Tujue kutofautisha maana halisi ya neno Mungu na mungu

fourtypercent

Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
53
Reaction score
20
Habari,

Nimekuwa nikiona post, comment hapa Jf na wakati mwingine Sms nikitumiwa
na watu mbalimbali nimegundua kuwa watu hawajui kutofautisha maana ya neno
Mungu au MUNGU au Bwana au BWANA na mungu au bwana.

Haya maneno mawili yana maana mbili tofauti
1. Mungu au MUNGU- lina maanisha Mungu tunayemwabudu, Mungu wa
Ibrahimu,Isaka na Yakobo ni Mungu aliye hai. aliyekuwepo,aliyepo
na atakayekuwepo. nafikiri nimeeleweka

2. mungu- linamaanisha miungu kama mungu Baal au Ndama wa dhahabu
aliyetengenezwa na wana wa Israel safarini kuelekea Kaanan au chochote
mtu aabuducho kisicho na sifa za Mungu niliyemtaja kipengele cha kwanza

For reference, angalia katika Biblia utaona hiki ninachokiongelea hapa
Ahsante najua kuanzia leo tutakuwa makini na kile tunachokiandika tusije
tukawa tunamwabudu shetani pasipo kujua. Mbarikiwe
 
Hizo ni mbwembwe tu. uandike Mungu au mungu atabaki yeye pekee ndiye aliyeumba dunia na vilivyomo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…