Diwani
JF-Expert Member
- Oct 25, 2014
- 2,680
- 2,779
Katika maisha licha ya kuwepo na changamoto nyingi, kuna matukio ama changamoto ambazo zinakaa ndani ya mioyo yetu bila kutoka kwa sababu ya uzito wake hasa pale yanapo tufanya tunusurike kifo.
Niende kwenye tukio, Mwaka 2019, jijini Dodoma, kwa uwezo wa Mungu nilifanikisha kupata kaelimu kangu ka chuo, sasa wakati wa mahafali, nilitembelewa na wazazi wangu pamoja na dada yangu.
Wakati tunatoka ukumbini, kwa ajili ya kwenda kusheherekea nje ya mji, nikawa napiga piga picha na rafiki zangu, kitendo kilichofanya wazazi wangu watangulie na kunipa muda wa mimi kuendelea na ratiba zangu, wakaniambia tu, “tutakutana hotelini pale” nikawaambia hakuna shida, nikaanza kupiga picha, mara stori za hapa na pale ili mradi tu, tusemezane neno la mwisho kila mtu akipotea kwenye uso wa mwenziwe iwe kwaheri.
Sasa basi; shida ikaja kwenye usafiri wa kutupeleka huko kwenye shughuli baada ya pale ukumbini, si gari, bajaji wala boda boda iliyokuwa na nafasi ya mimi kujiegesha, zote zimejaa, nikawa nashuka mdogo mdogo nikitaraji nitapata hata boda huko mbeleni, ghafla ikaja dala dala imejaa, ila kuna mahala pa kuning’inia mlangoni, mwanaume nikajiweka, hapo nipo kwenye suti, nimeshika maji kichwani nimevaa kofia ya muhitimu [emoji310] nikaanza kushika bomba, safari ikaanza, gari ikaanza kutembea, sasa kwa kuwa kwa kimo cha pale nilikuwa mrefu kidogo, nikaamua kuivua ile kofia nikamvalisha kondakta, gari ipo kwenye moto na ndio ilikuwa inashuka mlima, konda yupo mbele yangu, tunaning’inia wote mlangoni, mara upepo mkali ukaja ukapita na ile kofia kichwani kwa konda, ghafla kama wenge hivi nikajikuta najaribu kuikamata mguu ukateleza nikaenda chini na hapo gari ipo mwendo, nikabiringika kwenye rami nikazunguka kama mara tatu hivi halafu nikaingia mtaroni kabisa.
Mwili mzima unaniuma, nikawa nimechunika na suti ishachanika hapo, sio suruali wala koti, watu kwenye gari wakabaki wametahamaki wakajua ndio tayari hivyo, kwisha habari yangu nikawa nawasikia akina mama kwa mbali wanapiga yowe, mwanaume nikaamka najikongoja, walivoona vile wakanikimbilia, nikaenda mdogo mdogo naifuata kofia, damu zinatoja mkononi, nikaichukua nikawa narudi kwenye gari, nikapanda gari watu hawaamini kama ndio mimi, safari ikaendelea, nashuka ndio nikaanza kujua kumbe nimeumia sana ndani kwa ndani, nikaamua kwenda kwa fundi watu wananishangaa, uzuri ni kuwa fundi mwenyewe alikuwa anashonea ndani kwake, hivyo nilikaa humo ndani nikajipa huduma ya kwanza.
Nikapigiwa simu nipo wapi, nikawa naongea kwa upole kweli, nikakaa pale kama nusu saa hivi kisha ndio nikaenda kule, mwili mzima unaniuma lakini hakuna aliwahi kujua nini kimenitokea (hadi leo) nilikaa chini kwenye kiti sijanyanyuka mpaka shughuli inaisha.
Vipi kwa upande wako?
Niende kwenye tukio, Mwaka 2019, jijini Dodoma, kwa uwezo wa Mungu nilifanikisha kupata kaelimu kangu ka chuo, sasa wakati wa mahafali, nilitembelewa na wazazi wangu pamoja na dada yangu.
Wakati tunatoka ukumbini, kwa ajili ya kwenda kusheherekea nje ya mji, nikawa napiga piga picha na rafiki zangu, kitendo kilichofanya wazazi wangu watangulie na kunipa muda wa mimi kuendelea na ratiba zangu, wakaniambia tu, “tutakutana hotelini pale” nikawaambia hakuna shida, nikaanza kupiga picha, mara stori za hapa na pale ili mradi tu, tusemezane neno la mwisho kila mtu akipotea kwenye uso wa mwenziwe iwe kwaheri.
Sasa basi; shida ikaja kwenye usafiri wa kutupeleka huko kwenye shughuli baada ya pale ukumbini, si gari, bajaji wala boda boda iliyokuwa na nafasi ya mimi kujiegesha, zote zimejaa, nikawa nashuka mdogo mdogo nikitaraji nitapata hata boda huko mbeleni, ghafla ikaja dala dala imejaa, ila kuna mahala pa kuning’inia mlangoni, mwanaume nikajiweka, hapo nipo kwenye suti, nimeshika maji kichwani nimevaa kofia ya muhitimu [emoji310] nikaanza kushika bomba, safari ikaanza, gari ikaanza kutembea, sasa kwa kuwa kwa kimo cha pale nilikuwa mrefu kidogo, nikaamua kuivua ile kofia nikamvalisha kondakta, gari ipo kwenye moto na ndio ilikuwa inashuka mlima, konda yupo mbele yangu, tunaning’inia wote mlangoni, mara upepo mkali ukaja ukapita na ile kofia kichwani kwa konda, ghafla kama wenge hivi nikajikuta najaribu kuikamata mguu ukateleza nikaenda chini na hapo gari ipo mwendo, nikabiringika kwenye rami nikazunguka kama mara tatu hivi halafu nikaingia mtaroni kabisa.
Mwili mzima unaniuma, nikawa nimechunika na suti ishachanika hapo, sio suruali wala koti, watu kwenye gari wakabaki wametahamaki wakajua ndio tayari hivyo, kwisha habari yangu nikawa nawasikia akina mama kwa mbali wanapiga yowe, mwanaume nikaamka najikongoja, walivoona vile wakanikimbilia, nikaenda mdogo mdogo naifuata kofia, damu zinatoja mkononi, nikaichukua nikawa narudi kwenye gari, nikapanda gari watu hawaamini kama ndio mimi, safari ikaendelea, nashuka ndio nikaanza kujua kumbe nimeumia sana ndani kwa ndani, nikaamua kwenda kwa fundi watu wananishangaa, uzuri ni kuwa fundi mwenyewe alikuwa anashonea ndani kwake, hivyo nilikaa humo ndani nikajipa huduma ya kwanza.
Nikapigiwa simu nipo wapi, nikawa naongea kwa upole kweli, nikakaa pale kama nusu saa hivi kisha ndio nikaenda kule, mwili mzima unaniuma lakini hakuna aliwahi kujua nini kimenitokea (hadi leo) nilikaa chini kwenye kiti sijanyanyuka mpaka shughuli inaisha.
Vipi kwa upande wako?