Tuwaulizeni nyie huko ccmVipi hoja yake ilikuwa na mashiko ama la?
Ccm inajifanyia itakavyo sababu ya upumbavu wa wananchi.
Ndugai alikuwa wa kuungwa mkono, lkn ona kilichompata
Makame Mbarawa ni kichaaa. Mama ni kichaaa. Si wamekubali.
Hilo Bunge la wateuliwa wa Magufuli sio Bunge halali.nchi zimeshaingia mkataba hivyo gelesha ya kuupeleka bungeni ni hadaa kwa wananchi
Mkuu hata Ndugai walewale tu sababu hakua ndani ya mfumo tena!! Lkn angesapoti kama angekua bado speaker, mkuu usijewaamin wanaccm!! Imagine ni yeye aliongoza mkakati wa kuvunjwa katiba na kumuongezea Rais muda wa kutawala!! Usiwaamini.Leo ni michano
Kuna watanzania ni machiriku wa kuongea. Wanaongea bila hata kujua maana ya wanachokiongea.
Desemba 28 2021 Spika wa Bunge Ndugai alikosoa kasi ya ukopaji inayofanywa na serikali akitoa tahadhari kuwa kuna siku nchi itakuja kuuzwa.
Wakali wa verse wakalipuka kuwa anaisaliti na kuipinga serikali. Alisutwa akajaa na kujitokea kuomba radhi kwa maoni yake yale. Ikumbukwe serikali inajinasibu kuheshimu Ibara ya 18 ya uhuru wa maoni lakini shahidi wa Nazareti uhuru wake baada ya maoni ulipigwa roba ya mbao na Utawala Bora. Hatimaye akajiuzulu na kukaa kimya.
Hata kabla hatujakaa sawa tukaanza kuona ishu zinapambamoto huko Loliondo, watu wanahamishwa kwa nguvu huku neno hiyari likitumika kuipaka rangi siasa.
Leo nchi nzima inabembelezwa ilie na wale wale machiriku wakidai bandari inauzwa. Wasichokijua ni kwamba hili suala la nchi kuanza kuuzwa halikuanza jana. Wanajua kuwa Ndugage alikuwa sahihi kwani mkataba huu wa Bandari ni chanzo tu cha kupima kina cha maji.
Mkurugenzi wa TPA anasema nchi zimeshaingia mkataba hivyo gelesha ya kuupeleka bungeni ni hadaa kwa wananchi ionekane wabunge waliridhia. Pia hili limevuja ili tusijadili kupinga sheria mbaya kwa taifa ya kutoa kinga kwa wale jamaa zetu wanaonyooshewa vidole kutumika kuua, kuteka, kutesa na kuhukumu wakosoaji wa serikali. Hayo marekebiaho yatapita na hakuna atakayetapinga. Mkataba utapita na povu tunalolitoa leo tutaenda kufulia nguo kesho.
Tufikirie miaka 100 ijayo wajukuu zetu wataishije. Tuache kuwaza kama hatujui kuna kesho. Akina Livingstone. Carl Peters etc walijitoa mhanga kwa ulaya ya leo. Waliishi ndoto na matumaini ya vizazi vya ulaya ya leo.
Sisi tunapambania matumbo yetu.
Unafiki tuache. Tuisaidie nchi. CCM ni kinara wa rushwa na ufisadi na hivi wanajua wananchi wamewachoka, basi wanaingia mikataba isiyoponyeka maana wao na familia zao wataishi kwenye hayo matendo yao maisha yote
Kuuzwa no. Kubinafsishwa miaka mia no pia. Kubinafsishwa miaka isiyozidi 15 kama kuna hela ya maana tutapata kama nchi na maendeleo zaidi ya tupatayo sasa naweza kuelewa. Muda mwingine mashirika ya umma yanashindwa kujiendesha na yanatutia hasara lakini tunaendelea kuyakumbatia kati yanakula hela. Nimechoka kusikia watu wanaibiwa mizigo bandarini mara kuna upigaji bandariniWewe unataka iuzwe au hutaki?
Tatizo hiyo miaka 15 endapo hawatafanya vizuri je hasara kwa nchi si itakuwa kubwa sana?Kuuzwa no. Kubinafsishwa miaka mia no pia. Kubinafsishwa miaka isiyozidi 15 kama kuna hela ya maana tutapata kama nchi na maendeleo zaidi ya tupatayo sasa naweza kuelewa. Muda mwingine mashirika ya umma yanashindwa kujiendesha na yanatutia hasara lakini tunaendelea kuyakumbatia kati yanakula hela. Nimechoka kusikia watu wanaibiwa mizigo bandarini mara kuna upigaji bandarini
Umeandika ujingaTunapotumia madudu ya leo kutaka kuyasafisha/dogosha ya jana, huwa najuliza kama tuna nia ya kweli ya progress au ni mbio za panya za kutukuza tunaowaona wakombozi wetu. End game ni nini? Hii chain ikiendelea hata ya leo yatakuwa dhahabu yakilinganishwa na ya kesho, race to the bottom bila kujifunza.
View attachment 2649877
.Hilo Bunge la wateuliwa wa Magufuli sio Bunge halali.
Naona Kisukari kinaenda kumtwaa.
Lisu aliposema kura zimeibiwa ingia barabarani simlisema ubwabwa mtamu?Siyo bandari tu tena ikiwezekana taasisi zote nyeti wapewe wageni labda tija itapatikana. Watu wetu wengi wamekuwa wezi na mafisadi wakubwa na hawana uchungu na nchi zaidi ya kufikiria maslahi yao binafsi.
Ikiwezekana hata jeshi la polisi wakabidhiwe wageni pengine kuna mabadiliko tutayaona. Kazi yetu kulalamika tu lakini tukipewa nafasi utendaji ni sifuri tu. Angalia kila kitu chetu ni ovyo tu: barabara mbovu, huduma mbovu ili mradi shaghala baghala.
WALIOMSUTA NDUGAI WAKAMWOMBE RADHI KWANI BANDARI IPO CHINI YA DUBAI BADO BAHARI sijui ATAPEWA MCHINA AU MRUSI?Leo ni michano
Kuna watanzania ni machiriku wa kuongea. Wanaongea bila hata kujua maana ya wanachokiongea.
Desemba 28 2021 Spika wa Bunge Ndugai alikosoa kasi ya ukopaji inayofanywa na serikali akitoa tahadhari kuwa kuna siku nchi itakuja kuuzwa.
Wakali wa verse wakalipuka kuwa anaisaliti na kuipinga serikali. Alisutwa akajaa na kujitokea kuomba radhi kwa maoni yake yale. Ikumbukwe serikali inajinasibu kuheshimu Ibara ya 18 ya uhuru wa maoni lakini shahidi wa Nazareti uhuru wake baada ya maoni ulipigwa roba ya mbao na Utawala Bora. Hatimaye akajiuzulu na kukaa kimya.
Hata kabla hatujakaa sawa tukaanza kuona ishu zinapambamoto huko Loliondo, watu wanahamishwa kwa nguvu huku neno hiyari likitumika kuipaka rangi siasa.
Leo nchi nzima inabembelezwa ilie na wale wale machiriku wakidai bandari inauzwa. Wasichokijua ni kwamba hili suala la nchi kuanza kuuzwa halikuanza jana. Wanajua kuwa Ndugage alikuwa sahihi kwani mkataba huu wa Bandari ni chanzo tu cha kupima kina cha maji.
Mkurugenzi wa TPA anasema nchi zimeshaingia mkataba hivyo gelesha ya kuupeleka bungeni ni hadaa kwa wananchi ionekane wabunge waliridhia. Pia hili limevuja ili tusijadili kupinga sheria mbaya kwa taifa ya kutoa kinga kwa wale jamaa zetu wanaonyooshewa vidole kutumika kuua, kuteka, kutesa na kuhukumu wakosoaji wa serikali. Hayo marekebiaho yatapita na hakuna atakayetapinga. Mkataba utapita na povu tunalolitoa leo tutaenda kufulia nguo kesho.
Tufikirie miaka 100 ijayo wajukuu zetu wataishije. Tuache kuwaza kama hatujui kuna kesho. Akina Livingstone. Carl Peters etc walijitoa mhanga kwa ulaya ya leo. Waliishi ndoto na matumaini ya vizazi vya ulaya ya leo.
Sisi tunapambania matumbo yetu.
Unafiki tuache. Tuisaidie nchi. CCM ni kinara wa rushwa na ufisadi na hivi wanajua wananchi wamewachoka, basi wanaingia mikataba isiyoponyeka maana wao na familia zao wataishi kwenye hayo matendo yao maisha yote