Ashadii dadaa, mbona unaniangusha, yaani uoni hikma yake kwenye hizo taboo?
Kabla sijadadaua, inakupasa utambue kwanini waliweka hiyo miko, kwenye jamii. Kwanza ili kutunza kuheshimiana, kutodharauliana na dhana nzima ya usafi wa mwanamke na vitendea kazi.
Kila mtu anaelewa kazi ya kinu, ni kutwanga/kukoboa nafaka, iki ni kifaa muhimu sana na kinatakiwa kupewa hishma yake ili kibakie kwenye hali ya usafi, na ndio maana miko mingi ipo kwenye dhana ya kutishana ili watu waifuate. Ebu mwenyewe fikiria umkute mtu kakalia kitu upande ule wa kutwangia, kisha akipumulie, na kesho atwangie humo humo.
Mf: Ukitaka kuwatisha wanaume wasinywe/kula kinywaji/chakula fulani basi waambie kuwa kula/kunywa kutawapunguzia nguvu za kiume. Ni rahisi sana kuacha kuliko wangeambiwa kutawapelekea kupata saratani (cancer) japo ndio ukweli.
Sasa hapa ujui kuwa wanawake wanatakiwa kuwa wasafi, wao na mazingira yao, hivi kila mwanamke kijijini au mjini au uko mitaani akitupa hizo Space Shuttle za kuendea mwezini, ujui kuwa ni kueneza maradhi kwenye jamii inayo wazunguka.
Hapa tuaelekezwa kuonyesha kuheshimiana, kama wewe unamuona zeruzeru ni mchafu au anakuchefua kwa arufu yake basi temea mate kwenye brouse yako (kama unaweza).
Mwanaume kulia kwenye sufuria ni dalili ya ulafi, kinachokufanya mpaka ule kwenye sufuria ni nini? Ndio wakatishwa kwa kuambiwa hayo waliyo ambiwa.
Kuna lingine dadangu!?