Tukubaliane bila aibu kwamba mchakato wa katiba mpya usimamishwe mara moja.

Tukubaliane bila aibu kwamba mchakato wa katiba mpya usimamishwe mara moja.

milimo

Member
Joined
Nov 29, 2012
Posts
61
Reaction score
32
Ninamwomba sana Mwenyezi Mungu asikie kilio cha watu wengi wanaojali maslahi pana ya wananchi wengi kuhusu kusimamisha mchakato wa kuelekea kwenye upigaji kura za Ndiyo au Hapana kwa katiba inayopendezwa. Karibu watu wote wenye nia njema na nchi hii walipiga kelele, wanapiga kelele na bado wataendelea kupiga kelele kusisitiza kwamba katiba ni suala la MARIDHIANO na wala sio suala la USHINDANI.

Tukubali kwamba tulikosea tangu mwanzo kulifanya jambo la katiba ni la misimamo ya vyama vya siasa na madhehebu ya dini. Na bahati nzuri Mungu ni mwema kwamba kwa hali ilivyo katiba hii haiwezi kupigiwa kura kwa sasa japokua watawala bado wanasisitiza kuwa lazima kura ipigwe. Kwa mazingira yaliyopo haiwezekani labda kama Serikali wameamua kuilipua nchi na baadaye kujilipua wenyewe.

Kwa mtazamo wangu hatua za awali ambazo zilishirikisha watu wenye uelewa na weledi (Tume ya kukusanya maoni, mabaraza ya katiba, na Bunge maalum la Katiba) ndizo zilikua msingi mkubwa wa mafanikio ya katiba mpya. Kwa mawazo yangu hao ndio baadhi ya watu wenye uwezo wa kifikra nchini. Lakini bahati mbaya wote tunakumbuka kilichofanyika kwenye Bunge la Katiba na baadhi ya mabaraza ya Katiba.

Kwenye Bunge la katiba ndiko matumaini ya kupata katiba mpya yenye kutatua matatizo ya kimfumo yanayotusumbua sasa yalizamishwa na kuzikwa hivyo tunaoelewa kidogo tulikata tamaa ya kupata katiba bora. Huko ndiko Maprofesa na Madakatari wa shule walipokua wameamua kujidharirisha wazi wazi kwa michango yao. Kuna wakati fulani nilipokua namwona profesa tena wa siku nyingi anachangia nilitamani kufukia uso wangu chini ya ardhi ili nisiendelee kumsikiliza jinsi anavyodhalilisha wasomi kwa hoja zake.

Hatua zile tatu za mwanzo ndizo zilikua muhimu sana, na baada ya hapo ndio ingeletwa kwetu wananchi wote kwa ajili ya taratibu tu za kuipitisha kwa sababu tulio wengi hata mtugawie hizo katiba pendezwa kila mmoja na yake ili tuzisome, ni wazi kwamba ni asilimia sio zaidi ya kumi (10%) wanaweza kuelewa na kuoanisha na maisha halisi.

Kwa mantiki hiyo, kama tungepiga kura kwa katiba hii pendezwa kama ilivyo na udhaifu pamoja na utangano uliopo, basi MATOKEO YAKE INGEKUA NI KAMA KUFANYA SURVEY YA KUJUA NANI ANASIKILIZWA/KUBALIKA NA WANANCHI KATI YA CCM AU UKAWA.

Mwisho nawashangaa baadhi ya makundi kuipigia kampeni hii katiba ili ipitishwe ati kwa sababu haki zao zimezingitiwa kwenye katiba inayopendekezwa, hivi hawa watu wanaishi kwenye kisiwa peke yao? Huu ni ubinafsi ulipindukia na unatakiwa kudhitiwa mapema sana. Kwa sababu tu maslahi yako yamezingatiwa ati hakuna sababu ya kupigia kelele masuala ya Maadili ya viongozi wa umma, suala la uwajibikaji kwa viongozi wa umma wanapofanya makosa au sehemu wanazosimamia zinapofanya makosa, madaraka makubwa ya Raisi, muundo tata wa muungano.

Kuna siku niliandika na kusema kwamba “muhimu tujadili mambo muhimu yaliyoachwa na mabaya yaliyomo badala ya kujadili yale mazuri ambayo wote tunakubaliana nayo”

Mwenyezi Mungu tunakuomba Ibariki Tanzania ili nchi iwe na Amani ya kweli.
 
Tunasubili miujiza Mh Lubuva na team yake ya tume ya uchaguzi ktk uandikishaji wa wapiga kura takribani 21,000 kwa siku 45 zilizobaki kufikia 30/4/1015.

Bahati nzuri ukawa imetufundisha haki zetu. Kupiga kura ni haki yetu.....hatuwezi kupata haki hiyo pasipo andikishwa....tutaidai kwa nguvu zote.....polisi tuunge mkono kudai haki hiyo...kama hamtaki mtajua jinsi tunavyoweza kudai hski....
 
Ninamwomba sana Mwenyezi Mungu asikie kilio cha watu wengi wanaojali maslahi pana ya wananchi wengi kuhusu kusimamisha mchakato wa kuelekea kwenye upigaji kura za Ndiyo au Hapana kwa katiba inayopendezwa. Karibu watu wote wenye nia njema na nchi hii walipiga kelele, wanapiga kelele na bado wataendelea kupiga kelele kusisitiza kwamba katiba ni suala la MARIDHIANO na wala sio suala la USHINDANI.

Tukubali kwamba tulikosea tangu mwanzo kulifanya jambo la katiba ni la misimamo ya vyama vya siasa na madhehebu ya dini. Na bahati nzuri Mungu ni mwema kwamba kwa hali ilivyo katiba hii haiwezi kupigiwa kura kwa sasa japokua watawala bado wanasisitiza kuwa lazima kura ipigwe. Kwa mazingira yaliyopo haiwezekani labda kama Serikali wameamua kuilipua nchi na baadaye kujilipua wenyewe.

Kwa mtazamo wangu hatua za awali ambazo zilishirikisha watu wenye uelewa na weledi (Tume ya kukusanya maoni, mabaraza ya katiba, na Bunge maalum la Katiba) ndizo zilikua msingi mkubwa wa mafanikio ya katiba mpya. Kwa mawazo yangu hao ndio baadhi ya watu wenye uwezo wa kifikra nchini. Lakini bahati mbaya wote tunakumbuka kilichofanyika kwenye Bunge la Katiba na baadhi ya mabaraza ya Katiba.

Kwenye Bunge la katiba ndiko matumaini ya kupata katiba mpya yenye kutatatua matatizo ya kimfumo yanayotusumbua sasa yalizamishwa na kuzikwa hivyo tunaoelewa kidogo tulikata tamaa ya kupata kataba bora. Huko ndiko Maprofesa na Madakatari wa shule walipokua wameamua kujidharirisha wazi wazi kwa michango yao. Kuna wakati fulani nilipokua namwona profesa tena wa siku nyingi anachangia nilitamani kufukia uso wangu chini ya ardhi ili nisiendelee kumsikiliza jinsi anavyodhalilisha wasomi kwa hoja zake.

Hatua zile tatu za mwanzo ndizo zilikua muhimu sana, na baada ya hapo ndio ingeletwa kwetu wananchi wote kwa ajili ya taratibu tu za kuipitisha kwa sababu tulio wengi hata mtugawie hizo katiba pendezwa kila mmoja na yake ili tuzisome, ni wazi kwamba ni asilimia sio zaidi ya kumi (10%) wanaweza kuilewa na kuoanisha na maisha halisi.

Kwa mantiki hiyo, kama tungepiga kura kwa katiba hii pendezwa kama ilivyo pamoja na utangano uliopo, basi MATOKEO YAKE INGEKUA NI KAMA KUFANYA SURVEY YA KUJUA NANI ANASIKILIZWA/KUBALIKA NA WANANCHI KATI YA CCM AU UKAWA.

Mwisho nawashangaa baadhi ya makundi kuipigia kampeni hii katiba ili ipitishwe ati kwa sababu haki zao zimezingitiwa kwenye katiba inayopendekezwa, hivi hawa watu wanaishi kwenye kisiwa peke yao? Huu ni ubinafsi ulipindukia na unatakiwa kudhitiwa mapema sana.

Kwa sababu tu maslahi yako yamezingatiwa ati hakuna sababu ya kupigia kelele masuala ya Maadili ya viongozi wa umma, suala la uwajibikaji kwa viongozi wa umma wanapofanya makosa au sehemu wanazosimamia zinapofanya makosa, madaraka makubwa ya Raisi, muundo tata wa muungano.

Kuna siku niliandika na kusema kwamba "muhimu tujadili mambo muhimu yaliyochwa na mabaya yaliyomo badala ya kujadili yale mazuri ambayo wote tunakubaliana nayo"

Mwenyezi Mungu tukuomba Ibariki Tanzania ili nchi iwe na Amani ya kweli.

Wewe ndo huitakii mema nchi hii, kwanini usemem mchakato huu muhimu usimamishwe? mie siungi mkono kabisa ushauri wako hapo juu.
 
Wewe ndo huitakii mema nchi hii, kwanini usemem mchakato huu muhimu usimamishwe? mie siungi mkono kabisa ushauri wako hapo juu.

Lumumba buku 7 FC ni vipofu hamuoni. Endeleeni na upofu wenu.
 
Wewe ndio unatakiwa usimamishwe kwa aibu ya kupinga mchakato huu,una hoja dhaifu sana hata sipotezi muda kuchangia kiongozi wenu mmoja aliwahi kusema hawezi kumsusia nyani shamba lake la mahindi halafu akatenda yaleyale aliyokua anayapinga mnachofanya ninyi ni usanii tena na kuwapotezea muda watanzania, na kwa dhambi hii lazima muhukumiwe umesema mwenyewe "Kwenye Bunge la katiba ndiko matumaini ya kupata katiba mpya yenye kutatatua matatizo ya kimfumo yanayotusumbua sasa" Bunge hilo limeshapita muda mrefu sasa sijui unataka bunge ambalo na wewe utakuwemo, hata haueleweki.
 
Wewe ndio unatakiwa usimamishwe kwa aibu ya kupinga mchakato huu,una hoja dhaifu sana hata sipotezi muda kuchangia kiongozi wenu mmoja aliwahi kusema hawezi kumsusia nyani shamba lake la mahindi halafu akatenda yaleyale aliyokua anayapinga mnachofanya ninyi ni usanii tena na kuwapotezea muda watanzania, na kwa dhambi hii lazima muhukumiwe umesema mwenyewe "Kwenye Bunge la katiba ndiko matumaini ya kupata katiba mpya yenye kutatatua matatizo ya kimfumo yanayotusumbua sasa" Bunge hilo limeshapita muda mrefu sasa sijui unataka bunge ambalo na wewe utakuwemo, hata haueleweki.

Acha hasira mtanzania mwenzangu badala yake jenga hoja watu watakuelewa vizuri. Nina imani kuna siku utaelewa tunamaanisha nini baada ya upende mwingine kuwa madarakani. Wengine hutushabikii vyama ila tunataka yeyote atakaye kuwa madaraka utende sawa sawa.
 
Kikwete na serikali yake walikurupuka kufanya mchakatomwa katiba..sasa wamejipakaza mavi mikononi wanashindwa kunawa..hakuna katiba mwaka huu na hilo liko wazi
 
Huyu naye kachoka. Hivi tabia ya kususa watanzania hawa wanaipata wapi. Naanza kuwa na wasi wasi uraia wao. Ngoja tumalize mchakato wa katiba na uchaguzi mkuu ili tuanze ya uraia. Sijui kama opresheni kimbunga ilimaliza kazi yake. Endelea kusema hayo ya kusitisha mchakato, mnaanza na wa katiba mwisho mtasema hata uchaguzi mkuu tuususia. Nilishawambia acheni hizoo! Waza mambo makubwa ya kimaendeleo sio kususa mchakato. Umesikia eeh!
 
ninamwomba sana mwenyezi mungu asikie kilio cha watu wengi wanaojali maslahi pana ya wananchi wengi kuhusu kusimamisha mchakato wa kuelekea kwenye upigaji kura za ndiyo au hapana kwa katiba inayopendezwa. Karibu watu wote wenye nia njema na nchi hii walipiga kelele, wanapiga kelele na bado wataendelea kupiga kelele kusisitiza kwamba katiba ni suala la maridhiano na wala sio suala la ushindani.

Tukubali kwamba tulikosea tangu mwanzo kulifanya jambo la katiba ni la misimamo ya vyama vya siasa na madhehebu ya dini. Na bahati nzuri mungu ni mwema kwamba kwa hali ilivyo katiba hii haiwezi kupigiwa kura kwa sasa japokua watawala bado wanasisitiza kuwa lazima kura ipigwe. Kwa mazingira yaliyopo haiwezekani labda kama serikali wameamua kuilipua nchi na baadaye kujilipua wenyewe.

Kwa mtazamo wangu hatua za awali ambazo zilishirikisha watu wenye uelewa na weledi (tume ya kukusanya maoni, mabaraza ya katiba, na bunge maalum la katiba) ndizo zilikua msingi mkubwa wa mafanikio ya katiba mpya. Kwa mawazo yangu hao ndio baadhi ya watu wenye uwezo wa kifikra nchini. Lakini bahati mbaya wote tunakumbuka kilichofanyika kwenye bunge la katiba na baadhi ya mabaraza ya katiba.

Kwenye bunge la katiba ndiko matumaini ya kupata katiba mpya yenye kutatatua matatizo ya kimfumo yanayotusumbua sasa yalizamishwa na kuzikwa hivyo tunaoelewa kidogo tulikata tamaa ya kupata kataba bora. Huko ndiko maprofesa na madakatari wa shule walipokua wameamua kujidharirisha wazi wazi kwa michango yao. Kuna wakati fulani nilipokua namwona profesa tena wa siku nyingi anachangia nilitamani kufukia uso wangu chini ya ardhi ili nisiendelee kumsikiliza jinsi anavyodhalilisha wasomi kwa hoja zake.

Hatua zile tatu za mwanzo ndizo zilikua muhimu sana, na baada ya hapo ndio ingeletwa kwetu wananchi wote kwa ajili ya taratibu tu za kuipitisha kwa sababu tulio wengi hata mtugawie hizo katiba pendezwa kila mmoja na yake ili tuzisome, ni wazi kwamba ni asilimia sio zaidi ya kumi (10%) wanaweza kuelewa na kuoanisha na maisha halisi.

Kwa mantiki hiyo, kama tungepiga kura kwa katiba hii pendezwa kama ilivyo na udhaifu pamoja na utangano uliopo, basi matokeo yake ingekua ni kama kufanya survey ya kujua nani anasikilizwa/kubalika na wananchi kati ya ccm au ukawa.

Mwisho nawashangaa baadhi ya makundi kuipigia kampeni hii katiba ili ipitishwe ati kwa sababu haki zao zimezingitiwa kwenye katiba inayopendekezwa, hivi hawa watu wanaishi kwenye kisiwa peke yao? Huu ni ubinafsi ulipindukia na unatakiwa kudhitiwa mapema sana. Kwa sababu tu maslahi yako yamezingatiwa ati hakuna sababu ya kupigia kelele masuala ya maadili ya viongozi wa umma, suala la uwajibikaji kwa viongozi wa umma wanapofanya makosa au sehemu wanazosimamia zinapofanya makosa, madaraka makubwa ya raisi, muundo tata wa muungano.

Kuna siku niliandika na kusema kwamba "muhimu tujadili mambo muhimu yaliyochwa na mabaya yaliyomo badala ya kujadili yale mazuri ambayo wote tunakubaliana nayo"

mwenyezi mungu tunakuomba ibariki tanzania ili nchi iwe na amani ya kweli.

wewe kwani hujui kuwa ulikuwepo kisheria ambapo hakuna mwenye kuitengua ama kusimamisha hilo jambo. Hautasimamishwa ng'ooo mpaka atakapokuja yesu kwa mara ya pili labda.
 
Acha hasira mtanzania mwenzangu badala yake jenga hoja watu watakuelewa vizuri. Nina imani kuna siku utaelewa tunamaanisha nini baada ya upende mwingine kuwa madarakani. Wengine hutushabikii vyama ila tunataka yeyote atakaye kuwa madaraka utende sawa sawa.

Eeee eee hapa hakuna hasira ndugu, tunajadili hoja iliyo mbele yetu tunajadili Katiba Pendekezwa ambayo ndio mpango mzima wa kupigiwa kura sasa wewe unaanza kuleta tena kampeni za kushika madaraka, Tanzania ni moja na ni yetu sote tunachokiangalia sasa ni kupiga kura huo upande mwingine unaousema wewe hata si ujui nakuachia wewe!
 
Kikwete na serikali yake walikurupuka kufanya mchakatomwa katiba..sasa wamejipakaza mavi mikononi wanashindwa kunawa..hakuna katiba mwaka huu na hilo liko wazi

Kweli kuna watu humu si waungwana hata kidogo kazi yao ni ku-attack personalities za watu, sio mpango kabisa, ukiona huna hoja unkaa kimya kuliko kutukana na kutumia maneno yasiyoeleweka kama hutopiga kura ni wewe mwenyewe ila wenzio kibao watapiga afu tuone mjanja nani aliyepiga Ndiyo au aliyesusa.
 
Acha hasira mtanzania mwenzangu badala yake jenga hoja watu watakuelewa vizuri. Nina imani kuna siku utaelewa tunamaanisha nini baada ya upende mwingine kuwa madarakani. Wengine hutushabikii vyama ila tunataka yeyote atakaye kuwa madaraka utende sawa sawa.

Wewe kushika madaraka kwa upinzani hilo sahau, usiwe bendera fuata upepo!! Katiba imetulia, isome ujue yaliyomo.
 
Back
Top Bottom