Tujikumbushe Taifa Stars ya Marcia Maximo

Somi

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2009
Posts
3,921
Reaction score
4,858
Bila shaka bila ubishi bila ajizi Taifa Stars ya Mbrazil Marcio Maximo ndiyo iliyoweka rekodi ya mafanikio kuliko wakati wote katika historia ya Tanzania.
Timu za jirani zilikuwa hazitusumbui kabisa lazima zipigwe magoli zikikutana na sisi.
Peak ya mafanikio ilikuwa kufuzu mashindano ya Chan 2009 Côte D’ Ivoire .
Tulikuwa kidume wa afrika mashariki na Kati sio kwa staili ya kubebwa kwa Kuwapiga kenya, Uganda , Ethiopia na Sudan huku rwanda na Burundi wakifungwa na Uganda na Sudan .
Kule Côte d’Ivoire tukifungwa kwa taabu na senegal ya Mane, diouf,fall, ndiaye,ndiour,diamanka Sow nk mpaka leo diouf anaijua Stars.
Tukawafunga cote d’ ivoire wenyeji .
Mechi ya mwisho tukatoka sare na Zambia.zambia wakiponea chupuchupu kwa kusawazisha dakika ya 94 hivyo tukakosa nusu fainali ya africa kwa nukta ya mwisho ya saa.
Zambia hii ndiyo ilikuja kuwa mabingwa wa Africa miaka mawili baadae zambia ya singuluma,Banda nk
DR Congo ya tresor mputu ikawa
Mabingwa wa kwanza chan 2009
 
Hii timu ya maximo ilikuwa tishio sema walikosa bahati
Yule mzee alikuwa nini maana ya kuwa kocha halisi wa taifa
 
Tutakuja kuchambua mda mwingine..
tupo busy na SIAIJIIII
 
yule ndiyo Mwl wa mpira ambaye alituweza! Full misimamo! Alimuacha JUMA K JUMA akamuita SHABAN DIHILE (amsaidie Ivo Matunda)
 
ilikua pasi nne shida,alipokaa muda wa kutosha tukawa tunapga hadi pasi 12
 
Kipindi hiki ndo watu walikua so proud kuvaa jezi ya timu ya taifa.
 
Starz ya mdenish ndiyo.ilikuwa ikicheza mpira wa kuvutia mrudisheni kim paulsen
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…