Acheni. Tuli hamia kurasini sh.udongo miaka ya 1990, baada ya mzee kuuziwa nyumba pale ikiwa imekimbiwa na mwenye nayo. Inasemekana nyumba alijengea hela ya dhulma, so usiku walikuwa wanakuja mipaka kucheza pale usiku kucha kila siku, na ukimponda anakusemesha, ama unavimba mkono uliompondea.. Ni kweli ilikuwa changamoto sababu paka wana kila milio anzia ya mtoto mdogo hadi ya bi kizee akiongea. So mwenye nyumba aliiuza 4.2mil bei ya hasara. Mzee alikuwa mtu wa kanisani sana hakuamini katika uchawi. Wale paka ukuta wafensi kwanza tukaweka chupa, nakumbuka nimesomba sana chupa kutoka kiwanda cha vioo keko na torori. So ndo ilikuwa njia ya paka. Pili nikatengeneza manati niliwapiga paka hadi wakaacha kuja. Breki yao mzee akaenda kilwa road akauziwa mbwa. Tokea hapo sikuona paka akija