Tukisema tufanye jaribio kwa watu wanaomiliki leseni za udereva, wangapi watapopolewa?

Tukisema tufanye jaribio kwa watu wanaomiliki leseni za udereva, wangapi watapopolewa?

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Ukiuliza watu wanaomiliki leseni za udereva walipata vipi leseni zao, asilimia kubwa watakwambia nilipiga mishe nikapita huku na kule nikapata leseni yangu. Wengi wa madereva hawa wanaomiliki leseni hizi hawajawahi kupata mafunzo rasmi ya udereva, jambo linalochangia kuwa na madereva ambao wawajui lolote kuhusu taaluma hii.

Unakuta mtu ni dereva wa chombo fulani cha usafiri lakini hata alama za barabarani tu hajui zinamaanisha nini. Mara nyingi watu hutafuta jamaa zao wanaojua kuendesha chombo husika, anamfundisha siku mbili tatu, akikariri vizuri basi anaingia barabarani halafu ndio unafuata mchakato wa kufanya mishemishe ili apate leseni. Jambo hili linasababisha matatizo mengi sana ikiwemo ongezeko hili la ajali tunalolishuhudia kila kukicha.

Je, tukisema leo tufanye jaribio kwa wamiliki wote wa leseni za udereva, unafikiri wangapi wataendelea kumiliki leseni zao?​
 
Mimi mzee wangu kaanza endesha gari enzi za Nyerere mpaka mwaka jana anafariki hakuwahi miliki leseni ya gari na hakuwahi simamishwa na trafiki akamdai leseni. Walikuwa tu wana assume anayo.

Ila alipata stroke upande wa kushoto 2014 so akawa hana uwezo wa kuendesha gari hivyo mfumo wa makosa ya barabarani kuambatana na namba ya leseni ungemuumbua.
 
Mimi mzee wangu kaanza endesha gari enzi za Nyerere mpaka mwaka jana anafariki hakuwahi miliki leseni ya gari na hakuwahi simamishwa na trafiki akamdai leseni....
Mimi mwenyewe niliwahi kuendesha gari kwa miaka 8 bila ya leseni, na sikuwahi kupata ajali ya aina yoyote ile!

Na mara zote matrafiki waliamini nilipowaambia nimeisahau nyumbani. Maana wakiangalia gari lenyewe wanakuta ni manual! Hivyo wanaamini tu kirahisi.

All in all, umakini na kufuata sheria za usalama barabarani, ndiyo kila kitu uwapo barabarani.
 
Hata kama huna taaluma ya udereva kuna baadhi ya sehemu unaona kabisa hatari inayoweza kuwepo lakini unakuta dereva anapuuzia
 
hahaaaa leo asubuhii dereva mmoja kapigwa full light, akayumbaaa yumbaa yaaniii wanaoendesha manual wataponaaa

wa passo/vits/istz wanajua tu kukanyaga clutch
 
Mimi mwenyewe niliwahi kuendesha gari kwa miaka 8 bila ya leseni, na sikuwahi kupata ajali ya aina yoyote ile!

Na mara zote matrafiki waliamini nilipowaambia nimeisahau nyumbani. Maana wakiangalia gari lenyewe wanakuta ni manual! Hivyo wanaamini tu kirahisi.

All in all, umakini na kufuata sheria za usalama barabarani, ndiyo kila kitu uwapo barabarani.
😀😀😀
 
Zamani Barabara nyingi zilikuwa za vumbi na za lami zilikuwa hadi ile michoro inapauka na kwisha kabisa sasa ishara nyingi zilikuwa ni Daraja na kona.
 
Back
Top Bottom