Tujikumbushe Majina ya Utani Mashuleni

Kichankuli

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2008
Posts
887
Reaction score
190
Wadau tukumbushane AKA za mashuleni tulikosomea.

Mimi naanza na Minaki na Umbwe:

Minaki aka Dabanga
Tumbili aka Vinyanyiko
Mkuu wa Shule aliyekuwepo wakati wetu aka Faza
Mkuu wa Shule Msaidizi aka Pilato
Maticha wengine walikuwemo kina Braza Kei, Kiburungutu, Mpapa Mabuga, Mpapampapa, Mshua, Zanta, n. k.

kwenda Jijini DSM = Kudrop Town;
Ugali = Jiwe;
Uji = Udaga
Kusoma = kuchima
Mwanafunzi anayesoma sana = Kichimbuzi
Choo cha Shimo = Cheche

Umbwe = Mti Safi;
Head Master wa wakati huo = Savimbi
Walimu wengine walikuwa kina Lobilo, Jogoo, Zimwi, Mchemfu, Bob Liz kulikuwa na mfanyakazi mdada aliyeitwa Kuku

Ugali = Bonge;
Uji = Sifongo;
ujazo wa sahani tatu za uji = Ninga moja;
Mkate wa Arusha = Mbuzi;
Eneo la mbele ya duka = Slaidi;
Kukaa eneo la mbele ya duka la shule na kuwaangalia mabinti wa Kikibosho wanapita = Kuslaidi;
Kusoma usiku kwa mda mrefu = Kurusha Eya
Choo cha Shimo = Maputo

Karibuni muongezee mengine
 
Tabora Boys :
(i) Wasichana wa Tabora girls - Mawosoo
(ii) Kuongea pumba-kufuka
(iii) Kusoma - kubundi
(iv) Mtu anaesoma Sana - kibunda
(v) Kengele ya chakula ikipigwa - limebani
(vi) Mkuu enzi zile - Dulla
(vii) Wanafunzi wa shule ya Milambo (actually kulikuwa na bifu lisiloisha) - Walambo
(viii) Walikuepo maticha kama Manywele(alikua anadis nywele ndefu), Marwa(kauzu), Tevez(sababu uwanjani alikua anavaa tshirt imeandikwa "Tevez" mgongoi n.k
(ix) Sehemu ya wenyeji wako kipindi cha shule - ubalozini
(x) Zilikuepo chemba Kama Umofia, Galapagos, Versity, White House, n.k
(xi) Wali-Nyali
(xii) Uji-pola
 
NSUMBA BOYS
Kujificha kutokwenda darasani- chaka
Maandazi - makamata
Wasichana - Ngada
 
Kijana we wa enzi za Jana

Unyuka aka sukari huujui?
Je Berlin?
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji119] [emoji119] [emoji119] [emoji119]
 
kibaha boys...!!
Kuongea pumba=kufuka
wasichana wabovu=mapolygoni
ugali=bondo
maharage=ndondo
maandz =mapisi
mikate=mipongoo
kunywa chai tupu= kupiga deki
kuoga= kuchirizi
na mengineee ongezea
#preciousKibaha
 
Uji =sifongo.... Haha.. I like that.
 
Asee umenikumbusha watt wakinyanyiko na ile kona yenu...umenikumbusha na Zanta, tulikuwa tunaweka kambi ya UMISETA mkoa wa pwani...good old days
 
kibaha boys...!!
Kuongea pumba=kufuka
wasichana wabovu=mapolygoni
ugali=bondo
maharage=ndondo
maandz =mapisi
mikate=mipongoo
kunywa chai tupu= kupiga deki
kuoga= kuchirizi
na mengineee ongezea
#preciousKibaha
Minaki wasichana wenye sura mbaya = Vipori/kipori

Umbwe kutokuoga na badala yake kunawa uso na mikono kwa sabvabu ya baridi kali = Kupiga passport
 
kibaha boys...!!
Kuongea pumba=kufuka
wasichana wabovu=mapolygoni
ugali=bondo
maharage=ndondo
maandz =mapisi
mikate=mipongoo
kunywa chai tupu= kupiga deki
kuoga= kuchirizi
na mengineee ongezea
#preciousKibaha
Minaki wasichana wenye sura mbaya = Vipori/kipori

Umbwe kutokuoga na badala yake kunawa uso na mikono kwa sabvabu ya baridi kali = Kupiga passport
 
hedaru sec
kuungalia au kuchungulia madem inaitwa kula upoda
muda wa kukaa chemba na dem ni papaso time
 
Meta sekondari
1.kupiga pushup-dar mpaka moro
2.mwalim mkuu njegite
3.mwalimu wa somo la kiingereza mpaka leo hafahamiki jina ila anafahamika kwa jina la pepe kale kutokana na uvaaji wake wa suruali
4.mwalimu baroka hilo ni aka naye hafahamiki
5.mwalimu mnose aka fashona ilitokana na kupendeza kwake kila ck so smart
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…