Tujikumbushe mchakato wa katiba Kenya ulivyosaidia kuing'oa KANU: Kujirudia kwa CCM?...

Tujikumbushe mchakato wa katiba Kenya ulivyosaidia kuing'oa KANU: Kujirudia kwa CCM?...

Tuko

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
11,180
Reaction score
7,346
Kwa wanaokumbuka, Kenya ilikuwa na mchakato wa katiba kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2002.

KANU wakitumia wingi wao bungeni walilazimisha kuandikwa kwa rasimu mbovu ambayo ilipingwa na vyama vyote vya upinzani wakati ule. Walipoenda kwenye kura ya maoni, "wapinzani mahasimu"; Raila na Kibaki walijikuta katika kundi moja la Orange lililokuwa likipinga rasimu ile.

Matokeo ya kura ya maoni yalishuhudia kundi la orange likishinda na rasimu ile kutupiliwa mbali. Wapinzani kwa kuona matunda ya kuungana kwao waliendeleza umoja wao na ndipo Raila alipotamka, katika uwanja wa Kasarani kuwa "Kibali tosha"... akimaanisha kwa mara ya kwanza Mjaluo anaungana na Mkikuyu. Mafanikio ya ushindi katika kura ya maoni yalipelekea wapinzani kushinda uchaguzi mkuu mwaka 2002. Je, kuungana kwa wapinzani wa kweli Tz katika mchakato wa katiba, itakuwa chachu ya kuwaunganisha na kushinda uchaguzi mkuu ujao?...

Kwenu wachambuzi
 
Definitely, ndio maana sasa hivi CCM wamekuwa mbogo.
 
Hata bila katiba CCM wanang'oka asubuhi hata kabla vituo havijafunguliwa...!!!!!
 
Nywele zinaisha kichwani sababu ya kuwaza rasimu ya katiba
 
Kwa wanaokumbuka, Kenya ilikuwa na mchakato wa katiba kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2002. KANU wakitumia wingi wao bungeni walilazimisha kuandikwa kwa rasimu mbovu ambayo ilipingwa na vyama vyote vya upinzani wakati ule. Walipoenda kwenye kura ya maoni, "wapinzani mahasimu"; Raila na Kibaki walijikuta katika kundi moja la Orange lililokuwa likipinga rasimu ile. Matokeo ya kura ya maoni yalishuhudia kundi la orange likishinda na rasimu ile kutupiliwa mbali. Wapinzani kwa kuona matunda ya kuungana kwao waliendeleza umoja wao na ndipo Raila alipotamka, katika uwanja wa Kasarani kuwa "Kibali tosha"... akimaanisha kwa mara ya kwanza Mjaluo anaungana na Mkikuyu. Mafanikio ya ushindi katika kura ya maoni yalipelekea wapinzani kushinda uchaguzi mkuu mwaka 2002. Je, kuungana kwa wapinzani wa kweli Tz katika mchakato wa katiba, itakuwa chachu ya kuwaunganisha na kushinda uchaguzi mkuu ujao?...

Kwenu wachambuzi

CCM hawana pa kutokea, ndio wanajitahidi kufanya hila lakini hawatoki.
Sikio la kufa halisikii dawa.
Kizazi cha digitally kiko macho sana!
 
Back
Top Bottom