Uchaguzi 2020 Tuiache Tume itimize jukumu lake kusimamia Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba na Sheria

Uchaguzi 2020 Tuiache Tume itimize jukumu lake kusimamia Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba na Sheria

Machomane

Member
Joined
Jul 10, 2020
Posts
6
Reaction score
4
Nimepitia baadhi ya machapisho kadhaa yakimzungumzia Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Ibara ya 74 (7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977: Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake yaliyoainishwa katika ibara hii, Tume ya Uchaguzi itakuwa ni idara huru inayojitegemea, itafanya maamuzi yake rasmi kuhusu utekelezaji wa majukumu yake kwa vikao, na mtendaji mkuu wake atakuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye atateuliwa na kufanya kazi kwa mujibu wa masharti ya Sheria iliyotungwa na Bunge.

Kifungu cha 6(1) cha Sharia ya Taifa ya Uchaguzi: Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, atateuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, kutoka miongoni mwa Watumishi wa Umma.

Ibara ya 74 (14) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977: Itakuwa ni marufuku kwa watu wanaohusika na uchaguzi kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa tuu kwamba kila mmjoja wao atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika Ibara ya 5 ya Katiba hii.

Katika Taarifa za Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, sijaona wala kusikia pahala akimsifu wala kumnadi mgombea wa chama chochote cha siasa. Hivyo machapisho yenye tuhuma dhidi ya Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ni kada wa chama fulani cha siasa si sahihi.

Tuiache Tume itimize jukumu hili la kusimamia Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba na Sheria. Mtanzania aliyejiandikisha kuwa mpiga kura atapiga kura kwa kumchagua mgombea ambaye anaamini ndiye mwenye sera zinazoshabiiana na matakwa yake.

Ninachoweza kusema Kila mmoja wetu aliyejiandikisha ifikapo tarehe 28 oktoba, akapige kura.
 
Ukweli Hujitenga ndani ya Uwongo,katika Maelezo yako Yote Umejishitaki na Kujihukumu.Mwalimu Nyerere aliwahi sema Ukweli Unatabia ya Kusimamia
 
Unajitambua mkuu?Unaelewa kuwa kwa muundo wa NEC ya sasa hivi ulivyo mwenyekiti/mkurugenzi wake ni Magufuli?
 
..kutokana na matamshi aliyoyatoa jana Mkurugenzi anatakiwa ajiuzulu ili kulinda heshima ya tume.

..kuendelea ktk nafasi yake kutawatia hofu wadau wa uchaguzi kwamba tume haitaweza kutenda haki.
 
Umejikaanga mwemyewe kwenye vifungu ulivyoweka hapo!

Vipi kama Mkurugenzi huyo angetoka na kusema "watanzania wanataka maendeleo ya watu na sio vitu tu"!
Akaongeza,"watanzania hawataki ndege ziwe kipaumbele"

Unadhani angekuwa salama?
 
Unajitambua mkuu?Unaelewa kuwa kwa muundo wa NEC ya sasa hivi ulivyo mwenyekiti/mkurugenzi wake ni Magufuli?
Tundu Lissu waliomtuma kuihujumu Nchi yetu kwa kumfungia Mtambo wa kutumia taarifa huko huko waliko mtuma umejikologa. Mungu hadhihaikiwi.
Tulianza na Mungu, Mungu hajatuacha Watanzania. Tundu ni hatariii saaana kwa usalama wa Afrika.
 

Attachments

  • VID-20200928-WA0017.mp4
    6.6 MB
Tundu Lissu waliomtuma kuihujumu Nchi yetu kwa kumfungia Mtambo wa kutumia taarifa huko huko waliko mtuma umejikologa. Mungu hadhihaikiwi.
Tulianza na Mungu, Mungu hajatuacha Watanzania. Tundu ni hatariii saaana kwa usalama wa Afrika.
Unaongea pumba gani?Sisi tunajadili juu ya tume wewe inakuaje unaleta mada tofauti?Una akili timamu?Unajitambua?Umelogwa?
 
Back
Top Bottom