Tuinyooshe Katiba kabla ya kunyoosha maslahi Tanzania, Zanzibar na Tanganyika ndani ya Muungano

Tuinyooshe Katiba kabla ya kunyoosha maslahi Tanzania, Zanzibar na Tanganyika ndani ya Muungano

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ili kuyafafanua masilahi ya Zanzibar ndani ya Muungano lazima kwanza useme kweli tupu ni kwanini Tanganyika haipo Tanzania lakini Zanzibar ipo Tanzania. Pili, useme kweli tupu kama Zanzibar ni sehemu ya Tanzania ama ni nchi. Katiba lazima inyooshe kuhusu maswali haya maana ndiyo yatakayotumika kwenye hata mgawanyo wa majukumu na masilahi ya Zanzibar na Tanganyika ndani ya Muungano.

Kama Zanzibar ni nchi ndani ya Muungano basi Katiba lazima iirudishe Tanganyika kwanza kabla ya kunyoosha maslahi ya Zanzibar kikamilifu. Na kama Zanzibar ni sehemu tu ya Tanzania basi lazima nchi ya Zanzibar iondoke ndani ya Tanzania, maana Jina la Tanzania tayari limeibeba Zanzibar na Tanganyika.

Kama Zanzibar ni nchi basi maslahi yake ndani ya Muungano lazima yaende kikamilifu kama nchi mbili kwenye Muungano, lakini kama ni sehemu ya Tanzania basi masilahi yake lazima yafuate uwiano wa mahitaji, uhitaji na idadi ya watu walioko Zanzibar. Yaani, tuseme Zanzibar, Tanga, Mwanza, Dodoma nk.

Kama Zanzibar ni nchi basi mtu kutoka Zanzibar hawezi kuwa Rais Tanganyika, Zanzibar na Tanzania na mambo yake yote kwa wakati mmoja kama ilivyo kwa mtu kutoka Bara asivyoweza kuwa Rais wa Tanzania na Zanzibar na mambo yao yote kwa wakati mmoja. Yaani Rais Mtanganyika kuna mambo hayaguzi Zanzibar, inatakiwa iwe hivyo hivyo pia Rais Mzanzibar awe na mambo ya Tanganyika yasiyo ya Muungano asiyaguse pia.

Wenzetu CCM hasa bara inaonekana hamna jicho la moyoni la kuona kisichoonekana leo kinachokuja kesho. Mnatizima ya leo kila siku hamuoni ya kesho. Afadhali kidogo CCM Zanzibar Wana muono wa mbali sana na taifa lao ndani ya Muungano na matokeo yake Leo hii ni dhahiri.

Ushauri wangu kwa maoni yangu, jambo la kwanza Kutimiza sambamba na mambo mengine ni unyooshaji wa Katiba haraka iwezekavyo ili kuondosha kero za Muungano.
 
Hapo uliposema mtu kutoka Zanzibar anaweza kuwa Rais Bara, lakini mtu kutoka Bara hawezi kuwa Rais Zanzibar ndio panaonesha huu muungano feki unavyolazimishwa kuwepo kwa kubembelezwa badala ya matakwa ya pande zote mbili.

Tunawalea wazanzibari kama watoto wakati sioni chochote cha maana tunachopata toka kwao.
 
Ili kuyafafanua masilahi ya Zanzibar ndani ya Muungano lazima kwanza useme kweli tupu ni kwanini Tanganyika haipo Tanzania lakini Zanzibar ipo Tanzania. Pili, useme kweli tupu kama Zanzibar ni sehemu ya Tanzania ama ni nchi. Katiba lazima inyooshe kuhusu maswali haya maana ndiyo yatakayotumika kwenye hata magawanyo wa majukumu na masilahi ya Zanzibar na Tanganyika ndani ya Muungano.

Ndugu Kavulata

Kwanza nakuomba, nakunasihi, nakushauri ujuwe kwamba Mtangavyika leo hii hana kwao anakoweza kujivunia. hili lilianza tangia pale 1964 kwa utashi wa mtu mmoja tu alipoamua kuiuwa Tanganyika. Leo Tanganyika ni taboo hata kutajwa ndani ya siasa. Mtanganyika hana haki hata ya kujitambua uasili wake.

Kumbuka kwamba Tanzania si nchi bali ni JINA LA KUPANGA ambalo lilitokana na muungano baina ya Zanzibar na Tanganyika, yaani kabla ya hapo hakukuwa na nchi iitwayo Tanzania. Pia kumbuka kwamba kwasababu Tz si nchi asilia, jina hilo la kupanga linaweza kufutika kama yalivo futika majina ya kupanga ya nchi kama vile Yugoslavia, USSR, Checkslovakia. Kwahivyo kwanza inakupasa kufahamu kiundani na kiukweli hakuna uzalendo wa Tanzania maana kule Zanzibar muulize mzawa yoyote, "wewe ni nani?" jawabu litakuwa "mimi ni Mzanzibari" nakuhakikishia hakuna Mzawa wa anzibar anayejiita, anayejitambua, anayejithamini kama Mtanzania akiwa ndani ya zanzibar au hata akiwa Tanganyika. Lakini ukija Tanganyika ukamuliiza mzawa wa Tanganyika "wewe ni mtu wa wapi?" atakujibu "mimi ni mtanzania".

Wanganyika, ndugu zenu waliopenya kwenye tundu ya sindano wanakubabaisheni, munadanganywa, mnafanywa watoto, munafanywa wajinga, mfano munaambiwa hili ni suala la muungano na hili ni sualal la Zanzibar, sisikii mtu yoyote kuhoji, jee ikiwa si suala la muungano wala si suala la zanzibar sasa hilo litakuwa suala la wapi? Unajua ukiiliza suala hilo utajibiwa nini, kama hukuwekwa kizuizini basi utajibiwa utumbo tu maana hakuna jawabu kwa suala hilo.

Watangayika muko kwa mfano wa refugees katika ardhi yenu wenyewe. Kwahivo kama ulivosema la maana zaidi ni kuhakikisha Utangayika unafufuliwa. Na raha mtu ni kuwa na kwao anakoweza kujivunia.

Ili mtu ajulikane kwao ni wapi, passport ziseme Tanzania na chini yake paandikwe Tanganyika au Zanzibar.
 
Ndugu Kavulata

Kwanza nakuomba, nakunasihi, nakushauri ujuwe kwamba Mtangavyika leo hii hana kwao anakoweza kujivunia. hili lilianza tangia pale 1964 kwa utashi wa mtu mmoja tu alipoamua kuiuwa Tanganyika. Leo Tanganyika ni taboo hata kutajwa ndani ya siasa. Mtanganyika hana haki hata ya kujitambua uasili wake...
Bahati nzuri au mbaya, Zanzibar haihusiki na kuifuta Tanganyika, ni wa Tanganyika wenyewe kwa sababu na mitego iliyowanasa wenyewe. Lakini hili linazungumzika, turejee tulipokosea na kukosea kwetu isiwe sababu ya kuwanyima wengine wanaojiita Bua masilahi yao kama hapo.

Mbaya wetu kaka kwenye hili ni CCM Bara. Wana agenda ambayo itatufikisha pabaya kwakuwa wao wanalenga kuwa itokee siku moja kuwe na Serikali moja tu Tanzania, thubuuutu!!!! Yaani Serikali ya Zanzibar ifutike, kasema Nani!
 
Watanganyika wenyewe waliamua hivyo.
 
Bahati nzuri au mbaya, Zanzibar haihusiki na kuifuta Tanganyika, ni wa Tanganyika wenyewe kwa sababu na mitego iliyowanasa wenyewe. Lakini hili linazungumzika, turejee tulipokosea na kukosea kwetu isiwe sababu ya kuwanyima wengine wanaojiita Bua masilahi yao kama hapo. Mbaya wetu kaka kwenye hili ni CCM Bara....
Sasa Shekhe,vipi maoni yako ni nini

?;Je, ulazima wa kuwa na Serikali tatu upo au haupo?.
 
Sasa Shekhe,vipi maoni yako ni nini

?;Je, ulazima wa kuwa na Serikali tatu upo au haupo?.
Lazima Tatu au moja, nothing less nothing more. Hata Katiba ya Jamhuri na ile ya Zanzibar haziongei lugha moja kwenye hili. Tumuombe kwa unyenyekevu Rais wetu asukume mbele unyooshaji wa Katiba ya Jamhuri kabla ya kusukuma masilahi ya upande mmoja tu wa Muungano.
 
Sasa Shekhe,vipi maoni yako ni nini

?;Je, ulazima wa kuwa na Serikali tatu upo au haupo?.
Hata waasisi wetu wa muungano wazee Nyerere na Karume inaonekana hawakuwa na common vision na muundo wa Muungano. Inavyoonekana Mzee Nyerere alitaka serikali moja na ndicho kilichomfanya akaifyeka Tanganyika, Mzee Karume inaonekana kuwa alikuwa na vision na muundo wa serikali tatu. Wazanzibar sio wanafiki wala wavivu bila kujali itikadi zao walilisimamia wazo la mzee wao la kuibakiza serikali yao tukufu hadi leo, lakini watanganyika hawakushuhulika na kulisukuma wazo la mzee wao la serikali moja, badala yake kundi ndogo la wana CCM lilikuwa linatumia janjajanja ya kutaka kuifuta serikali ya Zanzibar ndani ya muungano.

Tume ya Warioba ilikusanya maoni ya wananchi Tanzania nzima kuhusu katiba na imethibitisha kuwa watanzania wanataka serikali tatu, lakini kundi lilelile dogo la wanaCCM linapingana na maoni ya wananchi ya serikali tatu na kutaka kuendelea za shida ileile ya serikali mbili.

Kadiri lile kundi la wazee waliokuwepo wakati wa Mwl Nyerere na Mzee Karume linavyozidi kumomonyoka ndiyo ndoto ya serikali moja au mbili inavyozidi kuwa impossible. Tutabaki hivi hadi lini? Kubaki hivi tulivyo inawezekana kabisa milele lakini asitokee mtu anaedai kitu kutoka upande wowote. Maana hata majimbo ya Marekani pia yana malalamiko yao juu ya serikali ya muungano lakini hakuna anaepewa wala kulipwa chochote. Yaani kama walikosea waazilishi basi wamekosea kwa niaba yao wote.
 
Back
Top Bottom