Tujadili mapungufu ya Sera yetu ya Viwanda. Unadhani ina mapungufu gani?

Tujadili mapungufu ya Sera yetu ya Viwanda. Unadhani ina mapungufu gani?

EllySkyWilly

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
2,204
Reaction score
2,085
Habari za leo wakuu,

Uzii huu utakuwa maalum kuijadili sera yetu ya viwanda.

Bila kutukana wala kumnyoshea mtu yeyote kidole, naomba kila mmoja atoe maoni yake.

Mada: Wewe unahisi sera yetu ya viwanda ina mapungufu gani?

Zingatia ili taifa letu liweze kuendelea linahitaji kuwa na sera bora ya viwanda. Sera bora ya viwanda inatakiwa kutoa dira ya maendeleo ya uchumi wa taifa.

Zingatia muda mwingine sera inaweza kuchukua mda mrefu kuleta matokeo chanya.

Sote tumeona jitihada zinazo fanywa na serikali yetu ya awamu ya tano na sita katika kutoa motisha kwa watanzania kujenga na kuanzisha viwanda.

Lakini pia tumeona jinsi ambavyo serikali imetumia jitihada kufufua taasisi za umma. Serikali imefufua ATCL, TTCL, n. k.

Zingatia mfumo wowote wa biashara ya kiuchumi hauwezi kufanya kazi vizuri bila serikali kuingilia. Hivyo ni lazima serikali nayo iingie kwenye mfumo huo ili kazi iende vizuri. Ndio sababu mnaona kwenye usafiri wa anga mnaiona serikali kupitia ATCL, kwenye mawasiliano mnaiona serikali kupitia TTCL, n.k.

Serikali ikiwa karibu na mfumo wa kiuchumi ni rahisi kupata taarifa zinazo husu mzunguko mzima wa kiuchumi, kasoro na matatizo mbalimbali. Mimi nadhani pia kuiachia sekta binafsi iendeshe mfumo mzima wa uchumi peke yake sio vizuri na swala hili lina athari kiuchumi.

Nikija kwenye swala la mchakato mzima wa sera yetu ya viwanda. Sera yetu ni nzuri sana na itatuletea faida nyingi sana huko mbeleni. Ila nilikua napenda ili sera yetu ifanikiwe asilimia 100 hasa kwenye swala la ujenzi wa viwanda, nadhani ingechagua baadhi ya viwanda vile ambavyo tunaona tunaweza kuviendesha vizuri na vikatatuletea faida nyingi kama vile utoaji wa ajira nyingi, mapato mengi na bidhaa nyingi.

Nilikua nasoma jarida moja jinsi ambavyo china wanapigana kukuza uchumi wao, wao katika sera yao ya viwanda wamechagua utengenezaji wa magari ya umeme. Hivyo nguvu yao yote wameilekeza kwenye uwekezaji wa viwanda vya magari ya umeme, utafiti na ubunifu katika viwanda vya magari ya umeme.

Naomba niishie hapa.

Hivyo ndugu yangu kama una maoni dondosha maoni yako

Usitukane.

Hiki ni moja ya kiwanda katika Tanzania yetu ya viwanda.

 
Tutatue kwanza kero ya umeme, maji ndo tujadili kuhusu viwanda vinginevyo tunapotezeana muda tu.
 
Siku hizi sisikii zile mbwembwe za Tanzania ya viwanda, sijui viwanda 100@mkoa. Mlipojiandaa kufanya uchaguzi wa wizi mbona hamkutaka ushauri?

Mmekwama huko ndio mnajifanya mnataka ushauri. Itaneni mshauriane wenyewe kuhusu viwanda, kama mlivyoitana kupanga wizi wa kura. Sisi tunataka viwanda vijana waajiriwe fullstop.
 
Siku hizi sisikii zile mbwembwe za Tanzania ya viwanda, sijui viwanda 100@mkoa. Mlipojiandaa kufanya uchaguzi wa wizi mbona hamkutaka ushauri? Mmekwama huko ndio mnajifanya mnataka ushauri. Itaneni mshauriane wenyewe kuhusu viwanda, kama mlivyoitana kupanga wizi wa kura. Sisi tunataka viwanda vijana waajiriwe fullstop.
Kweli kabisa.
 
Siku hizi sisikii zile mbwembwe za Tanzania ya viwanda, sijui viwanda 100@mkoa. Mlipojiandaa kufanya uchaguzi wa wizi mbona hamkutaka ushauri? Mmekwama huko ndio mnajifanya mnataka ushauri. Itaneni mshauriane wenyewe kuhusu viwanda, kama mlivyoitana kupanga wizi wa kura. Sisi tunataka viwanda vijana waajiriwe fullstop.
Mkuu Sisi sote ni waTanzania, tuweke vyama pembeni tupige kazi sasa.
 
Warekebishe mfumo wao wa Kodi na TOZO mbali mbali.

1. Wapewe nafuu Angalau ya mwaka 1 wa matazamio wa kulipa Kodi.

Sio ile ukishakata TIN, uanze kulipa Kodi wakati ata bidhaa zenyewe hujaanzakuzalisha.

2. Warekebishe mfumo wao wa VAT.
Sio ile Kila mahali wanakula vat TU.
-Kwenye mashine unakatwa VAT,
-ukipakia mzigo kupeleka GODOWN, fuso linakatwa VAT.
-Ukifikisha GODOWN, godown linalipiwa VAT.
- Ukitoa GoDOWN kupeleka dukani, Dukan nako ulipie VAT.

Yaan Unajikuta inakua Usumbuf juu ya usumbuf mpk Mtu anakata tamaa ya biashara.
 
Mimi sijawahi kuisoma popote hiyo sera wala sijui inapatikana wapi naomba mwenye nayo atuwekee hiyo sera tuisome halafu tujadiliane
 
Weka hapa hiyo Sera ya Viwanda tuisome, au andika kwa ufupi inaeleza nini.
 
Hii sera haiwezi fanikiwa kwenye mfumo wa ujamaa. Yafuatayo muhimu Ili sera ya viwanda ifanikiwe.
. Ruhusa mzunguko wa pesa mtaani Ili kuongeza uwezo wa watu kununua anayekula mara 4 kwa wiki ( ukila leo kesho unaruka Hadi kesho kutwa sababu ya ukosefu wa kipato) amudu kula milo 3 kwa siku.
.Fungua mipaka iwe wazi watu wazalishe wawezavyo wauze nje.
.punguza au ondoa kabisa Kodi zisizo lazima.
 
Sera ya viwanda upingana na sera ya matajiri kutakiwa waishi kishetani.
Lengo kuu la kusomesha watu namba ni kuuwa uchumi wa nchi. Ili wote wawe masikini ili watawaliwe kwa urahisi
 
Habari za leo wakuu,

Uzii huu utakuwa maalum kuijadili sera yetu ya viwanda.

Bila kutukana wala kumnyoshea mtu yeyote kidole, naomba kila mmoja atoe maoni yake.

Mada: Wewe unahisi sera yetu ya viwanda ina mapungufu gani?

Zingatia ili taifa letu liweze kuendelea linahitaji kuwa na sera bora ya viwanda. Sera bora ya viwanda inatakiwa kutoa dira ya maendeleo ya uchumi wa taifa.

Zingatia muda mwingine sera inaweza kuchukua mda mrefu kuleta matokeo chanya.

Sote tumeona jitihada zinazo fanywa na serikali yetu ya awamu ya tano na sita katika kutoa motisha kwa watanzania kujenga na kuanzisha viwanda.

Lakini pia tumeona jinsi ambavyo serikali imetumia jitihada kufufua taasisi za umma. Serikali imefufua ATCL, TTCL, n. k.

Zingatia mfumo wowote wa biashara ya kiuchumi hauwezi kufanya kazi vizuri bila serikali kuingilia. Hivyo ni lazima serikali nayo iingie kwenye mfumo huo ili kazi iende vizuri. Ndio sababu mnaona kwenye usafiri wa anga mnaiona serikali kupitia ATCL, kwenye mawasiliano mnaiona serikali kupitia TTCL, n.k.

Serikali ikiwa karibu na mfumo wa kiuchumi ni rahisi kupata taarifa zinazo husu mzunguko mzima wa kiuchumi, kasoro na matatizo mbalimbali. Mimi nadhani pia kuiachia sekta binafsi iendeshe mfumo mzima wa uchumi peke yake sio vizuri na swala hili lina athari kiuchumi.

Nikija kwenye swala la mchakato mzima wa sera yetu ya viwanda. Sera yetu ni nzuri sana na itatuletea faida nyingi sana huko mbeleni. Ila nilikua napenda ili sera yetu ifanikiwe asilimia 100 hasa kwenye swala la ujenzi wa viwanda, nadhani ingechagua baadhi ya viwanda vile ambavyo tunaona tunaweza kuviendesha vizuri na vikatatuletea faida nyingi kama vile utoaji wa ajira nyingi, mapato mengi na bidhaa nyingi.

Nilikua nasoma jarida moja jinsi ambavyo china wanapigana kukuza uchumi wao, wao katika sera yao ya viwanda wamechagua utengenezaji wa magari ya umeme. Hivyo nguvu yao yote wameilekeza kwenye uwekezaji wa viwanda vya magari ya umeme, utafiti na ubunifu katika viwanda vya magari ya umeme.

Naomba niishie hapa.

Hivyo ndugu yangu kama una maoni dondosha maoni yako

Usitukane.
Mimi awali ya yote naomba kufahamishwa Kama ipo halisi ,kwani yaweza kuwa mtazamo wangu hauko sawa.
 
Jiwe alivyokuwa Hamnazo utasikia.

WAPINZANI WAMETUKWAMISHA SANA , WAMETUCHELEWESHA SANAA.

SHWAIN
 
Back
Top Bottom