IHOLOMELA
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,807
- 1,675
Habari Wakuu.
Kama ilivyosikika na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii juu ya tukio la kuvamiwa na kuchomwa moto kwa kituo cha polisi na baadhi ya vibanda vya biashara na nyumba za askari huko Simiyu.
Inasemwa kuwa tayari raia 27 wamekamatwa kwa tukio hilo ila hatujasikia askari waliouwa watuhumiwa wa wizi kukamatwa. Ikumbukwe kwamba, chanzo cha wananchi kuvamia na kufanya uharibifu huo ni baada ya vijana wawili kuuwawa wakiwa ndani ya kituo hicho, wasingeuwawa hizo fujo zisingetokea.
Kwa kuwa hadi sasa hakuna taarifa za kukamatwa kwa chanzo cha vurugu (Polisi), je kuna haja ya kuliomba jeshi la polisi kuwakamata hao askari waliosababisha?
Nawasilisha kwa hatua zenu.
Kama ilivyosikika na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii juu ya tukio la kuvamiwa na kuchomwa moto kwa kituo cha polisi na baadhi ya vibanda vya biashara na nyumba za askari huko Simiyu.
Inasemwa kuwa tayari raia 27 wamekamatwa kwa tukio hilo ila hatujasikia askari waliouwa watuhumiwa wa wizi kukamatwa. Ikumbukwe kwamba, chanzo cha wananchi kuvamia na kufanya uharibifu huo ni baada ya vijana wawili kuuwawa wakiwa ndani ya kituo hicho, wasingeuwawa hizo fujo zisingetokea.
Kwa kuwa hadi sasa hakuna taarifa za kukamatwa kwa chanzo cha vurugu (Polisi), je kuna haja ya kuliomba jeshi la polisi kuwakamata hao askari waliosababisha?
Nawasilisha kwa hatua zenu.