuta? tulaumiane?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,186
Reaction score
7,492
Kuna baadhi ya vitu vinavyotokea ambavyo viko nje ya uwezo wa mtu mmoja au kundi fulani la watu. Kwa mfano, suala la upandaji wa bei ya mafuta katika kipindi hiki cha vita ya Urusi na Ukraine liko nje ya uwezo wa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.

Kuna watu wanamlaumu Rais, Wengine serikali n.k Sasa sijui walitaka Rais amzuie Putin asivamie Ukraine au vipi? jiulize ungekuwa wewe ungeweza hilo?

Kimsingi katika jambo hili hatupaswi kulaumiana maana haitasaidia chochote. Tunatakiwa tutoe mawazo na si kupiga kelele kwamba ni nini tufanye ili kupunguza athari za upandaji bei za mafuta na hivyo kuathiri bei za vitu vingine pia.

Moja ya mapendekezo ni;-

1. Kupunguza kodi kwenye mafuta;
changamoto ya kwanza ya njia hii ni kuwa kodi kwenye mafuta ni moja ya vyanzo vya msingi vya mapato ya serikali, hivyo kuiondoa ni kuathiri vibaya mapato ya serikali hivyo wenye wazo hili wanapaswa kupendekeza mbadala ni nini, pili kodi hizo zishawekwa kwenye sheria, hivyo inabidi kubadili sheria kwanza na tatu, kama bei inapanda sana kwenye soko la dunia, hata ukiondoa kodi bado itabaki kuwa juu.

2. Wazo la pili ni la Shabiby alilotoa jana kuwa dealers wanaoweza na wanaotaka waruhusiwe kuingiza mafuta wenyewe badala ya ununuzi wa pamoja, lakini haifahamiki vizuri kuwa hii itapunguzaje bei ikiwa bei kwenye chanzo iko juu.

3. Wazo la tatu ni kukubaliana na mabadiliko ya hali halisi na kubeba yatokanayo.

4. Wazo la nne ni.......................?
5...............................................?

Kimsingi kama mtu ana mbinu anayofikiri inaweza kufanya kazi ni vizuri akatoa badala tu ya mara Kumlaumu Rais, Mara serikali n.k hawa nao ni watu, hivyo pendekeza nini kifanyike sio lawama tu, lawama hazijawahi kutatua tatizo lolote duniani.
 
Asilimia kubwa ya watu kama sio wote wanaolaumu juu ya kile kinachotokea sasa, ukiwauliza cha kufanya ni nini na faida na hasara za kuchukua hatua husika ni nini nao hawana majibu, wanalaumu tu.

Wakulaumiwa kwa haki ni Putin
 
Msitumie vyombo vya moto
Tumieni Uber, daladala, bodaboda mwendokasi

Ova
 
Msitumie vyombo vya moto
Tumieni Uber, daladala, bodaboda mwendokasi

Ova
Labda useme watu wapaki magari binafsi. Lakini ulivyovitaja navyo vya moto vile vile
 
Asilimia kubwa ya watu kama sio wote wanaolaumu juu ya kile kinachotokea sasa, ukiwauliza cha kufanya ni nini na faida na hasara za kuchukua hatua husika ni nini nao hawana majibu, wanalaumu tu.

Wakulaumiwa kwa haki ni Putin
Unapigana na matawi ya mti badala ya mizizi bwana Azizi Mussa . Chochote kinachotokea Tanzania wananchi hulaumu serikali na rais kwa sababu ya mfumo wetu wa uongozi. Mfumo wetu hauwashirikishi wananchi na badala yake unawafanya viongozi wawe ndiyo kila kitu. Na mbaya zaidi viongozi wetu wanapenda sana kusifiwa kunapokuwa na mafanikio hata kama siyo wao wameyaleta. Na kama unavyojua.... ukiishi kwa sifa, utakufa kwa lawama.
 
Unapigana na matawi ya mti badala ya mizizi bwana Azizi Mussa . Chochote kinachotokea Tanzania wananchi hulaumu serikali na rais kwa sababu ya mfumo wetu wa uongozi. Mfumo wetu hauwashirikishi wananchi na badala yake unawafanya viongozi wawe ndiyo kila kitu. Na mbaya zaidi viongozi wetu wanapenda sana kusifiwa kunapokuwa na mafanikio hata kama siyo wao wameyaleta. Na kama unavyojua.... ukiishi kwa sifa, utakufa kwa lawama.
Ni sawa. Lakini huoni hiyo haisaidiii chochote? Au lengo linakuwa ni ile kutafuta mtu uumlaumu ili upunguze stresss?
 
Back
Top Bottom