Tuliowahi kupiga/kupigana au kupigwa tukumbushane hapa

Tuliowahi kupiga/kupigana au kupigwa tukumbushane hapa

Bombabomba

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2017
Posts
1,804
Reaction score
2,128
Nimekumbuka mbali sana.

1. Niliwahi kupigwa na mbabe mmoja huko kijijni kwetu tukichunga mbuzi. Yeye kazi yake ilikuwa kutuma wenzake tu hadi anaboa. Beberu wake akipigwa na wako naye anakupiga. One day nikamkatalia manyanyaso yake akaanza kunipiga, nikawaambia jamaa tupigane, jamaa wakashika mchanga sote tukapuma kukubali kupigana.

Kwa vile yeye tayari mbabe, akanijia kasi mimi nikawahi miguu nikamlalia, nikampa kichapo hadi damu puani na mdomoni. Akaomba msamaha tukaamuliwa. Then kutumana kukaisha.

2. Nikiwa darasa la pili kuna mbabe kiongozi wetu aliniaibisha mstarini kaniambia nina chawa mgongoni. (Tuliosoma 1980-90s chawa na funza ilikuwa ni kitu cha kawaida sana, hasa vijijini)

Akiwa amejisahau nilimshambulia kwa jiwe moja tu - tunayopanga mstarini hadi alilia, nikaishia kushambuliwa na wababe wengine na walimu na kuandikwa black book.

3. Nikiwa darasa la tatu, kuna mbabe wetu class nilimtania ameota nywele matakoni (mwenzetu alikuwa mkubwa kama 14-16 hivi, sisi tukiwa 11-13, hatukuwa nazo), niliziona tulipoenda oneshana vyupi VIP!

Jamaa alinipiga na kuninyanyasa daily, siku hiyo wakati ameniita ili anipe manyanyaso nikamtemea mate usoni, akijifuta nikamuunganishia ngumi mfululizo akiwa kakaaa dawatini, mimi nipo free huku nikishangiliwa hadi ticha akaja kuamua. Nikapigwa bakora assemble na kuandikwa black book mara ya 2.

Jamaa baadae aliacha shule darasa la nne tukiwa tunaheshimiana. Mwishowe hiyo black book ilipotea ofisini kwa Mkuu wa Shule. Tulishukuru kwa kuwa kilitisha sana.

4. Sekondari nilipigwa katika ubabe wa shule jirani, lakini pia kwenye kufukuzia mademu, kaka zake walinitandika hadi nikashindwa kukimbia. Demu nilimkosa japo sasa kachoka tayari.

5. Nilipigwa na polisi nikizamia uwanjani kucheki mechi ya Yanga hadi nikapoteza fahamu kwa muda; nikastukia napepewa na wasamaria.

Nafurahi kwa sasa sina adui yeyote katika maisha yangu na sipendi ugomvi kabisa. Hata home na wife tuna zaidi ya 15 yrs hatujawahi pigana.

Nawe tukumbushe kile kichapo unachokumbuka hadi sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi hata ushindi wa meno ni kupiga? Maana nilikuwa nagaragaza sana watu kwa meno kipindi nikiwa kijana.
 
We jamaa mgomvi aisee[emoji23].

Kipindi niko Shule ya Msingi Darasa la 4 niliwahi kupigana mtoto wa watu akazimia, siku 3 hajaja shule. Walimu hapo washanibutua vya kutosha na wananitisha akifa utafungwa.

Kile kihoro kilichonipata tangu siku ile sijawahi kurudia kupigana mpaka leo. Watu wakipigana sipendi, kwanza napenda kusuluhisha. Ni heri nimuombe mtu msamaha yaishe hata kama kanikosea au tuongee yaishe kuepukana na ugomvi.

Nimekua wa baridi sana kwenye masuala ya kupigana naogopa ugomvi kama ukoma. Rafiki zangu wagomvi mno wananijua tukiwa mahala wako na mimi hawaanzishi ugomvi wanajua ntasuluhisha; stakagi kujaza nzi, kurushiana machupa, kutoana ngeu, hapana kwakweli.

NB: Wazazi wangu ni wanapenda ugomvi mno, ukichokozwa huko usiwaambie wananunua bifu[emoji23], hawajui kuishi kwa amani kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikiwa Form One shule flani ya boarding, nilikuta Form Four mmoja ni mbabe wa room kwetu (room zetu zilikuwa kama hall hivi, watu kama 25).

Alikuwa na tabia ya kuonea wanafunzi, hasa wa chini yake. Alikuwa amezoea kulala kwenye vitanda vya watu bila ruhusa yao; yani ukimkuta amelala wewe tafuta pengine.

Basi bwana, siku moja mvua ilikuwa inanyesha nikarudi usiku baada ya PREPO nikamkuta kalala kitandani kwangu tena na viatu na kachafua mashuka yangu mapya. Ilibidi nimuamshe kumuuliza mbona amelala kwangu tena na viatu. Alinambia nirudi darasani. Aiseee sijui nilipata wapi nguvu na ujasiri. Ebana nilimkamata pale nikamrusha chini akaanguka kama mzigo room nzima wakaamka, tukaanza kupigana aseee, tulipigana for hrs usiku ule na hakuna aliyeamua. Naweza kusema nilimpa za nguvu mana alikuwa na damu nyingi kuliko zangu.

Toka siku hiyo nikawa mbabe mpya room ila nilikuwa sionei watu na sijawai kuonea watu. Jamaa aliniheshimu kupita kawaida na ndio ikawa mwisho wa ubabe wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We jamaa mgomvi aisee[emoji23].
Kipindi niko Shule ya Msingi Darasa la 4 niliwahi kupigana mtoto wa watu akazimia , Siku3 hajaja shule walimu hapo washanibutua vya kutosha na wananitisha akifa utafungwa. Kile kihoro kilichonipata tangu siku ile Sijawahi kurudia kupigana mpaka leo, watu wakipigana sipendi kwanza napenda kusuluhisha ni heri nimuombe mtu msamaha yaishe hata kama kanikosea au tuongee yaishe kuepukana na ugomvi. Nmekua wa baridi sana kwenye maswala ya kupigana naogopa ugomvi kama ukoma. Rafiki zangu wagomvi mno wananijua tukiwa mahala wako na mimi hawaanzishi ugomvi wanajua ntasuluhisha stakagi kujaza nzi ,kurushiana machupa,kutoana ngeu hapana kwakweli.
NB : wazazi wangu ni wanapenda ugomvi mno , ukichokozwa huko usiwaambie wananunua bifu[emoji23] hawajui kuishi kwa amani kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna kitu kizuri kama ugomvi. Unakosa mengi sana.
 
Mimi nilikuwa kunguru sana ila kuna bro wangu mmoja hivi, tupo form 1 ila ye kanizidi kama miaka 6 hivi tunatoka sehemu moja na kuna kaudugu flani kiukoo, anaitwa Himid!

Zilikuja mbavu za form 3 prefects, zina mikanda mikononi (boarding kupigwa mikanda ilikuwa ishu ya kawaida kabisa!). Bila kuuliza zikaanza kututandika just because tumechelewa kutoka dom kwenda class baada ya break ya uji saa nne!

Bro alimdindishia mmoja, akakamata mkanda na kumpokonya, akamtandika nao kichwani! Ebwana hizo ngumi zilizopigwa hapo ilikuwa hatari, mpaka double decker zinaanguka! Bro alikuwa na ubavu wa hatari, akazifletisha njemba kama nne hivi kila mmoja katoka na ngeu! From that day niliishi kwa kuvimba sana kwa sababu ya bro!

Broo akawa mbabe mpya wa shule, tena akiwa form one (njuka)! Nikukumbuka huwa nacheka sana.
 
Nimepigana sanaa...
Siku niliyopatikana ndio ikawa mwishoo.

Mazoea yalizidi nikawa napiga mpk mibabaa. Na sababu nilikuwa na jina nayo ikawa inaniogopaa.

Nikakutana na kisikiii ambacho nilishakipiga kama mara tatu hivi (alikua ana kigugumizi)

Kumbe sijampandisha hasiraa

Aloo hio siku nilipigikaa.
Nikakimbia huyo,
Nikiomba yaishe hataki,
Mpaka nikaingia kwenye karavatii jamaa kanifuata humo humo ananikanyaga.

Nilivyofanikiwa kutokea upande wa pili aloo zile mbio hazijawahi tokea kwangu.
 
Nimepigana sanaa...
Siku niliyopatikana ndio ikawa mwishoo.

Mazoea yalizidi nikawa napiga mpk mibabaa. Na sababu nilikuwa na jina nayo ikawa inaniogopaa.

Nikakutana na kisikiii ambacho nilishakipiga kama mara tatu hivi (alikua ana kigugumizi)

Kumbe sijampandisha hasiraa

Aloo hio siku nilipigikaa.
Nikakimbia huyo,
Nikiomba yaishe hataki,
Mpaka nikaingia kwenye karavatii jamaa kanifuata humo humo ananikanyaga.

Nilivyofanikiwa kutokea upande wa pili aloo zile mbio hazijawahi tokea kwangu.
[emoji23] [emoji23]
 
Binafsi nimepigana na nimepiga....

SIJAWAHI KUPIGWA NA SITAKUJA KUPIGWA

Ngoja nirudi TEMPLE kwanza japo umri umeenda
 
nikiwa darada la kwanza hadi lanne nlikua mpole na muoga sana kupigana..home ata nikipigwa siendi kusema...sasa tuko kitaa madogo tunaocheza nao na ni marafiki mmoja wao akaanzisha ubabe..akanipigaa ..nikaliiaa...baba akaskia nalia akachungulia afu akarudi...usiku akasema "yani uko mtaani ukipigwa usije kushtaki apa,ukija nakuongezea .ila ukipiga mtu ata umtoe meno kesi ntamaliza mwenyewe"

maana tulikua na mdogo wangu nae wakiume,,,..baada ya wiki baba mdogo akatua kutoka kigoma kwenye temple ya martial arts,,basi dingi akatoa amri tupikwe tuive....mamaaa pale ndo vichaa tulipewa rungu....kuanzia miaka hiyo watu walikua wanapewa vipigo vya mbwa mwizi....na kazi ya baba yeye ni kumaliza kesi tuu...baada ya kukua utukutu ukapungua..wa mwisho kumpiga alikua kibaka mwaka 2018 alikua na panga ..hahaaaaa alijuta
 
nikiwa darada la kwanza hadi lanne nlikua mpole na muoga sana kupigana..home ata nikipigwa siendi kusema...sasa tuko kitaa madogo tunaocheza nao na ni marafiki mmoja wao akaanzisha ubabe..akanipigaa ..nikaliiaa...baba akaskia nalia akachungulia afu akarudi...usiku akasema "yani uko mtaani ukipigwa usije kushtaki apa,ukija nakuongezea .ila ukipiga mtu ata umtoe meno kesi ntamaliza mwenyewe" maana tulikua na mdogo wangu nae wakiume,,,..baada ya wiki baba mdogo akatua kutoka kigoma kwenye temple ya martial arts,,basi dingi akatoa amri tupikwe tuive....mamaaa pale ndo vichaa tulipewa rungu....kuanzia miaka hiyo watu walikua wanapewa vipigo vya mbwa mwizi....na kazi ya baba yeye ni kumaliza kesi tuu...baada ya kukua utukutu ukapungua..wa mwisho kumpiga alikua kibaka mwaka 2018 alikua na panga ..hahaaaaa alijuta
Anayejua Temple inayofundisha KOMBAT MARTIAL ARTS kwa Dar msaada tafadhari, maana nimepoteza mawasiliano na Master wangu hata kwa Meditation simpati
 
Mimi nilikuwa natembea na spana ya mzee home kwenda nayo shule..

Mbona heshima ilitawala
 
Mimi nilikuwa kunguru sana ila kuna bro wangu mmoja hivi, tupo form 1 ila ye kanizidi kama miaka 6 hivi tunatoka sehemu moja na kuna kaudugu flani kiukoo, anaitwa Himid!

Zilikuja mbavu za form 3 prefects, zina mikanda mikononi (boarding kupigwa mikanda ilikuwa ishu ya kawaida kabisa!). Bila kuuliza zikaanza kututandika just because tumechelewa kutoka dom kwenda class baada ya break ya uji saa nne!

Bro alimdindishia mmoja, akakamata mkanda na kumpokonya, akamtandika nao kichwani! Ebwana hizo ngumi zilizopigwa hapo ilikuwa hatari, mpaka double decker zinaanguka! Bro alikuwa na ubavu wa hatari, akazifletisha njemba kama nne hivi kila mmoja katoka na ngeu! From that day niliishi kwa kuvimba sana kwa sababu ya bro!

Broo akawa mbabe mpya wa shule, tena akiwa form one (njuka)! Nikukumbuka huwa nacheka sana.
Dadeq

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nliwahi kufukuzwa shule kisa kumpiga mwalimu manati ya kichwani. Nlikimbia shule week mbili, ila siku nlivo report class nlitamani mungu ashushe kiama (sio kwa viboko nlivyochezea).

Ilinichukua miezi miwili kupona majeraha ya fimbo na kuweza kukaa kitako.
 
Write your reply...nimepigana sana watu mpaka nimetengua watu viungo


sahivi nimeacha ninayopigana nayo sana ni papuchi
 
Back
Top Bottom