Tujikumbushie Michael Wambura, visa, visanga na kesi za mara kwa mara

Eli Cohen

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2023
Posts
4,460
Reaction score
13,715
Huyu jamaa ilikuwa ni kama kila siku kwenye taarifa ya habari unakutana na visanga vyake.

Mara mahakamani, mara sijui wamezinguana na TFF, mara analalamika anaonewa, etc.

Nafikiri tunaweza kumuweka yeye kuwa mmoja kati ya watu waliokuwa na visanga vingi mahamakani hapa bongo.

 
Adhabu ya kufungiwa maisha kujihusisha na soka bado haijaisha muda wake? Ila huyu jamaa alipambana hasa kwenya kupata fursa za kuongoza mambo ya soka akaishia kupewa adhabu ya kufungiwa maisha asijihusishe na mambo ya mpira. Bora akajiingize kwenye siasa, tena siasa za upinzani huenda akatimiza ndoto zake za kuwa kiongozi bora wa umma
 
Alitaabika sana
 
Moja kati ya watu waliokuwa na uchungu na soka la Tanzania tangu ikiitwa FAT (TFF) lakini manyangau na malafi ya kushibisha matumbo yao yakamuundia mizengwe.
Alikuwa kundi la waharibifu wa mpira wa miguu. Yeye na mwenzake Jamal Malinzi na Kaburu. Waliongoza mpira wakati fulani wadhamini wakakosa confidence ya kuwekeza. Toka wafungiwe Sasa hivi mpira umetulia.
 
Usitutoe mchezoni na historia zako za Wambura wako hatusaidii chochote. Nakukumbusha kuwa leo ni siku ya unyama mwingi hapo Lupaso
 
Alikua mtata kweli kweli nakumbuka Kuna siku msimbazi pale klabu alimtolea bastola kiongozi mmoja wa Simba wakati ule,
na mikwala mingi Sana ,alikua anajiamini Sana uyo jamaa
 
๐Ÿ˜„๐Ÿ˜€๐Ÿ˜„๐Ÿ˜€Huyu jamaa kuna kipindi alikua katibu wa Tff na mwenyekiti alikua Ndolanga walikua hawapatani kabisa

Kila siku wanagombana,kesi
 

Yanga wamemuweka kwenye Dokomentary yao kesho tutamuona vizuri zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ