Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,362
- 48,879
Maandamano ya vijana wa Kenya ya kupinga mswada wa sheria ya kodi 2024/2025 yaliyanza kwa amani, na baadaye yameishia kwenye maafa. Lakini inaelezwa kuwa chanzo ni baada ya Polisi kumwua kijana asiye na kosa, na hivyo kuamsha hasira za waandamanaji.
Vitendo zaidi vya uhalifu vimefanywa na Polisi usiku wa kuamkia jana ambapo Polisi walifanya mauaji ya vijana si chini ya 12, na kuwakamata wengine, baadhi mpaka sasa hawajulikani waliko. Kutokana na Polisi kuzidiwa nguvu na waandamanaji, Serikali iliamua kuwapeleka wanajeshi kusaidiana na Polisi, lakini uamuzi huo umepingwa vikali na Baraza la Maaskofu Katoliki, lililomtaka Rais Ruto kuwarudisha haraka wanajeshi makambini kwao.
Kufuatia vitendo vya Polisi kukiuka katiba, Jaji Mkuu wa Kenya ametoa onyo kali kwa mamlaka zote, ikiwemo Serikali, kuhakikisha hawakiuki katiba, na ametoa wito kwa Wakenya wote kupeleka malalamiko mahakama kuu ya Kenya kama kuna mtu yeyote ametekwa na Polisi, na kuahidi mahakama kufanya kazi hata nje ya masaa ya kazi ili kuwatendea haki waathirika.
Pia soma: Mahakama kuu yaamuru serikali kusitisha zoezi la wanajeshi kwenda mtaani kuzuia maandamo
Kitendo hiki cha Jaji Mkuu wa Kenya kinaonesha uhuru wa mhimili wa mahakama nchini Kenya. Tujiulize kama Jaji Mkuu wa Tanzania anaweza kudiriki kufanya hata 10% ya hiki alichokifanya Jaji Mkuu wa Kenya. Hakika Watanzania katika masuala ya kiutawala bado tupo gizani sana, hata mwanga hatujaanza kuuona.
Ikumbukwe kuwa hakuna nchi hata moja ambayo mambo yote yanaenda na kutendwa kwa 100% perfection, lakini ubora wa mifumo ya utawala inapimwa na uwepo wa mifumo ya kudhibiti waovu na wanaokiuka katiba na sheria. Angalao Kenya wamefika mahali hapo. Kwetu mpaka Rais analalamika juu ya ukiukaji mkubwa wa haki za
raia unaofanywa na Polisi, ikiwemo mahabusu kuuawa wakiwa mikononi mwa Polisi lakini hakuna anayewajibika wala anayewawahibisha Polisi. Wote tunaishia kulalamika. Sijawahi kumsikia Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea ukiukaji wa haki dhidi ya raia unaofanywa na mhimili wa Serikali hata mara moja, japo matukio hayo yapo mengi.
Tangazo la Jaji Mkuu wa Kenya:
Vitendo zaidi vya uhalifu vimefanywa na Polisi usiku wa kuamkia jana ambapo Polisi walifanya mauaji ya vijana si chini ya 12, na kuwakamata wengine, baadhi mpaka sasa hawajulikani waliko. Kutokana na Polisi kuzidiwa nguvu na waandamanaji, Serikali iliamua kuwapeleka wanajeshi kusaidiana na Polisi, lakini uamuzi huo umepingwa vikali na Baraza la Maaskofu Katoliki, lililomtaka Rais Ruto kuwarudisha haraka wanajeshi makambini kwao.
Kufuatia vitendo vya Polisi kukiuka katiba, Jaji Mkuu wa Kenya ametoa onyo kali kwa mamlaka zote, ikiwemo Serikali, kuhakikisha hawakiuki katiba, na ametoa wito kwa Wakenya wote kupeleka malalamiko mahakama kuu ya Kenya kama kuna mtu yeyote ametekwa na Polisi, na kuahidi mahakama kufanya kazi hata nje ya masaa ya kazi ili kuwatendea haki waathirika.
Pia soma: Mahakama kuu yaamuru serikali kusitisha zoezi la wanajeshi kwenda mtaani kuzuia maandamo
Kitendo hiki cha Jaji Mkuu wa Kenya kinaonesha uhuru wa mhimili wa mahakama nchini Kenya. Tujiulize kama Jaji Mkuu wa Tanzania anaweza kudiriki kufanya hata 10% ya hiki alichokifanya Jaji Mkuu wa Kenya. Hakika Watanzania katika masuala ya kiutawala bado tupo gizani sana, hata mwanga hatujaanza kuuona.
Ikumbukwe kuwa hakuna nchi hata moja ambayo mambo yote yanaenda na kutendwa kwa 100% perfection, lakini ubora wa mifumo ya utawala inapimwa na uwepo wa mifumo ya kudhibiti waovu na wanaokiuka katiba na sheria. Angalao Kenya wamefika mahali hapo. Kwetu mpaka Rais analalamika juu ya ukiukaji mkubwa wa haki za
raia unaofanywa na Polisi, ikiwemo mahabusu kuuawa wakiwa mikononi mwa Polisi lakini hakuna anayewajibika wala anayewawahibisha Polisi. Wote tunaishia kulalamika. Sijawahi kumsikia Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea ukiukaji wa haki dhidi ya raia unaofanywa na mhimili wa Serikali hata mara moja, japo matukio hayo yapo mengi.
Tangazo la Jaji Mkuu wa Kenya: