Mzalendo120
JF-Expert Member
- Jul 2, 2022
- 1,842
- 2,410
Habari zenu wanajukwaa.
Pia soma > Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa
Suala lililoshika kasi sana jana tarehe 08/09/22 ni sakata la kibanda cha mlinzi huko Uyui mkoani Tabora kugharimu milioni 11 za kitanzania
Katika hali isiyo ya kawaida eti mkuu wa mkoa nae anakua mkali kuhoji. Sasa anahoji nini wakati alitakiwa ahojiwe? Hapo balozi Batilda amepwaya na aibu kubwa sana kwake. Hii inatoa taswira kwamba viongozi wote waliohusika niwazembe au wamegawana fedha hizo za tozo
Hii ni aibu kwa mkuu wa mkoa kwenda na waziri mkuu kwenye mradi ambao yeye hajawahi hata kujua gharama ya mradi hata wa kibandatu cha mlinzi!!! Aibu kubwa sana kwa mkuu wa mkoa wa Tabora
Kama ambavyo waziri mkuu ametoa maelekezo kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi inabidi waanze na mkuu wa mkoa na wasaidizi wake kwenye masuala ya ujenzi ndio itapatikana picha kamili.
Ingekuwa kuna uwajibikaji wa dhahiri,mkuu wa mkoa na timu yake wangepisha uchunguzi
Haiwezekani tozo zikaliwa kizembe kiasi hicho
Pia soma > Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa
Suala lililoshika kasi sana jana tarehe 08/09/22 ni sakata la kibanda cha mlinzi huko Uyui mkoani Tabora kugharimu milioni 11 za kitanzania
Katika hali isiyo ya kawaida eti mkuu wa mkoa nae anakua mkali kuhoji. Sasa anahoji nini wakati alitakiwa ahojiwe? Hapo balozi Batilda amepwaya na aibu kubwa sana kwake. Hii inatoa taswira kwamba viongozi wote waliohusika niwazembe au wamegawana fedha hizo za tozo
Hii ni aibu kwa mkuu wa mkoa kwenda na waziri mkuu kwenye mradi ambao yeye hajawahi hata kujua gharama ya mradi hata wa kibandatu cha mlinzi!!! Aibu kubwa sana kwa mkuu wa mkoa wa Tabora
Kama ambavyo waziri mkuu ametoa maelekezo kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi inabidi waanze na mkuu wa mkoa na wasaidizi wake kwenye masuala ya ujenzi ndio itapatikana picha kamili.
Ingekuwa kuna uwajibikaji wa dhahiri,mkuu wa mkoa na timu yake wangepisha uchunguzi
Haiwezekani tozo zikaliwa kizembe kiasi hicho