Comrade Ally Maftah
Member
- Nov 6, 2016
- 77
- 271
TUNALOJUKUMU LA KUDHIBITI HALI YA UKATILI NA UNYAMA UNAOJENGEKA KATIKA WENZETU
Na Comrade Ally Maftah
Nilipata kusikia tukio la dada aliyefanyiwa ukatili wa kijinsia nikajidhibiti sana nisitazame tukio hilo, ila kwa bahati mbaya sana nimeona kipande kidogo cha tukio lile.
Tukio limenitafakarisha mno nimejiuliza maswali mengi sana baada ya kuona tukio lile.
1. Nimemwona mwathirika akiomba radhi na kusema hatorudia tena, lakini jamaa walikosa utu kabisa, hawakuguswa kabisa na msamaha aloomba mwathirika.
2. Kuna sauti inaashiria watendaji wa jambo ni watumishi wa uma, ambao wanalipwa kwa kodi zetu.
3. Uungwana na ustaarabu wa mwafrika ulipotea kabisa, utendaji wa uhalifu pamoja na uchukuaji wa video haikuwa taratibu za tamaduni zetu, tendo lililofanyika haliweze kutendwa na mtu mwenye hekima, na mtu asingeweza kurecord tukio lile, unamuumiza mtu na unamdhalilisha.
Sisi wazalendo tuchukue hatua za kudhibiti ukatili unaojionyesha kwa watoto wetu angali wadogo, tuwafundishe watoto wetu kuheshimu wanawake, tuwakanye kuhusu kulipiza kisasi, tuwafundishe kuhusu kusamehwme.
Mfano mzuri wa binadamu aliyekamilika tunauona kwa Dr Samia, anatufundisha kwa vitendo kuhusu kusamehe, kuridhiana, kujadiliana na kupendana.
Nafikiri chanzo cha tukio kinatokana na kutokuwa na uvumilivu, kuwa na kiwango kikubwa cha chuki na kulipiza kisasi, kama wale vijana walitumwa na mwanamke kwa wivu wa mapenzi basi somo kuhusu uvumilivu, kusamehe, kuridhiana na kukubali uhalisia litiliwe mkazo, kama kuna hali ya matatizo kwenye ndoa ni bora tuzungumze, tukishindwa tuvishirikishe vyombo mbalimbali vya kuleta maridhiano, kama BAKWATA, taasisi za usuluhishi na maridhiano, na mabaraza mengine ya kidini.
Upande wa pili ndugu zetu watumishi wa umma, tunawaomba mzidishe upendo kwetu mkumbuke nyinyi mpo hapo kwa ajili ya kutuhudumia na si kutuumiza, sisi tunawapenda sana, ila kuna wenzenu wanashindwa kutoa huduma sahihi.
Mwisho nitoe pongezi kubwa sana kwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es Salaam, kwa sisi tulokuwa kwenye uwanja wa Taifa tumeshuhudia hali ya utulivu na amani pamoja na idadi kubwa ya washabiki wa mpira wa miguu, tukamkanda mtani goli moja kila mtu akalala unono
NDIMI
Comrade Ally Maftah
PAKOME WA MCHONGO
Comrade Wa Yanga
Na Comrade Ally Maftah
Nilipata kusikia tukio la dada aliyefanyiwa ukatili wa kijinsia nikajidhibiti sana nisitazame tukio hilo, ila kwa bahati mbaya sana nimeona kipande kidogo cha tukio lile.
Tukio limenitafakarisha mno nimejiuliza maswali mengi sana baada ya kuona tukio lile.
1. Nimemwona mwathirika akiomba radhi na kusema hatorudia tena, lakini jamaa walikosa utu kabisa, hawakuguswa kabisa na msamaha aloomba mwathirika.
2. Kuna sauti inaashiria watendaji wa jambo ni watumishi wa uma, ambao wanalipwa kwa kodi zetu.
3. Uungwana na ustaarabu wa mwafrika ulipotea kabisa, utendaji wa uhalifu pamoja na uchukuaji wa video haikuwa taratibu za tamaduni zetu, tendo lililofanyika haliweze kutendwa na mtu mwenye hekima, na mtu asingeweza kurecord tukio lile, unamuumiza mtu na unamdhalilisha.
Sisi wazalendo tuchukue hatua za kudhibiti ukatili unaojionyesha kwa watoto wetu angali wadogo, tuwafundishe watoto wetu kuheshimu wanawake, tuwakanye kuhusu kulipiza kisasi, tuwafundishe kuhusu kusamehwme.
Mfano mzuri wa binadamu aliyekamilika tunauona kwa Dr Samia, anatufundisha kwa vitendo kuhusu kusamehe, kuridhiana, kujadiliana na kupendana.
Nafikiri chanzo cha tukio kinatokana na kutokuwa na uvumilivu, kuwa na kiwango kikubwa cha chuki na kulipiza kisasi, kama wale vijana walitumwa na mwanamke kwa wivu wa mapenzi basi somo kuhusu uvumilivu, kusamehe, kuridhiana na kukubali uhalisia litiliwe mkazo, kama kuna hali ya matatizo kwenye ndoa ni bora tuzungumze, tukishindwa tuvishirikishe vyombo mbalimbali vya kuleta maridhiano, kama BAKWATA, taasisi za usuluhishi na maridhiano, na mabaraza mengine ya kidini.
Upande wa pili ndugu zetu watumishi wa umma, tunawaomba mzidishe upendo kwetu mkumbuke nyinyi mpo hapo kwa ajili ya kutuhudumia na si kutuumiza, sisi tunawapenda sana, ila kuna wenzenu wanashindwa kutoa huduma sahihi.
Mwisho nitoe pongezi kubwa sana kwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es Salaam, kwa sisi tulokuwa kwenye uwanja wa Taifa tumeshuhudia hali ya utulivu na amani pamoja na idadi kubwa ya washabiki wa mpira wa miguu, tukamkanda mtani goli moja kila mtu akalala unono
NDIMI
Comrade Ally Maftah
PAKOME WA MCHONGO
Comrade Wa Yanga