Tujikumbushe, ni kitu gani kimewahi kukutoa ushamba!?

Naingia benki mara ya kwanza baada ya kufungua mlango na kuingia naona mlango unarudi wenyewe sasa nikaogopa usije kujibamiza kwasababu ni wa kioo nkaushika na kuuanza kuupeleka taratibu .

Mlinzi ndo akanambia hauna shida we achia tu
Hahahahaha....kama nakuona mkuu, ulivyojifaragua baada ya kuambiwa hivyo.
 
Nimekumbuka past kidogo kuzama ndani ya darkweb asee, siku hio nljiona sijui i.t hata chembe,kila kitu kilikua kigeni.
 
HAKIKA NIMEPONYEKA JUU YA USHAMBA...LABDA SABABU HUWA SIPENDI KUJIFANYA MJUAJI....KTK JAMBO LAUGEN KWANGU HUWA NACHUKUA TAHADHAR MAPEMA AU KUJIWEKA NYUMANYUMA....UZUR KUSOMA NAKO TUNASAIDIKA JMN HUWA SIKURUPUKII JAMBO...YAN NIKIFIKA SEHEM HUSIKA HUWA NATULIA KWA KUZUGA NAWASOMA WENYEJ WANAFANYAJE....LABDA NIULIZE KWA HILI MSHAMBA NANI......NILITOKA SHOPPING NA MCHUMBA YY AKIWA NA MDOGO WAKE TOKA MORE TO DAR KKOO....MIMI NIMEZOE KKOO HUWA NASHUKIA ICHO KITUO CHA SIMBAZI THEN NAZURULA KILA NNAKOHISI NTAPATA HITAJIO LANGU....SASA NILIPO KUWA NA HAWA WAREMBO MWENDO KAS LILIPOFIKA HAPO NIKASHUKA NIKASHANGAA WAO HAWAJASHUKA KUWAANGAALIWA WANANIAMBIA BADO HATUJAFIKA(JAMANIIII) NIKARUD GARINI WAKAWA WANANISHANGAA JMN BADOOOO...TUKAENDA HAD MWISHO WA GAR KITUO KIKUBWA SIJUI YAN ICHO KITUO KIKWEL CJAWAH KUKIFIKA NDIO TUKASHUKA HAPO....SASA SIJUI NI SABABU YA KUWA SHOPPING NIYA NGUO SO KITUO KILE NDIO KIKO KARIBU....MIMI NIMEZOEA KUSHUKIA ICHO CHA MSIMBAZ COZ MAHITAJ YANGU HUWA NI BIDHAA ZA ELECTRONICS.....MPK LEO NAKUMBUKA SIJUI NDIO WALINIONA MSHAMBA...
 
Escalator/Ngazi inayotembea.
Mpaka sasa mimi na huyo jamaa ni maadui wa kudumu, sijawahi kumzoea na sitaki kumzoea.
siku ya kwanza nilishikiliwa kama vile mbuzi akiwa hataki kwenda anavyovutwa aisee ilikua hatari.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] lol.

Mdogo wangu ndio sababu mie dada yako huwa nazikwepa labda itokee siku niwe sina jinsi ya kufika ninapopataka kwenda nje ya hapo wazipande tu wenye kuweza sababu sitaki aibu mie.
 
Last edited by a moderator:
Teh!kilichonitoa mimi ushamba nitakuambia pm
 
nimeenda posta kutuma barua ilikuwa kazi siku ile nawaza naidumbukiza ki namna gani? kwa urefu ama upana.

nikaona isiwe shida nikamfata mtu mmoja kumuuliza mzee hii barua naidumbukiza vp? kwa upana ama urefu alicheka saanaaaa yule mzee akanambia vyovyote vile.
 
Escalator/Ngazi inayotembea.
Mpaka sasa mimi na huyo jamaa ni maadui wa kudumu, sijawahi kumzoea na sitaki kumzoea.
siku ya kwanza nilishikiliwa kama vile mbuzi akiwa hataki kwenda anavyovutwa aisee ilikua hatari.
ile kitu inataka taiming kwenye kuweka mguu wa. kwanza.Mi kinachoniokoa kwenye vitu nisipovijua ni kupenda kujifunza kwa kupitia kuangalia wengine wanafanyaje.kisha nikashaona ndo namie nafanya
 
Mmh. Ushamba tena wakati ndio uendeshaji wao wa kila siku

Japokuwa huwa sibariki watu wanaoendesha gari Automatic kwa miguu miwili kwani wapo na hawana ushamba hata chembe.
Hii huchangia kuharibu gari
Kwa mujibu wa kitabu cha gari
 
mkuu ushamba wako uko kwenye kutype.unatumia herufi kubwa paragraph nzima hii kiundishi humaanisha unazungumza kwa kupayuka.
 
Hii huchangia kuharibu gari
Kwa mujibu wa kitabu cha gari
Kuumbe au sijakuelewa Mkuu?

Nina watu wangu wa karibu Mtu na Mkewe sijui utawaambia kwa lugha gani wakuelewe maana wameshazowea wenyewe.

Ila akiendesha mmoja wapo huwa nakuwa na wasiwasi tu halafu sijuagi kwa nini?

Itakuwa hawasomagi hizo vitabu basi Mkuu.
 
mkuu ushamba wako uko kwenye kutype.unatumia herufi kubwa paragraph nzima hii kiundishi humaanisha unazungumza kwa kupayuka.
HAHAHAA SAWA MKUU...WEWE SIO MSHAMBA MAANA UMEANDIKA KWA HERUFI NDOGO HATA BAADA YA KUWEKA NUKTA...KAMA HUJUI HAKUNA MAKOSA KUANDIKA KWA HERUFI KUBWA INSHA NZIMA ILA NI KOSA KUANZA KWA HERUFI NDOGO AU BAADA YA NUKTA....NANI MSHAMBA....HALAFU KUNA UZI WANGU UNAZUNGUMZIA TOFAUTI KATI YA MSHAMBA NA MJINGA....KASOME KISHA JITAFUTIOE NAFAS YAKO KATI YA MJINGA AU MSHAMBA.....
 
Ndio mkuu, washauri watumie mguu mmoja,mwingine ukae pembeni
Kwenye kitabu cha subaru wametaadharisha kuwa kukanyagia mikuu yote huaribu kitu fulani kwenye engine,nimekisahau
 
Umenichekesha sana hapo kwenye quality centre
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…