Tukilimaliza la Feisal Salum tulirudie la SportPesa

Tukilimaliza la Feisal Salum tulirudie la SportPesa

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Wakati mgogoro wa Yanga na Feisal Salum ukionekana ukienda kumalizika, tukumbuke pia kulikuwa na mgogoro mwingine wa kimkataba kati ya Yanga na mdhamini wao mkuu SportPesa.

Ilionekana kutokana na ratiba ngumu za mashindano, mgogoro wa Yanga na SportPesa uwekwe pembeni kwanza hadi msimu utakapoisha. Za ndaaani inasemekana SportPesa mpaka sasa wamegoma kulipa bonus zozote za ligi ya NBC na zile za Kombe la Shirikisho kutokana na wao kuamini kuwa makubaliano ya mkataba yalikiukwa.

Kama mnakumbuka M-Bet walitangaza kulipa bonus baada ya Simba kuvuka hatua ya makundi ila mpaka leo hatujawahi kusikia SportPesa wakifanya hivyo kwa Yanga.

Kilichokuwa kinaleta ugumu zaidi katika mgogoro huu ni muingiliano wa maslahi uliopo kutokana na Abbas Tarimba kuwa si tu mtu muhimu ndani ya SportPesa lakini akiwa pia na maslahi ndani ya Yanga na ameonekana kuweka maslahi ya Yanga mbele zaidi ya SportPesa.

Kuonyesha Yanga wanajaribu kuwapoza SportPesa sasa hivi kuelekea mwishoni mwa msimu, wakijua lolote linaweza kutokea hasa kutoka makao makuu ya SportPesa, wakati wa halfa ya chakula iliyofanyika Ikulu, Yanga walivaa jezi zenye nembo ya SportPesa badala ya mdhamini wao wa Kombe la Shirikisho ambao ni kampuni ya Haier.
 
Tatizo la Sportpesa hawana balls kwenye misimamo yao.

Abbasi Tarimba mara ya mwisho kuzungumzia hili swala alisema watatumia busara hivyo ilionesha ile kauli yao ya kuitaka Yanga watoe nembo ya mdhamini mpya ilikuwa kama ni kuufyata tu.

Kauli yao ilionekana kama Sportpesa wamekubali kuwa wanyonge

Na Yanga ni kama amefanya hivi makusudi akijua Sportpesa lazima atakuwa mnyonge kutokana ma kwamba nje ya Simba na Yanga Sportpesa hawezi ku brand biashara yake.

Na kwasababu Simba alikwisha jitoa hivyo kwa Sportpesa ni kama Yanga ndio only asset aliyobakia nayo.

Lakini pia kuna habari zinadai kuwa moja ya sababu za Yanga kumleta mdhamini mpya bila authorization kutoka kwa Sportpesa ni kwasababu huyo Haier anataka kuwa main sponsor

So ni kama wanamtafutia sababu tu Sportpesa.
 
Sawa


yangasc-20230607-0001.jpg
 
Tatizo la Sportpesa hawana balls kwenye misimamo yao.

Abbasi Tarimba mara ya mwisho kuzungumzia hili swala alisema watatumia busara hivyo ilionesha ile kauli yao ya kuitaka Yanga watoe nembo ya mdhamini mpya ilikuwa kama ni kuufyata tu...
Uko sahihi, Yanga walijua SportPesa hawawezi kufurukuta ila nao SP wanaweza kuwabana Yanga kwa njia watakayoona inafaa bila kuvunja mkataba mfano kama hili la kutotoa bonus, msimu ujao wanaweza kupiga panga lingine kwenye pesa za udhamini.

Binafsi sidhani kama Haier wanaweza kutoa udhamini kama wa SportPesa maana aina ya biashara yao haina mrejesho mkubwa kifedha katika uchumi kama wetu ila tusubiri tuone.
 
Sidhani kama Haier wanaweza kutoa udhamini kama wa SportPesa maana aina ya biashara yao haina mrejesho mkubwa kifedha katika uchumi kama wetu ila tusubiri tuone.
Hiyo ni kampuni kubwa Mkuu hata revenue yake kwa mwaka ni pesa nyingi haiwezi kushindwa kutoa hela ya udhamini
 
Hiyo ni kampuni kubwa Mkuu hata revenue yake kwa mwaka ni pesa nyingi haiwezi kushindwa kutoa hela ya udhamini
Sijakataa kuwa ni kubwa ila ninaona ugumu wa wao kuweka kiasi kama cha SP kwenye marketing unless Yanga wanataka tu kuachana na SP kwa sababu zingine na wako tayari kuwa na udhamini mdogo zaidi ya ule wa SP.

Ila wakiweza kuwauzia idea kuwa Yanga itaendelea kufanya vizuri kimataifa wanaweza kuweka mzigo wa kueleweka maana wataweza kutangaza bidhaa zao sehemu nyingine Afrika nje ya Tanzania kwa kupitia mafanikio ya Yanga ila kwa soko la Bongo pekee udhamini huo hauwezi kuwalipa.
 
Tatizo la Sportpesa hawana balls kwenye misimamo yao.

Abbasi Tarimba mara ya mwisho kuzungumzia hili swala alisema watatumia busara hivyo ilionesha ile kauli yao ya kuitaka Yanga watoe nembo ya mdhamini mpya ilikuwa kama ni kuufyata tu...
Ufafanuzi mzuri
 
Sijakataa kuwa ni kubwa ila ninaona ugumu wa wao kuweka kiasi kama cha SP kwenye marketing unless Yanga wanataka tu kuachana na SP kwa sababu zingine na wako tayari kuwa na udhamini mdogo zaidi ya ule wa SP...
Nakubaliana na wewe

Lakini pia

Sababu kuu inayotajwa ni kupitia mahusiano ya GSM na Haier.

Haier amekuwa akishirikiana na GSM kwenye maswala ya kibiashara na ukicheki GSM ndio joint pale Yanga.
 
Back
Top Bottom