TUJIKUMBUSHE HISTORIA YETU YA WAZALENDO

TUJIKUMBUSHE HISTORIA YETU YA WAZALENDO

Nyanda Banka

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2023
Posts
304
Reaction score
1,054
Pichani ni Nduna Songea Mbano Luwafu. Alipigwa picha hii muda mfupi kabla ya kunyongwa na wajerumani Machi mwaka 1906.

Kifo chake kilitanguliwa na mauaji ya Mashujaa wengine 66 wa Majimaji walionyongwa Februari 27, mwaka 1906.

Songea Mbano alinyongwa pekee yake siku tatu baada ya wenzake hao 66 kunyongwa na kuzikwa katika kaburi la pamoja àmbalo lipo katika Makumbusho ya Taifa ya Majimaji katikati ya Mji wa Songea.

Hata hivyo Songea Mbano alizikwa katika kaburi la peke yake.Inasadikika kuwa wajerumani walikata kichwa chake na kuondoka nacho na hapa wamezika kiwiliwili chake tu.

Wazee wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea kila mwaka wamekuwa wanaiomba serikali na Wizara ya Maliasili na utalii kufuatilia kichwa cha Songea nchini Ujerumani ili kiweze kurudishwa Tanzania, jitihada ambazo bado hazijazaa matunda.

Ikumbukwe kuwa Jina la Mji wa Songea limetokana na jina la shujaa huyu mzalendo, ambaye kwayo ustahimilivu wake katika kudai haki ulipelekea kifo chake cha kinyama.

Mwezi Machi mwaka huu tutafanya kumbukizi ya miaka 112 tangu kifo chake kilichotokana na hila za serikali ya kikoloni chini ya Wajerumani.

Hakika ataendelea kukumbukwa daima dumu.
 

Attachments

  • 1719828017149.jpg
    1719828017149.jpg
    352.4 KB · Views: 12
Hiyo "Luwafu" ni kifupisho cha Abdul Rauf.

Aliupinga ukoloni kwa hal
Pichani ni Nduna Songea Mbano Luwafu. Alipigwa picha hii muda mfupi kabla ya kunyongwa na wajerumani Machi mwaka 1906.

Kifo chake kilitanguliwa na mauaji ya Mashujaa wengine 66 wa Majimaji walionyongwa Februari 27, mwaka 1906.

Songea Mbano alinyongwa pekee yake siku tatu baada ya wenzake hao 66 kunyongwa na kuzikwa katika kaburi la pamoja àmbalo lipo katika Makumbusho ya Taifa ya Majimaji katikati ya Mji wa Songea.

Hata hivyo Songea Mbano alizikwa katika kaburi la peke yake.Inasadikika kuwa wajerumani walikata kichwa chake na kuondoka nacho na hapa wamezika kiwiliwili chake tu.

Wazee wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea kila mwaka wamekuwa wanaiomba serikali na Wizara ya Maliasili na utalii kufuatilia kichwa cha Songea nchini Ujerumani ili kiweze kurudishwa Tanzania, jitihada ambazo bado hazijazaa matunda.

Ikumbukwe kuwa Jina la Mji wa Songea limetokana na jina la shujaa huyu mzalendo, ambaye kwayo ustahimilivu wake katika kudai haki ulipelekea kifo chake cha kinyama.

Mwezi Machi mwaka huu tutafanya kumbukizi ya miaka 112 tangu kifo chake kilichotokana na hila za serikali ya kikoloni chini ya Wajerumani.

Hakika ataendelea kukumbukwa daima dumu.
Pichani ni Nduna Songea Mbano Luwafu. Alipigwa picha hii muda mfupi kabla ya kunyongwa na wajerumani Machi mwaka 1906.

Kifo chake kilitanguliwa na mauaji ya Mashujaa wengine 66 wa Majimaji walionyongwa Februari 27, mwaka 1906.

Songea Mbano alinyongwa pekee yake siku tatu baada ya wenzake hao 66 kunyongwa na kuzikwa katika kaburi la pamoja àmbalo lipo katika Makumbusho ya Taifa ya Majimaji katikati ya Mji wa Songea.

Hata hivyo Songea Mbano alizikwa katika kaburi la peke yake.Inasadikika kuwa wajerumani walikata kichwa chake na kuondoka nacho na hapa wamezika kiwiliwili chake tu.

Wazee wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea kila mwaka wamekuwa wanaiomba serikali na Wizara ya Maliasili na utalii kufuatilia kichwa cha Songea nchini Ujerumani ili kiweze kurudishwa Tanzania, jitihada ambazo bado hazijazaa matunda.

Ikumbukwe kuwa Jina la Mji wa Songea limetokana na jina la shujaa huyu mzalendo, ambaye kwayo ustahimilivu wake katika kudai haki ulipelekea kifo chake cha kinyama.

Mwezi Machi mwaka huu tutafanya kumbukizi ya miaka 112 tangu kifo chake kilichotokana na hila za serikali ya kikoloni chini ya Wajerumani.

Hakika ataendelea kukumbukwa daima dumu.
Nyanda...
Tafadhali angalia hayo hapo chini:
  1. Abdulrauf Songea Mbano
  2. Hassan Omari Makunganya
  3. Khadija Mkomanile
  4. Abdallah Nchimai
  5. Selemani Mamba
  6. Mtwa Abdallah Mkwawa
  7. Abushiri bin Salim
  8. Shomari Jumbe Jahazi
  9. Makanda Mwinyimkuu
  10. Omar Chinyalanyala
  11. Sultan Mataka bin Hamin Massaninga.
Ukisoma historia ya Vita Vya Maji Maji utakutana na jina Mkomanile.
Linaandikwa jina moja tu, ''Mkomanile.''

Kwa nini liandikwe jina moja tu?

Huyu ndiye mwanamke pekee katika majina karibu 67 ya mashujaa wa Vita Vya Maji Maji aliyenyongwa na kuzikwa katika kaburi la halaiki Mahenge Songea.

Huyu mwanamke jina lake ni Khadija Mkomanile.
Kwa nini jina la Khadija halikuandikwa?

Tuseme hawakulijua?
Ukisoma historia ya Maji Maji utasoma jina Chinyalanyala jina moja tu.

Kwa nini liandikwe jina moja tu?
Jina lake ni Omar Chinyalanyala.

Inawezekana kuwa jina la Omar hawakuifahamu?
Ukisoma historia ya Vita Vya Maji maji utasoma jina la Songea Mbano.

Hapa unasoma majina mawili jina moja halikutajwa.

Kwa nini jina lake la kwanza halikuandikwa lifahamike?
Huyu jina lake lake la kwanza ni Abdulraufu.

Hili jina Abdulraufu hawakulijua?
Kuna ''Kazembe'' lakini jina lakini la kwanza halipo.

Haya yanashangaza sana.
 
Back
Top Bottom