Tujadili kwa uwazi kisheria kuhusu kujiuzulu kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM bara Abdulrahman Kinana. Sheria, Katiba na Kanuni zihusike

Kumbuka Kinana alishajiuzulu wakati wa Shujaa Magufuli

Mpendwa Wetu Mh Mwenyekiti Dr Samia alimuomba tu arejee kwa muda so hakuwa na mkataba wa kikatiba tena

Ahsante πŸ˜‚
Hakuwa na Mkataba Wa kikatiba πŸ€”πŸ€”
Seriously kabisa..
Nataka Kuamini kama Unatania..

Kamati iliyopitisha Jina Lake ilikuwa ni kamati ya CC na wala haouchaguliwa na Mwenyekiti..

Kuna vitu huwa tunadanganyana Mwenyekiti Hana maamuzi yeye kama Yeye Kuamua Kipi kifanyike na Kipi kisifanyike ila Kamati kuu pamoja na CC ndo yenye maamuzi..

Hakuna kiongozi ambaye yupo Pasipo kuwepo kikatiba isipokuwa Naibu waziri Mkuu pekeee
 
Thats True!
 
Tatizo kubwa la Malkia ni ku "underate serious things witkout a proper timing of events"

Hili ni kosa kubwa la kisiasa ambalo aliliifanya mtangulizi wake. Anachokifanya hivi sasa alipaswa kufanya pale awali tu alipokabidhiwa uongozi mwaka 2021.

Believe me. Kwa uamuzi wake huu wa sasa amekwisha panua wigo wa mahasimu wake, ndani na nje ya chama chake.
 
Katika mambo yote ya kujadili umeona hilo?
Uchawa shida sana.
 
Chama Kinaruhusiwa Kujenga Nchi bila kuvunja Katiba ya Chama wala Kanuni za Chama
Mtiririko unafuatwa kama amejiuzulu, sasa yeye amefurushwa mtiririko wa nini?
Au labda niulize kwanza, je kama amefurushwa katiba inasemaje kuhusu kuchaguliwa mwingine, ni mtiririko huo huo au kuna mtiririko wake
 
Naona anakosa Washauri wa Kisiasa Na hiyo inaweza kumuweka mahali ambapo sio pazuri
 
Mtiririko unafuatwa kama amejiuzulu, sasa yeye amefurushwa mtiririko wa nini?
Au labda niulize kwanza, je kama amefurushwa katiba inasemaje kuhusu kuchaguliwa mwingine, ni mtiririko huo huo au kuna mtiririko wake
Akifurushwa Linapelekwa Jina tu siku ya Mkutano mkuu, Lakini Mind you Mwenyekiti hana Mamlaka ya Kumfurusha Makamu wake kwa sababu hakumchagua Yeye..
maana Njia iliyotumika Kumchagua Mwenyekiti ni njia iliyotumika Kumchagua Makamu🀣🀣
 
Kamati Kuu ni ya Mwenyekiti Ndio sababu kila Mwenyekiti anayeingia huamua idadi ya Wajumbe wa Kamati Kuu anayoitaka yeye πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Msomali na Mkwere ni washirika wa muda mrefu,lakini hii misheni inaonekana msomali alikuwa peke yake na Vijana wake.
Mkwere yupo kimyaa anapiga trip na SGR tu na mwanae kaukwaa uwaziri.
Maisha Hisabati haya.
Msomali ameng'oka,Makamu Mwenyekiti hajiuzulu ghafla hivyo na uchaguzi upo mlangoni.
 
Katika mambo yote ya kujadili umeona hilo?
Uchawa shida sana.
Hapo Uchawa Uko wapi?
Uko sawa Kiakili kweli Kijana?

Ulitaka Nijadili Kuhusu Mapenzi au Wasanii wenu au Simba na Yanga??

Huku nikiacha Tunu ya Nchi yangu au Mambo muhimu katika nchi yangu ambayo mimi ndiyo mnufaika Mkuu yakinipita bila Kuhoji kwaninu yametokea?

Ulitaka Nisihoji nisubiri mpaka mambo yatakapoharibika ndo nijifanya kuhoji kama Mnafiki?

Kijana Una Elimu gani?
Maana Kwa uwezo wako wa Kufikiri hufai hata kuwa na Elimu ya Darasa la Saba maana Mh Msukuma Akiwa Bungeni anakuzidi Ufikiri wewe!

na hata Mjukuu wangu anayesoma Form one anakuzidi uwezo wa Kufikiri na Kuchambua Mambo kwa upana..

Unajua kwanini Vijana wa Tanzania Mnaonekana Wapuuzi Kuliko Vijana wa Nchi zingine??

Kwasababu Vijana wa Tanzania hamna Critical Intellectual Thinking mnachowaza Nyinyi ni kufanya Kitu bila kufikiria wala Reasoning na ndo maana Vijana mnaburuzwa sana...

Unakuta Mtu kama wewe asubuhi unawaza Mpira, Mchana unawaza Diamond na Alikiba,Usiku unawaza Demu wako Au betting!

Unajiuliza Ni muda gani kama Kijana utapata Kuchukua Vitabu usome upanue Akili na ufahamu wako au upitie Sheria za Nchi ili upate ufikiri wa kulinda Rasilimali zako??

Napata Hofu na Vijana wengi sana maana Wengi mnayatamani Maarifa ila Maarifa yana Mbio kuliko Nyinyi..

Wengi ni Weupe sana Kichwani, Jitahidini Kujiengage kwenye Midaharo na Kujadili hoja mtajua kwanini sisi wakubwa Wenu tuna uchungu na nchi na Kwanini tunaona Kama taifa tunaitaji kushauri ili mambo yaende sawa..

Asante na karibu
 
Well said
 
Kamati Kuu ni ya Mwenyekiti Ndio sababu kila Mwenyekiti anayeingia huamua idadi ya Wajumbe wa Kamati Kuu anayoitaka yeye πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Idadi ya wajumbe ipo kikatiba Mkuu..
Soma Katiba ya CCM ibara ya 102 ibara ndogo ya (1) kipengele( a )mpaka (x)

Wajumbe wanafahamika hawaongezwi au kupunguzwa
 
haupo utaratibu uliokiukwa na komrade A. Kinana katika kuomba kupumzika umakamu mwenyekiti wa chama bara kwa kujiuzulu..

heshima,
mila, desturi na utamaduni wa CCM katika kung'atuka uongozini daima daima utaenziwa na kamwe hakuna sababu ya mwanaccm kua na mashaka juu ya uamuzi wa comrade Kinana na wengineo kuomba kupumzika uongozi wa chama..

CCM ina hazina ya wanachama shupavu, madhubuti na wenye uwezo kushika nafasi ya comrade Kinana na CCM ikasonga mbele......

ni muhimu maandiko kama haya tukayatumia academically, kuongeza uelewa na ufahamu wa kutosha juu ya taratibu, kanuni na sheria za CCM katika katika kujaza nafasi zilizowazi kwa sababu mbalimbali na wanachama wake πŸ’
 
Ni kweli kabisa Comrade ila Utaratibu uliotumika kwa Kuridhia Ndo unaojadiliwa hata kama Jasiri kinana kajiuzulu kwa Barua ila mwenyekiti wa CCM sio excutive ila Ni rank ya Juu ya uongozi kwahiyo hana Maamuzi kikatiba na Kikanuni na hana Mandatory ya Kuridhia Kwake kujiudhuru ilibdi atangaze kwa Umma Kupokea Barua ya Kujiuzulu..

Na kiitishwe kikao cha Chama Cha Dharura Na wajumbe walidhie
 
Michezo ya kihuni ya sa100 , amemfanyia job,chongol,Mzee Tembo,
Uko Zako nyumbani unasoma gazeti, mara mkeo anakuja kukuambia ameona mtandaoni umeandika barua ya kujihuzulu
Unabaki hii😲.
 
Michezo ya kihuni ya sa100 , amemfanyia job,chongol,Mzee Tembo,
Uko Zako nyumbani unasoma gazeti, mara mkeo anakuja kukuambia ameona mtandaoni umeandika barua ya kujihuzulu
Unabaki hii😲.
🀣🀣🀣🀣
Kama nape Hapatikani kwenye simu, Wala account zake zote..
Na amedeactivate Account zote kwa Muda
Sasa sijui pressure iko ngapi yule jamaa🀣🀣
 
NAPE, JANUARY NA KINANA karma inawahukumu! Waliiba kura za mzee LOWASA 2015 mchana kweupe.

Na Bado!.
 
NAPE, JANUARY NA KINANA karma inawahukumu! Waliiba kura za mzee LOWASA 2015 mchana kweupe.

Na Bado!.

Paul Makonda yeye vipi? Ni karma au ni kawaida tu?

Hivi anaumwa, yuko likizo au na yeye kahifadhiwa Zahanati ya MZENA?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…