SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Kutokana na wingi wa magoli, naona hatujapata muda hasa wa kuyazungumzia vizuri ubora wa magoli waliyofunga Simba. Nimeona ni vizuri tulijadili hili.
Kwa upande wangu nitazungumzia hasa magoli mawili.
Goli la 6 ni moja ya magoli bora niliyowahi kuona timu ya Tanzania inafunga. Angalia wingi na ubora wa pasi zilivyokuwa zinapigwa kwa usahihi na kasi kuelekea goli lile na jinsi Chama alivyomalizia. Draft iliyochezwa pale utaiona tu kwa best teams duniani.
Angalia goli la 5 la Jean Baleke. Najua wengi ikiwemo mimi tulikuwa tunaona kama Baleke alikuwa na kauchoyo fulani kutompa mpira Chama apate hat trick pale, na Chama alikuwa anauomba mpira kweli. Nimekuja kuangalia tena, kumbe angempa mpira Chama pale ingekuwa offside na inahitaji umakini mkubwa kwa mchezaji kutambua hilo na kufanya maamuzi magumu. Lakini pia angalia utulivu wa Baleke na jinsi alivyopiga mpira kwenye tight angle lakini akiwa na almost uhakika wa kufunga. Nimeshawahi kusema Baleke anafungaga magoli magumu sana. Baleke ni silent killer!
Kuhusu Denis Kibu. Nashangaa kuna mcha-mbuzi juzi nimemsikia akisema Kibu hakucheza vizuri. Goli la pili lilitokana na shuti kali la Kibu kupanguliwa, mpira ukamfikia Baleke akafunga. Goli la 4 la Kanoute pia lilitokana na shuti la Kibuku kupanguliwa pia ndiyo mpira ukaenda kwa Saido aliyempasia Chama akamsogezea Kanoute. Kibu anacheza mpira sahihi kwa mahitaji ya timu sasa hivi.
Kwa upande wangu nitazungumzia hasa magoli mawili.
Goli la 6 ni moja ya magoli bora niliyowahi kuona timu ya Tanzania inafunga. Angalia wingi na ubora wa pasi zilivyokuwa zinapigwa kwa usahihi na kasi kuelekea goli lile na jinsi Chama alivyomalizia. Draft iliyochezwa pale utaiona tu kwa best teams duniani.
Angalia goli la 5 la Jean Baleke. Najua wengi ikiwemo mimi tulikuwa tunaona kama Baleke alikuwa na kauchoyo fulani kutompa mpira Chama apate hat trick pale, na Chama alikuwa anauomba mpira kweli. Nimekuja kuangalia tena, kumbe angempa mpira Chama pale ingekuwa offside na inahitaji umakini mkubwa kwa mchezaji kutambua hilo na kufanya maamuzi magumu. Lakini pia angalia utulivu wa Baleke na jinsi alivyopiga mpira kwenye tight angle lakini akiwa na almost uhakika wa kufunga. Nimeshawahi kusema Baleke anafungaga magoli magumu sana. Baleke ni silent killer!
Kuhusu Denis Kibu. Nashangaa kuna mcha-mbuzi juzi nimemsikia akisema Kibu hakucheza vizuri. Goli la pili lilitokana na shuti kali la Kibu kupanguliwa, mpira ukamfikia Baleke akafunga. Goli la 4 la Kanoute pia lilitokana na shuti la Kibuku kupanguliwa pia ndiyo mpira ukaenda kwa Saido aliyempasia Chama akamsogezea Kanoute. Kibu anacheza mpira sahihi kwa mahitaji ya timu sasa hivi.