Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 38,283
- 97,793
Lengo la dini ni kuhamasisha waumini wake kuishi maisha ya upendo na yenye nidhamu kwenye jamii. Tunafundishwa kutambua yapi ya kufanya (mema) na yapi ya kutokufanya (mabaya yenye machukizo kwetu na kwa Mwenyezi Mungu).
Inashangaza sana watu wenye utashi wa kutambua mema na mabaya wanafanya mambo ambayo ni kinyume na imani. Najua hatujakamilika kama binadamu, kuna mambo ni ngumu sana kutokufanya hata kama tunakosea, lakini kuna mambo mengine tunafanya hata shetani na uovu wake anashangaa ni nini hiki.
Unashiriki ibada kila iitwapo leo na hutaki na huna kusudio la kubadilika, huko kwenye ibada unaenda kufanya nini kama hautaki kubadilika na kuishi maisha ya upendo?
Kutwa kucha mtu upo na kukimbizana na mambo ya kiimani lakini kwenye jamii unaishi maisha ya ajabu na yenye kuwaumiza wengine bila kujali chochote mpaka watu wanajiuliza hivi huko kwenye nyumba za ibada huwa anafuata nini, au ndio anayofundishwa huko? Matendo yako yaendane na imani yako, wengi wanakuwa vielelezo vibaya kwa imani wanazoamini.
Kuna watu ni waumini wazuri sana na wanyenyekevu huko kwenye dini ila ndio vinara wa kutelekeza watoto na familia, unyanyasaji, uchonganishi, kukwepa majukumu, uchawi n.k.
Tuishi upendo tunaofundishwa kila leo kwenye imani zetu.
Jumapili njema.
Inashangaza sana watu wenye utashi wa kutambua mema na mabaya wanafanya mambo ambayo ni kinyume na imani. Najua hatujakamilika kama binadamu, kuna mambo ni ngumu sana kutokufanya hata kama tunakosea, lakini kuna mambo mengine tunafanya hata shetani na uovu wake anashangaa ni nini hiki.
Unashiriki ibada kila iitwapo leo na hutaki na huna kusudio la kubadilika, huko kwenye ibada unaenda kufanya nini kama hautaki kubadilika na kuishi maisha ya upendo?
Kutwa kucha mtu upo na kukimbizana na mambo ya kiimani lakini kwenye jamii unaishi maisha ya ajabu na yenye kuwaumiza wengine bila kujali chochote mpaka watu wanajiuliza hivi huko kwenye nyumba za ibada huwa anafuata nini, au ndio anayofundishwa huko? Matendo yako yaendane na imani yako, wengi wanakuwa vielelezo vibaya kwa imani wanazoamini.
Kuna watu ni waumini wazuri sana na wanyenyekevu huko kwenye dini ila ndio vinara wa kutelekeza watoto na familia, unyanyasaji, uchonganishi, kukwepa majukumu, uchawi n.k.
Tuishi upendo tunaofundishwa kila leo kwenye imani zetu.
Jumapili njema.