Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,096
- 4,948
Tumesikia Lissu akisema wazi tusimlaumu Waziri wa Fedha kwa sababu ni karani tu anayewelekezwa chakufanya na Rais. Nakubaliana asilimia mia moja na hoja kwa kuzingatia mambo yafuatayo;
~ Mzee Mtei alipokataa kumsikiliza Mwalimu Nyerere na kuamua kusimamia uelewa na taalum yake ilimlazimu aondoke Wizara ya fedha.
~ Wakina Kambona walipopingana na Mwalimu waliondoka si kwa sababu wakikosa hoja bali kwa sababu anayefahamu ni mmoja tu.
Hali hii imetokea enzi za Mwinyi, Mkapa kwenye ubinafsishaji, Kikwete na JPM.
Nchi za wenzetu Waziri wa Fedha anafahamika mrengo na msimamo wake kwenye uchumi na anapoteuliwa kila mwenye maarifa utabiri factors zinazoweza kufanya apimwe kama kufeli au kufaulu.
Upande wa Tanzania tukiulizwa msimamo au mwelekeo wa Waziri wa Fedha na Mawaziri wengine (except Bashe) ni vigumu kuona dira zao. Mawaziri wananeno yasiyo yao na hivyo wanashindwa kusimama. Lakini pia wanaona wakifanya kilichosahihi wanaweza kutumbuliwa kama watangulizi wao.
Najiuliza nini kifanyike kuwaondoa Mawaziri kwenye sifa ya ukarani (mpokea maagizo)?
~ Mzee Mtei alipokataa kumsikiliza Mwalimu Nyerere na kuamua kusimamia uelewa na taalum yake ilimlazimu aondoke Wizara ya fedha.
~ Wakina Kambona walipopingana na Mwalimu waliondoka si kwa sababu wakikosa hoja bali kwa sababu anayefahamu ni mmoja tu.
Hali hii imetokea enzi za Mwinyi, Mkapa kwenye ubinafsishaji, Kikwete na JPM.
Nchi za wenzetu Waziri wa Fedha anafahamika mrengo na msimamo wake kwenye uchumi na anapoteuliwa kila mwenye maarifa utabiri factors zinazoweza kufanya apimwe kama kufeli au kufaulu.
Upande wa Tanzania tukiulizwa msimamo au mwelekeo wa Waziri wa Fedha na Mawaziri wengine (except Bashe) ni vigumu kuona dira zao. Mawaziri wananeno yasiyo yao na hivyo wanashindwa kusimama. Lakini pia wanaona wakifanya kilichosahihi wanaweza kutumbuliwa kama watangulizi wao.
Najiuliza nini kifanyike kuwaondoa Mawaziri kwenye sifa ya ukarani (mpokea maagizo)?