chavalla
JF-Expert Member
- Apr 13, 2017
- 451
- 354
[HASHTAG]#FAHAMU[/HASHTAG] Muigizaji wa filamu ya 'God Must be Crazy', Nǃxau ǂToma, alizaliwa mwaka 1944 huko Namibia, ametokea katika jamii ya kabila la 'San'. Katika maisha yake aliwahi kuwaona wazungu watatu tu mpaka pale alipopata bahati ya kuigiza kwenye filamu hiyo, kabla ya hapo alikuwa hajui maana ya pesa na thamani yake wala hajui ilikuwa nini, aliona ni kama kipande cha karatasi, alipolipwa pesa yake kutokana na sanaa ilibidi aelimishwe pesa ni nini, baada ya hapo aliweza kuijengea familia yake nyumba ya tofali, yenye maji na umeme, kwa mujibu wa vyanzo vya Namibia, alikuwa hajui kuhesabu zaidi ya 1-20. Alipata bahati ya kuzunguka nchi mbali mbali duniani kuigiza filamu, baada ya hapo alirudi nyumbani kwake Namibia. Mwaka 2003 alifariki kwa ugonjwa wa TB.
Share na wenzako waweze kumjua 'Bushman'.
Share na wenzako waweze kumjua 'Bushman'.