Tukizeeka tutaishi vipi

Kisanduku

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2009
Posts
284
Reaction score
483
Ukweli ni kwamba tunaishi kwa kubahatisha bila kujua hatima yetu itakuwaje huko mbeleni.

Ninachojua nchi nyingi Ulaya na America, wao kwa kulijua tatizo hili basi wazee wanapofika umri wa kutojiweza wanawekwa kwenye quarters zao na huko kuna wangalizi maalum.

Hapa kwetu hakuna hilo. Ukimuuliza mzee akiishiwa nguvu kila mmoja ana jibu lake mwenyewe.

Kuna majibu kwamba watoto watakutunza. Lakini huko sasa hivi ni kubahatisha kwani huyo mtoto huna hakika atakuwa katika hali gani au nafasi gani katka dunia hii. Na anaweza akafa vilevile. Pia wategemezi wa hali hii inabidi sasa ukizeeka unyenyekee sana hao watoto ata kama unanyimwa stahili zako, maana wanaktunza.

Mimi nadhani tunajidanganya kutoliona hili kama ni tatizo. Leo tunachemka, tunabinyeza keyboard lakini ukweli ni kwamba tutazeeka na tutaishiwa nguvu. Je, tutaishije kipindi hicho.

Nimetoka majuzi kumtembelea shangazi yangu. Utotoni pale kwa shangazi kulijaa watu wa kila aina na kulichangamka kwa shughuli mbalimbali. Leo nimeguswa kuona shangazi yuko peke yake na anamuuguza mume wake kama vile hana watoto wakati ana watoto wanne wakubwa na kila mmoja anasema yuko bise na familia yake!

Shangazi anasema walitumia akili sana kujenga nyumba ambayo wameweza kuweka wapangaji ambao binafsi niliona wanamsaidia kumuuguza yule mume wa shangazi! Bila hivyo basi ina maana shangazi angekaa bila kupangisha basi angekuwa anauguza mwenyewe.

Wakati mnaleta maoni yenu, mimi wazo langu ni kwamba tujipange kuleta system kama ya Ulaya niliyosema. Walioko Ulaya watueleze inafanya kazi kwa kiasi gani. Kama ni kukatwa hela ili zitumike kukutunza uzeeni basi ni heri hizi pensheni ziwe zinalenga huko.

Bila kufikiri hivyo, basi ukweli ni kwamba kizazi cha wazee wa sasa hivi kina nafuu lakini kizazi chetu na uchumi mbovu kila waka sijui hali itakuwaje.

Nawasilisha.
 
Kisanduku,fainali uzeeni.Ukiwa kijana unakuwa na nguvu za kufanya lolote unalotaka,ila uzeeni kama hukujipanga wakati una nguvu ndo unaipata fresh.In comparison bora mama zetu kuliko baba zetu maana watoto wengi huwa na tendency ya kuwa na soft heart kwa mama zao kuliko baba zao na hivyo watoto wanawaangalia zaidi kuliko baba.Ujanani baba utahangaika kusomesha na hata kutoa mtaji wa biashara kwa watoto lakini akili yao itakuwa kumtunza zaidi mama.Ushauri wangu ni kuwa wakati bado tuna nguvu tujipange kwa ajili ya uzee ambao tutakuwa hatutegemei serikali wala watoto.Unaweza kununua vipande UTT,hisa,bonds au kuwa na nyumba za kupangisha.
 
Ujanani ndio wakati wa kulima, kupanda na kupalilia mazao,then uzeen ni mavuno,so uzeen utavuna ulichopanda ujanani!
 
Mi naona twende vijjni.
Sasa hivi watu, hasa vijana, wanakimbia vijijini kwa kasi kubwa. Ndiyo sababu ya ongezeko la watu mijini (urbanization). Miaka ishirini ijayo watu wengi watakuwa mijini kuliko vijijini. Ongeza mchakato wa sasa kwa ardhi kupokonywa na hao wanaoitwa 'wawekezaji', huko vijijini hapatakuwa pa kukimbilia tena. Mimi binafsi tayari ninalo tatizo hilo kwa sababu huko kijijini amebaki mama yangu ambaye ni mzee. Watoto wangu wote wamezaliwa mjini, wako vyuoni na sitegemei kuwa watarudi kijijini. Sijui hatma ya kaya yangu mimi mwenyewe nikizeeka au kufa. Kuhusu mipango ya uzeeni tayari vyombo vipo. Ni kujua namna ya kuvitumia: Mifuko ya pensheni, uwekezaji katika hisa, uwekezaji katika majumba, bima, n.k. Tunapaswa kuanzisha na vingine kama mutual funds au collective investment schemes. Tatizo ni kwamba hatujui namna ya kuvitumia au hatuna imani navyo.
 
Kwa mfanyakazi atakuwa na pensheni, hofu ni kwa wakulima na wasiokuwa na ajira rasmi au zenye uhakika
 
Ni jambo ambalo kama mambo mengi muhimu nchini limeachiwa liende kienyeji hakuna juhudi maalum za wahusika kuliangalia na ndio maana tunayashuhudi ya Tanzaznia legion na ya wataafu wa iliyokuwa EAC.

Ni kweli kizazi cha vijana wa sasa kitakuw an wakati mgumu sana hapo baadae!Mie pia naliunga wazo la kurudi sisi tulionanguvu tukashiriane na wenzetu kule vijijini kwa kuwekeza huko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…