Tukumbuke kufanya mazoezi kuimarisha miwili yetu, Hii ni kwa faida yetu sisi wenyewe

Tukumbuke kufanya mazoezi kuimarisha miwili yetu, Hii ni kwa faida yetu sisi wenyewe

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Leo nikiwa kanisani nilikaa na bibi mmoja, mrembo ametengeneza nywele vizuri, kucha zina rangi na rangi ya mdomo. Bibi huyu alikuwa na fimbo ya kukunja kama kiti aliyokuwa anatembelea.

Kuna wakati alihitaji msaada kidogo lakini alipochoka alikunjua kiti cha fimbo na kukaa. Alivutiwa na moyo wangu wa kusaidia. Baada ya ibada nilimsaidia mpaka nje ya kanisa, aliniambia anaita tax imrudishe kwake. Nilimjibu kuwa ninamuona kama mzazi wangu hivyo asijali. Aliniambia ana umri wa miaka 96.

Nilishtuka nikamuuliza siri ya kuishi umri ule ni nini? Alisema maisha yake ya ujana alikuwa polisi. Hakukua na mapolisi wengi wa kike enzi hizo, nidhamu ya kazi iliwataka wafanye mazoezi ya kwata kila wiki. Alipiga kwata sana. Hata alipopanda cheo hakuacha nidhamu ya kufanya mazoezi. Alistaafu akiwa na cheo cha Kamishna.

Tuliishia kuwa marafiki, aliniambia ana msusi wake anamtembelea kila Jumamosi kumtengeneza kwa nywele za Jumapili. Huyu bibi si kama ma bibi wengi wa miaka 96.
 
Nadhani unatuhakikishia tunaojitahidi kupata mechi za kirafiki kila siku tunaweza kuishi zaidi. Mtaalam mmoja aliniambia, kidume kikimwaga ni sawa na kukimbia km5. Ikiwa nitafanya mechi 1 kila siku kwa wiki inamaana huwa natembea km 35. Haya ni mazoezi mazuri ukimpata partner mzuri
 
Mabibi na mababu wenye afya kabisa wapo, pengine wana afya hata kuwazidi baadhi ya vijana (hapa nazungumzia nguvu kimwili na kiakili.)

Kijijini kuna mabibi na mababu wenye miaka 89+ wanafanya kazi zote za kila siku, kulima, kupika, kwenda mtoni kuchota maji, kupeleka mifugo malishoni n.k

Sehemu nyingine sasa hiki kipindi cha utandawazi, mtu una miaka 50+ umekuwa tayari mtu wa kuangaliwa (umekuwa mzigo tayari).

Ukiangalia vizuri, chakula na kazi (mazoezi) kinachangia kuongeza siku za kuishi!

Mtu unakula asubuhi, mchana unakula, usiku unakula, bado soda, bia, nyama choma za hapa na pale, pamoja na kuwa umekula vyakula vyote hivyo, hufanyi kazi yoyote ya kukifanya chakula ulichokula kifanye kazi.

Matokeo yake, una miaka 30, mafuta yamezidi, umenenepa umekuwa kama nguruwe sasa, umekuwa mzigo kwa watu, hata kubeba kidumu chenye ujazo wa lita tano hauwezi.

Pamoja na yote hayo unaendelea kufakamia kila chakula bila mpangilio.
Unakuja kufikia miaka 45+ hapa sasa umekuwa zaidi ya mzigo.
Ndugu zako hawasemi tu
 
Father of all Snipers,
Wengine wakishakua na watoto basi wamemaliza, hata glass ya maji ya kunywa ataitwa Tom ailete yeye anaangalia TV.
Hizi shughuli za kujihudumia zinachangamsha mwili.
 
Tuache kujifariji eti umri wa kuishi hauongezwi na mazoezi, mazoezi yana nafasi yake katika kuimarisha afya ya mwili!
Na mazoezi siyo kwamba mpaka uende GYM, hapana. Hata kupalilia majani yanayoota nyumbani kwako tayari ni zoezi.

Mwingine hata kufagia tu hawezi, sasa mtu kama huyu kufagia tu hawezi, unatarajia nini. Kuna watu hawajui chochote zaidi ya kula tu, tufanyeni mazoezi kazi wakuu.

Hata kwa wiki au mwezi mara moja siyo mbaya. Mambo ya kusema kufa kupo tu ni kuonesha kwamba umefeli kiasi gani katika uwezo wako wa kimawazo.
 
Back
Top Bottom