Tuliowahi kupigwa kabari, roba ya mbao tukutane hapa

Tuliowahi kupigwa kabari, roba ya mbao tukutane hapa

Nazjaz

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2011
Posts
7,730
Reaction score
9,088
Mwaka 1998 nilipigwa roba ya mbao mchana kweupe. Ilikuwa ni Mwananyamala, nina backpack 🎒 naenda kwa Taki Mdeng'o shosti wangu kumringishia visa yangu ya USA 🇺🇸.

Safari na ndoto za kuingia nchi pendwa zikaniisha. Taking yuko Uingereza. Hadi leo
 
Pole sana aise.
1824803_IMG_20180821_190304_551.jpg
 
Kuna jamaa miaka ya nyuma alikuwa kibaka, saizi kaokoka kaachana kabisa na mambo hayo. Sasa kwakua ni mtu mwenye interest na mchezo wa draft sikumoja tukamuuliza ilikuwaje kuwaje mpaka ukaachana na ukibaka

Akatuambia kua alikuwa na crew ya vibopa wawili, nayeye jumla watatu. Jamaa ndio alikua kiongozi wa hilo gang ambapo majukumu yake yalikua ni kupiga kabali halafu wale wawili kazi yao ni kuja kusachi mifukoni

Sasa unaambiwa mchizi alikuwa ana style yake ya kupiga kabali ambayo akisha kuleta kwenye kifua chake hauchomoki, na wale vibaka wawili wanakua wanajua tu tayari pale kabali imekubali ni muda sasa wasisi kwenda kusachi

Kuna siku moja walimuona jamaa akitoka benki na kile ki-briefcase afu kaulamba suti, vibopa wawa wanamlia timing, mara yule mdingi akasimamisha daladala na wao wakajipakia humo humo

Jamaa akashuka nao wakashuka na kuanza kumfata mdogomdogo kwa nyuma kwa machale zaidi ili wasistukiwe. Basi yule faza akaiacha main road na kuingia chocho, vibaka wakasema yees

Vibaka walipoona eneo hilo halina mpishano wa watu na kuhakikisha hakuna mtu mwingine zaidi yao na yule faza wakaamua sasa kufanya mpango wa kumpora bag yule mdingi

Ikabidi sasa wale wawili wajifiche sehemu afu atangulie master mzee wa roba ili hawa wengine wakishaona roba imekubali wasogee kupora lile begi

Basi master akanyata kwa nyuma na alipomkaribia yule mdingi akapitisha mkono shingoni kilichotokea yule dingi ule mkono ambao ulipitishwa shingoni mwake na yule kibaka aliyesimama nyuma yake, mdingi akaubana ule mkono wa yule kibaka uliopita shingoni kwa kidevu, huku mkono wake mmoja ukiwa mfukoni na mmoja ukiwa umeshikilia lile bag

Hawa vibaka wawili wakawa sasa wanaskilizia roba ikubali ili wasogee, lakini kila wakiangalia mazingira wanaona mambo yamekuwa magumu kwa mwenzao, walichokua wanakishuhudia ni jitihada za mwenzao kuhangaika kutoa ule mkono uliobanwa na kidevu cha yule dingi.

Alichokifanya yule dingi akautoa ule mkono ambao aliuweka mfukoni kisha akaunyoosha juu akauzungusha kwa nyuma akakamata shati pamoja na nyama ya bega afu akamnyanyua juu akamtua mbele yake kibaka akasikika akisema "samahani braza nilikua natania" afu mdingi akamshushia kikombe cha maana wacha aagawe ile kuamka kibaka kasepa na njia

Kumbe kibaka aliingia kwenye zone ya komando
 
Kuna jamaa miaka ya nyuma alikuwa kibaka, saizi kaokoka kaachana kabisa na mambo hayo. Sasa kwakua ni mtu mwenye interest na mchezo wa draft sikumoja tukamuuliza ilikuwaje kuwaje mpaka ukaachana na ukibaka

Akatuambia kua alikuwa na crew ya vibopa wawili, nayeye jumla watatu. Jamaa ndio alikua kiongozi wa hilo gang ambapo majukumu yake yalikua ni kupiga kabali halafu wale wawili kazi yao ni kuja kusachi mifukoni

Sasa unaambiwa mchizi alikuwa ana style yake ya kupiga kabali ambayo akisha kuleta kwenye kifua chake hauchomoki, na wale vibaka wawili wanakua wanajua tu tayari pale kabali imekubali ni muda sasa wasisi kwenda kusachi

Kuna siku moja walimuona jamaa akitoka benki na kile ki-briefcase afu kaulamba suti, vibopa wawa wanamlia timing, mara yule mdingi akasimamisha daladala na wao wakajipakia humo humo

Jamaa akashuka nao wakashuka na kuanza kumfata mdogomdogo kwa nyuma kwa machale zaidi ili wasistukiwe. Basi yule faza akaiacha main road na kuingia chocho, vibaka wakasema yees

Vibaka walipoona eneo hilo halina mpishano wa watu na kuhakikisha hakuna mtu mwingine zaidi yao na yule faza wakaamua sasa kufanya mpango wa kumpora bag yule mdingi

Ikabidi sasa wale wawili wajifiche sehemu afu atangulie master mzee wa roba ili hawa wengine wakishaona roba imekubali wasogee kupora lile begi

Basi master akanyata kwa nyuma na alipomkaribia yule mdingi akapitisha mkono shingoni kilichotokea yule dingi ule mkono ambao ulipitishwa shingoni mwake na yule kibaka aliyesimama nyuma yake, mdingi akaubana ule mkono wa yule kibaka uliopita shingoni kwa kidevu, huku mkono wake mmoja ukiwa mfukoni na mmoja ukiwa umeshikilia lile bag

Hawa vibaka wawili wakawa sasa wanaskilizia roba ikubali ili wasogee, lakini kila wakiangalia mazingira wanaona mambo yamekuwa magumu kwa mwenzao, walichokua wanakishuhudia ni jitihada za mwenzao kuhangaika kutoa ule mkono uliobanwa na kidevu cha yule dingi.

Alichokifanya yule dingi akautoa ule mkono ambao aliuweka mfukoni kisha akaunyoosha juu akauzungusha kwa nyuma akakamata shati pamoja na nyama ya bega afu akamnyanyua juu akamtua mbele yake kibaka akasikika akisema "samahani braza nilikua natania" afu mdingi akamshushia kikombe cha maana wacha aagawe ile kuamka kibaka kasepa na njia

Kumbe kibaka aliingia kwenye zone ya komando
Hicho Kidevu ni cha namna gani mpaka kinaweza kuudhibiti mkono?
 
Ndani ya mwanza mida ya saa mbili usiku,nipo na kundi la marafiki zangu wengine wakiwa mbele wawili tukiwa nyuma maeneo ya mission, sisi wawili tulikuwa tukitembea huku tukiigiza mwendo wa chiko yule muigizaji wa futuhi kipindi hiko.

Katika kutembea nikajikuta nikitangulia mbele na kumuacha mwenzangu nyuma kidogo. Kumbe mwenzangu akausoma mchezo akahepa mimi tahamaki nipo katikati ya kundi la vibaka waliokuwa barabarani hapo,nikaleta ubishi nikala ngumi moja ya tumbo nikakaa sawa!. Mara bisibisi tumboni ikawekwa!

Nilitulia tuliii wakanisachi nakutoka na kitita cha shilingi mia saba yangu iliyokuwa ya sikukuu ambayo nishaisahau Kati ya mwaka mpya au Christmas 😂😂
 
Back
Top Bottom