TULIOWAHI KULALA LOCKUP/SELO TUKUTANE HAPA

Mi matusi tu ya afande,

Hata sikumbuki nililala huko kwa nini!
 
Nilimpiga mtu kwa hasira akatoka meno ya mbele na kuchanika mdomo pamoja na kuwa alinikosea sikuonekana nilichokozwa, Hakufai kabisa, simenti baridi, harufu ya mkojo, mmbu, upweke...
 
Dar ni sehemu ngumu yakujifunza maisha nimeingia Mara kadhaa ila sikumoja nilifananishwa na binam yangu tuko rika moja na tunafanana sana ila wakati huo sikujua mpaka alipo kamatwa ndio nikamchunguza wakati huo nimeshakaa siku tano yani hujui kumekucha au ni usiku ni maisha magumu sana
 
Tulijikuta sero kosa hatukulijua kabisa kabisa ; Tulipata kosa tukiwa pale pale ndani ambalo ndilo tulilo litambua rasmi kua ni kosa ... Tulikua watu watatu siku hiyo tulipo ingia sero mdhamana haukukubalika kutokana na ishu kua ya mauaji sisi tulikamatwa eneo la tulio ..

# Tukiwa kizuizini kunajamaa flani alikua mshari sana na mwenye ubabe mwingi nilikua kimya sana
kumcheki jamaa zangu walikua waoga sana kwakweli mana alikua anatembeza Nako mbaya kwa wajamaa pale ndani ...

# Chakula cha madogo alikuwa anakila bila huruma na akuna alie sema kitu anajisaidia na kuamuru madogo wawajibike na usafi ni maneno toka kwa dogo flani aliekua pale ndani na alikua mwanafunzi nadhani aliwekwa pale kama kutishwa anakwenda gerezani mana alikua muhuni flani kwahiyo wazazi walicheza game na mkuu kama jaribio la kumshirikisha adabu ...

# Balaa lilikuja jioni ya siku hiyo hiyo jamaa kajaza alafu kesi yake jambazi ilipelekea watu kumuogopa sana akataka kuja kula kwanguvu jamaa zangu wananiambia mwache ale nikagoma akaleta matusi nikanyamaza siakataka kunipiga na ndoo ya kujisaidia ...

# Kickboxing nadhani mnajua alipo simama sikusubiri apige hatua mawashi ya shingoni hajatua chini ngumi za kichwani kama mvua alipasuka kama kapigwa visu mana alikuwa sio ngumi sana hakuweza kuzinduka pale mpaka alipofika hospitali ya wilaya mzee
 
Daah tusiojua kurusha ngumi tungeteseka sana na huyo jamaa
 
Aise siwezi kusahau ilikuwa mwaka 2010 nikiwa nipo sekondari kuna mzee alikuwa na kawaida ya kutongoza wavulana siku hiyo akaniita akamwaga sera zake kilichofuata baada ya hapo nikampa majibu ya hovyo ambayo yalimuuma na rafiki zangu wakaja nao wakampa matusi ya kutosha,baada ya siku mbili mzee akaenda kushitaki kituoni kwamba sie ni wezi tukaja kukamatwa usiku mida ya saa nane tukiwa tumelala mlango ukagongwa tulifungua tukafungwa mashati na pingu mikononi mpaka kituo cha polisi mpaka asubuhi,tulikamatwa wanne tena wawili tulikuwa wanafunzi,wengine wawili walikuwa saidia fundi garage, asubuhi ikaja kuripotiwa kwamba watoto wamepotea pale kituoni ikabidi afande aulize "ndio yale majambazi tuliyokamata usiku?"cha kushukuru sura zetu na wizi haziendani maana hata bangi wala pombe hatukuwahi kutumia ikabidi afande aelezwe full story A to Z ndio tukaachiwa tena free bila kutoa hata senti,hiyo ndio ilikuwa siku niliyolala selo japo katika maisha yangu nilishajiwekea siku za nyuma kwamba siwezi lala selo mimi,siwezi kusahau aisee
 
Siji sahau siku niliwekwa ndani kisa kuendesha bajaji mpya iliotoka kushuka kwenye gari kupeleka kwa fundi kuiweka vizuri. etii kwanini natembea na bajaji isio na stika yoyote ile? nilipigwa makofi nakuwekwa ndani siku tatu pamoja na bos wangu hio 2008.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…