Tukiwekeza kwa matajiri wanaotokana na viwanda na kilimo, umasikini utakuwa ni historia

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Mtazamo wangu;

Kama tukichukua matajiri wakubwa 1000 wanaotokana na umiliki wa viwanda; viwe vya kati au vikubwa.

Pamoja na matajiri 1000 wanaotokana na kilimo; wakapewa sera nzuri ya kodi, sera nzuri kwa masoko ya nje, sera nzuri katika kuagiza vipuli, na wakawezeshwa kwenye mitaji ya kutosha n.k

Ndani ya muda mfupi, tatizo la ajira litakuwa limeisha na uchumi utakuwa kwa kasi sana.

Kitakachotokea ni nini?​
  • Viwanda vikubwa na vidogo vitakuwa vingi​
  • Upatikanaji wa bidhaa utakuwa mkubwa​
  • Fedha za kigeni zitakuwepo za kutosha​
  • Mashamba makubwa na ya kisasa kila kanda yatakuwepo​
  • Watu wengi sana wataajiriwa​
  • Ukuaji wa teknolojia utakuwa kwa kasi​
  • Utaongeza ukuaji katika sekta zingine​
  • Mapato ya serikali yataongezeka​
  • Hakutokuwa na njaa​
  • Uagizaji bidhaa nje utapungua na kuimarisha uchumi n.k​
 
Ujinga na umaskini wa wengi ndio mtaji wao wa kuongoza na kutawala wajinga. Mipango inawezekana asubuhi tu hiyo wala haina haja ya kuiletea siasa.
 
Kuna kauli askofu Gwajima huwa anaongelea bungeni kuhusu maono ya nchi nadhani wengi hawajamulewa
Jamaa anahoja ya msingi sana
 
Mkuu siyo rahis kihivyo kwa mbongo
 
Mkuu nikikumbuka Takri ninalia. Nimeshaishi huko.
 
Mkuu siyo rahis kihivyo kwa mbongo
Nadhani kama kipaumbele kitakuwepo, pamoja na sera kuwa nzuri; watu wenye mitaji katika hayo maeneo watajiorodhesha, na kupewa semina kuhusu nini cha kufanya.

Na hakika wafanyabiashara (wenye viwanda, wakulima wakubwa) wako tayari muda wowote kuingia kazini; muhimu kwa sasa ni maazimio ya vitendo tu.
 
Tupo watu wenye mitaji. Tatizo serikali yenu na muundo wa utawala wa Tanzania, kila kiongozi anayeingia madarakani anakuja na lake! Mie nikitaka kuweka mabilioni yangu kwenye heka kama 500 napata wasiwasi baada ya awamu hii kwisha je ijayo itaweza kuniwekea mazingira mazuri ya shughuli zangu?? Au viongozi wataanza kuja kunisumbua na vishida vyao. Hapo tu ndipo panaporudisha nyuma Tanzania
 
Mdomo kila mtu anao ila tunafikaje huko ndio hakuna ulichoonesha..

JK alikuja na mpango mzuri Sana wa kuwaleta hao matajiri kwa njia za kuwapa tax holidays ila wajinga wakaanza makelele mara ooh hawalipi Kodi wanatuibia na blaa blaa zingine za kijinga..

No way out kutakuwa na investment kwenye kilimo bila kutoa incentives kwa investors na pia kuwapa ardhi wafanye large scale farming..
 
Mchakato unatakiwa uanzie kwenye wizara husika, baadaye bungeni kwa ajili ya sheria
 
Mchakato unatakiwa uanzie kwenye wizara husika, baadaye bungeni kwa ajili ya sheria
Sheria zipo Wala haihitaji mchakato bali uelewa tuu wa watu na utashi wa kisiasa..

Tukianza hivyo utasikia wanyonge wakianza kulalama na wanasiasa uchwara watasema wakulima wadogo wataporwa ardhi Ili kuwapa matajiri na hapo utasikia shamba la Riz Moko mara Makamba mara Mwigulu na upuuzi kama huo..

Twende hivi hivi Ili akili zitukae vizuri,tulikuwa na mradi hapa wa feed the future,sagot,kilimo kwanza,Big result now nk ila yakapigwa chini na Mwendazake akaenda kujenga sgr nk..
 
Ulimwengu wa sasa bila kuupeleka kibepari, maendeleo yatachelewa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…