Tujuzane: Kwanini matairi ya magari ni rangi nyeusi?

Alvajumaa

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2018
Posts
5,039
Reaction score
6,253
Kila mmoja wetu anajua kwamba matairi ya magari hutengenezwa na mpira, Lakini tunaweza kuzalisha rangi yoyote ile tuitakayo ,

Matairi mengi hutengenezwa kwa rangi nyeusi, Lakini kuna rangi za kuvutia kama blue, kijani, nyekundu, manjano ama hudhurungu
Kwanini iwe rangi nyeusi tu?
Tujuzane

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Matairi mengi hutengenezwa kwa rangi nyeusi, Lakini kuna rangi za kuvutia kama blue, kijani, nyekundu, manjano ama hudhurungu
Kwanini iwe rangi nyeusi tu


Yakiwa ya rangi jiandae na kamata kamata ya ushabiki wa kiitikadi
 
Yakiwa na rangi kuna watu watachagua either apande lenye rangi nyekundu na siyo la rangi ya kijani .
 
Taili za gari zinatengenezwa kwa kutumia ute unaotoka kwenye miti ya miraba. Miti hii ute wake ni mweupe kama ute wa miti ya mnyaa, lakini ili kutengeneza taili ya gari, huchanganywa na madini ukaa na viambata vingine vinavyotumika kuimarisha taili. Rangi nyeusi ni kiashiria cha uwepo wa madini hayo ya "Carbon" lakini kuna uwezekano wa kuongezea rangi nyingine na kuzifanya taili ziwe na rangi yoyote inayohitajika.
 
Shukran

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru kwa jibu lako kuntu!!
La ajabu ukihesabu idadi na uzalishaji wa matairi ktk Dunia hii uwepo wake kea wingi.. Sidhani hiyo miti itatosheleza kuProduce ukubwa na wimbi la masoko ya tairi!! (Nadhani huo Ute NI mfumo uliyoanza zamani Sana ikabadilishwa na Chemicals) !!
Maana ya kusema hivo Hakuna shamba za miti/Ute huo kuwiana na idadi za matayiri yanayotumika hivi Sana na mustakabali...
Prove me wrong!! Shukraan
 
Hizo ni aina mbili za barabara, siyo aina mbili za lami. Lami ni Asphalt lakini lami siyo Portland Cement. Ukiwa na hiyo flexible pavement ambayo inatengenezwa kwa Asphalt concrete hapo una barabara ya lami. Lakini ukawa na rigid pavement inayotengezwa kwa Cement, hapo siyo barabara ya lami bali ni barabara ya cement concrete. Lami = Asphalt.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tujivunie tairi zimetengenezwa kwa rangi zetu, maana hata ikimeguka haionekana, na traffic kuitambua ni vigumu.
 
Point of correction..
Rami[emoji777]
Lami[emoji3581]
Barabara ya mwendokasi siyo lami...zile ni barabara za zege.... concrete road..
Concrete na lami ni materials ya aina mbili tofauti

Sasa nirudi kwenye point...kama mjumbe mmoja alivyosema kuwa ute wa miti fulani huchanganywa na vitu vingine vyenye rangi nyeusi mfano carbon..

Kwa kuwa rangi nyeusi imekuwa ikitumika tangu enzi na enzi, basi imekuwa international standard....yaani ndiyo rangi inayokubalika kimataifa kwa upande wa matairi....ni kama vile rangi ya njano au orange ilivyokubalika kimataifa itumike sehemu mbalimbali kutoa ishara ya onyo au tahadhari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…