Tujenge 'mentality' mpya ile ya Serikali haipo kwa ajili ya faida bali kutoa huduma nafikiri ndio inaua mashirika ya Umma

Tujenge 'mentality' mpya ile ya Serikali haipo kwa ajili ya faida bali kutoa huduma nafikiri ndio inaua mashirika ya Umma

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Kuna mtazamo ambao umejengeka kwamba Serikali Haina lengo la kutengeneza faida bali kutoa huduma, mtazamo huu Kwa uono wangu hafifu nafikiri ndio chanzo kikubwa Cha baadhi ya mashirika kushindwa kujiendesha na kupelekea kubinafsishwa ama kuingia ubia na sekta binafsi.

Badala ya kuwa na mtazamo wa namna hii kwamba Serikali haipo Kwa ajili ya kutengeneza faida bali kutoa huduma, kwanza kabisa mtazamo huu ubadilishwe, Serikali ianze kujikita katika kutoa huduma na kutengeneza faida.

Serikali iwekeze Kwa lengo la kupata faida kwa namna hii itajikita katika kutoa huduma bora zaidi.

Kwa kufanya hivi, Serikali inaweza ikapunguza Kwa kiasi kikubwa utegemezi wa sera za ubinafsishaji kuendesha mashirika na taasisi zake Kwa kuwa itakuwa ina uwezo wa kuyaendesha yenyewe Kwa faida.
 
Kama wao hawataki faida waaanzishe then wabinafsishe wachukue faida ,tatizo lao wanakubinafsishia then wanaleta siasa zao umo ndan
 
Mtanena kwa lugha safari hii
mie nadhani tuende mbali zaidi,
hata viongozi wa kisiasa waondoe mentality kwamba hakuna wengineo wenye uwezo wa kuongoza chama ili kuibua, mawazo, fikra, uelekeo na dira mpya na kuongeza ufanisi wa taasisi 🐒

au unalionaje hili kamanda 🐒
 
Kuna mtazamo ambao umejengeka kwamba Serikali Haina lengo la kutengeneza faida bali kutoa huduma, mtazamo huu Kwa uono wangu hafifu nafikiri ndio chanzo kikubwa Cha baadhi ya mashirika kushindwa kujiendesha na kupelekea kubinafsishwa ama kuingia ubia na sekta binafsi.

Badala ya kuwa na mtazamo wa namna hii kwamba Serikali haipo Kwa ajili ya kutengeneza faida bali kutoa huduma ,kwanza kabisa mtazamo huu ubadilishwe, Serikali ianze kujikita katika kutoa huduma na kutengeneza faida.

Serikali iwekeze Kwa lengo la kupata faida kwa namna hii itajikita katika kutoa huduma bora zaidi.

Kwa kufanya hivi, Serikali inaweza ikapunguza Kwa kiasi kikubwa utegemezi wa sera za ubinafsishaji kuendesha mashirika na taasisi zake Kwa kuwa itakuwa ina uwezo wa kuyaendesha yenyewe Kwa faida.
Model lGani ya uchumi
Kama ni uchumi wa kibepari serikali iachane na biashara ibakie na huduma tu Hilo halina ubishi, tafiti zilifanyika
 
Back
Top Bottom