Tukumbushane vituko tulivyokuwa tunafanya siku ya Krismas enzi hizo

Tukumbushane vituko tulivyokuwa tunafanya siku ya Krismas enzi hizo

XaviMessIniesta

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2017
Posts
2,231
Reaction score
2,778
Duh nakumbuka enzi hizo mwishon mwa miaka ya 90' na mwanzoni mwa 2000s nilikuwa primary

Nakumbuka kuna jamaa ilikuwa kila Sikukuu lazma wapigane had watoane damu, kulikuwa na makundi mawili, Bhukulana na wengine Tangulaza yaan ilikuwa full bifu la kufa mtu.
Bifu lilikuja kuisha baada ya jamaa mmoja kupigwa hadi kuzirai ikibidi members wengi watoroke hadi leo wengi wao sijawah kuwaona
Siku za Sikukuu jamaa walikuwa wanatembea na visu pamoja na katolo(lile kufuri la baiskeli), Ukijichanganya ilikuwa unalimwa katolo ya kichwa.

Nakumbuka pia Disko lilikuwa lifanyikia jeshini pamoja na kuchek movie za kina Vandamme au kina Arnold chini ya tafsiri za Mtaalam Lufufu (R. I. P) Kuna jamaa walifanya fujo kwenye Disko jeshini walilowekwa kwenye Karo la maji hadi asubuhi

Nakumbuka siku ya Sikukuu ndio ilikuwa siku ya kuopoa demu uliyeahidiana naye, wengi ndio walikuwa wanatoroshwa siku hii

Nakumbuka papuchi ya kwanza niliila siku ya Krismas nipo la sita hapo dah msala sana
 
Back
Top Bottom