Vituka
JF-Expert Member
- Nov 9, 2011
- 2,266
- 1,264
Sijui kama ndio utaratibu wa sasa au vipi, nina takribani miezi 4 toka nimuanzishe shule mtoto mmoja (STD 1). Kila siku anatakiwa apeleke shilingi 300 kama pesa ya tuition. Nilijaribu kuulizia walimu wake muda gani wanasoma tuition nikaambiwa wanaingia darasani saa 1:30, wanatoka saa4, then saa4 hadi 6 wanakuwa tuition na ni lazima wanafunzi wote wasome tuition, na siyekuja na hiyo pesa atapata mikwayu ya kutosha.
Kwangu mimi sh 300 sio tatizo sana ila nahoji uhalali wa kuwatoza watoto pesa hiyo ili wasome tuition kwa muda huo wa masaa mawili!! Kama kuna anayejua kuhusu hili naomba anielimishe tafadhali.
Kwangu mimi sh 300 sio tatizo sana ila nahoji uhalali wa kuwatoza watoto pesa hiyo ili wasome tuition kwa muda huo wa masaa mawili!! Kama kuna anayejua kuhusu hili naomba anielimishe tafadhali.