Tulimnunulia mwanetu kopo la NIDO, limeisha kabla hajayatumia maana nimeyalamba, ni matamu sana

Tulimnunulia mwanetu kopo la NIDO, limeisha kabla hajayatumia maana nimeyalamba, ni matamu sana

Michael Ngusa

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2014
Posts
1,637
Reaction score
463
Majuzi mke wangu alisema mwanetu kafikisha umri wa kuanza kupewa vyakula laini na pia maziwa, asitegemee sana kifua chake. Basi mzee nikazama Nakumatt pale Pugu road, nikaelekezwa sehemu ya maziwa.

Lakini kwakweli sikuona maziwa ya mtoto, sana sana ni ya NIDO ambapo na yenyewe nilikuwa nashangaa mbona yana picha za vijana wakubwa na mama yao, nikasema anyway nisiangaike sana, nikalipia na kumfikishia wife nyumbani.

Siku ya pili nikasema hebu nionje huu unga unga, hawa watu wanayafanyeje maziwa ya ng'ombe yawe unga unga! nikachota kijiko na kuanza kulamba, kwakweli sikuacha, nimeendelea hivyo kila nikirudi kutoka kazini.

Mke wangu alikuwa anasema "wewe utamaliza maziwa ya mtoto!" mie namjibu aaah leo mwisho! najikuta tu naendelea hadi siku hii ya 4 kopo limeisha kabisa na mwanangu akiwa ametumia kama vijiko viwili vitatu tu.

Kusema kweli ni matamu ingawa najuta na nina wasiwasi hii tabia ya lambalamba inaninyemelea, hapa nipo njiani naelekea kumchukulia kopo lingine, nitajitahidi kwakweli zamu hii niuchune.
 
Nani kakwambia NIDO ya wakubwa ni maziwa ya watoto wadogo.... Kama yupo under one year unahatarisha afya ya mtoto
 
Nani kakwambia NIDO ya wakubwa ni maziwa ya watoto wadogo.... Kama yupo under one year unahatarisha afya ya mtoto

Ndio maana anakuwa na SHAPE NZURI, huyu si ndio aliyekuwa anajisifia kuwa ANA BONGE LA SHAPE NA NI MZURI pia Anazalisha watoto wazuri.

SHAPE NZURI LOOOH
 
Majuzi mke wangu alisema mwanetu kafikisha umri wa kuanza kupewa vyakula laini na pia maziwa, asitegemee sana kifua chake. Basi mzee nikazama Nakumatt pale Pugu road, nikaelekezwa sehemu ya maziwa...lakini kwakweli sikuona maziwa ya mtoto, sana sana ni ya NIDO ambapo na yenyewe nilikuwa nashangaa mbona yana picha za vijana wakubwa na mama yao, nikasema anyway nisiangaike sana, nikalipia na kumfikishia wife nyumbani.

Siku ya pili nikasema hebu nionje huu unga unga, hawa watu wanayafanyeje maziwa ya ng'ombe yawe unga unga! nikachota kijiko na kuanza kuramba...kwakweli sikuacha, nimeendelea hivyo kila nikirudi kutoka kazini, mke wangu alikuwa anasema "wewe utamaliza maziwa ya mtoto!" mie namjibu aaah leo mwisho! najikuta tu naendelea hadi siku hii ya 4 kopo limeisha kabisa na mwanangu akiwa ametumia kama vijiko viwili vitatu tu...

Kusema kweli ni matamu ingawa najuta na nina wasiwasi hii tabia ya rambaramba inaninyemelea, hapa nipo njiani naelekea kumchukulia kopo lingine, ntajitahidi kwakweli zamu hii niuchune.

Ndio maana ulikuja kujisifia eti UNA SHAPE nzuri kumbe una "mchina" hahahaha endelea kulamba pengine Utatoka na MAHIPS.
 
Ndio maana anakuwa na SHAPE NZURI, huyu si ndio aliyekuwa anajisifia kuwa ANA BONGE LA SHAPE NA NI MZURI pia Anazalisha watoto wazuri.

SHAPE NZURI LOOOH

Kumbe hamnazo kichwani eeeh.... Daah tumpe pole aiseee
 
Huyu anajutingazia biashara huyu. Eti tabia rambaramba inamnyemelea. Haya bana wamekuelewa
 
Watu wenye tabia kama yako walijikuta wanalamba sumu na wakafa
 
nimeamua kuichukulia kama joke..la sivyo!
 
inaelekea utoton hukulamba mkuu... 😂😂😂😂😀😀😀
 
Mkuu ungejaribu na zile pampers za watoto naimani utazipenda sana
 
Back
Top Bottom