Tukumbushane visa vya Simba wala watu

Tukumbushane visa vya Simba wala watu

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Miaka ya nyumba kulikuwa na visa vingi vya watu kuuliwa ama kujeruhiwa na Simba wala watu.

Wengi wa Simba hao walitajwa kuwa si Simba halisi ila walikuwa ni binadamu waliojibadilisha kuwa Simba.

Miaka ya tisini katikati kuna binamu yetu aliliwa na Simba huko Mtwara.

Lilikuwa na story nyingi sana za kustaajabisha za Simba hao.
1633803580112.png

1633803625936.png

Miongoni mwa stori hizo ni hii:-

Lilikuwa na jamaa alidhulumiwa shamba lake na tajiri mmoja, Basi akafanya jitihada zote ikiwa ni pamoja na kuushirikisha Uongozi wa juu ya Kijiji, lakini hakupata haki yake kwani bwana tajiri alimwaga fedha huko kwa kila mtu.

Alipo ona hajasikilizwa, akaenda kwa mkuu wa wilaya, na bwana kibopa akaitwa huko, Mambo yakawa yaleyale.

Akaenda mkoani na mahakama zote akazimaliza lakini hakupata haki yake.

Basi akaamua kwenda kuisaka haki zake kwa njia zetu zile ambazo hamna atakayekufinya gerezani.

Akaenda Msumbiji, akapewa dawa na masharti, akaambiwa asile damu ila aparueparue tu.

Basi akaelekezwa namna ya kuitumia dawa hiyo kisha akarudi kijijini kwao.

Basi alipofika kijijini akaenda kumvizoa mbaya wake, akamparuaparia, hakuridhika kwa uchungu na hasira aliyokuwa nayo akamla kabisa akbakiza kichwa tu.

Akarudi kwake akagundua kuwa kavunja sharti la kutokunywa damu.

Akajaribu kujirudisha kuwa binadamu Tena, lakini haikuwezekana.

Akaendelea kuuwa watu Hadi pale naye alipouwa na waganga maana watu wa game reserve walisha mshindwa kwani hakuwa wa kawaida.



 
Mmmh mmmh mmmmh ngoja waja waje watuthibitishie kua hii sio green lebel tea
Siti ya kwanza hapa!
 
Miaka ya nyumba kulikuwa na visa vingi vya watu kuuliwa ama kujeruhiwa na Simba wala watu.

Wengi wa Simba hao walitajwa kuwa si Simba halisi ila walikuwa ni binadamu waliojibadilisha kuwa Simba.

Miaka ya tisini katikati kuna binamu yetu aliliwa na Simba huko Mtwara.

Lilikuwa na story nyingi sana za kustaajabisha za Simba hao.
View attachment 1969591
View attachment 1969596
Miongoni mwa stori hizo ni hii:-

Lilikuwa na jamaa alidhulumiwa shamba lake na tajiri mmoja, Basi akafanya jitihada zote ikiwa ni pamoja na kuushirikisha Uongozi wa juu ya Kijiji, lakini hakupata haki yake kwani bwana tajiri alimwaga fedha huko kwa kila mtu.

Alipo ona hajasikilizwa, akaenda kwa mkuu wa wilaya, na bwana kibopa akaitwa huko, Mambo yakawa yaleyale.

Akaenda mkoani na mahakama zote akazimaliza lakini hakupata haki yake.

Basi akaamua kwenda kuisaka haki zake kwa njia zetu zile ambazo hamna atakayekufinya gerezani.

Akaenda Msumbiji, akapewa dawa na masharti, akaambiwa asile damu ila aparueparue tu.

Basi akaelekezwa namna ya kuitumia dawa hiyo kisha akarudi kijijini kwao.

Basi alipofika kijijini akaenda kumvizoa mbaya wake, akamparuaparia, hakuridhika kwa uchungu na hasira aliyokuwa nayo akamla kabisa akbakiza kichwa tu.

Akarudi kwake akagundua kuwa kavunja sharti la kutokunywa damu.

Akajaribu kujirudisha kuwa binadamu Tena, lakini haikuwezekana.

Akaendelea kuuwa watu Hadi pale naye alipouwa na waganga maana watu wa game reserve walisha mshindwa kwani hakuwa wa kawaida.




Hatari kubwa.

Tatizo la hii miziziology ukiamua kuwavaa nayo kina shirro watakumaliza.

Hawa chiboko yao inabakia kuwa hamja mla watu.
 
Mwaka 1995 wakati wa kuanzishwa wilaya mpya ya Mkuranga simba walikuwa wanachomoa watu kwenye fensi za makutii,kila kukicha lazima usikie Kijiji flani Simba kajeruhi au kala mtu.
Mkuu wa wilaya wa wakati huo Kama sikosei Captain Mwabeza aliwaita wazee maarufu ktk naninihiii baada ya kikao Simba wote walipotena kusikojulikana.
 
Mwaka 1995 wakati wa kuanzishwa wilaya mpya ya Mkuranga simba walikuwa wanachomoa watu kwenye fensi za makutii,kila kukicha lazima usikie Kijiji flani Simba kajeruhi au kala mtu.
Mkuu wa wilaya wa wakati huo Kama sikosei Captain Mwabeza aliwaita wazee maarufu ktk naninihiii baada ya kikao Simba wote walipotena kusikojulikana.
Icheki hii ya Simba wa Tunduru

 
Zama hizo kila mtu alikuwa anavaa hirizi
 
Tafuta kitabu kinaitwa Simba wa Tsavo. Kuna stori ndeefu sana kuhusiana na simba wala watu na vituko vyao

Kinaelezea jinsi simba wala watu walivyokua wakitesa na kusumbua wajenzi wa reli iliyopita katika mbuga ya Tsavo kule Kenya
Umenikumbusha Simba wa darajani pale Mikumi, Hadi daraja likaitwa daraja la Simba
 
 
Back
Top Bottom