Tuliowahi kutembea kwa sababu ya kukosa nauli tukutane hapa

Ilikuwa 2011 form 3 tulikuw na tabia ya kula naul 2nategemea lift cku iyo 2likaa kutok xhule SAA 8 kamili 2likaa kituon kihonda mbuyuni had SAA 12 no lift tulianz kuprint had mjin bahat nzur tunakaribia msamvu tulipata lift ilikuwa gar ya mrisho mpoto dah tulishukuru kumalizia nusu safari dah nkaachaga uo mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilitembea kutoka nyamagana mpaka buzuruga,sikula nauli bali sikuwa nayo jamaa niliyemuomba alinichomolea sijui alijua namtania, maana mimi ni mtu wa masihara sana.
 
Umenikumbusha mbali kidogo enzi hizo usafiri wa dar ni UDA pekee yake na ikifika mida flan ya usiku mwingi huwezi kuipata na wakati fulani hakuna route ya kwenda uendako!

Nilitoka Mwenge mpaka Temeke, Sam Nujoma rd mpaka ubungo nkakamata Mandela mpaka Veterinary nkapnda kulia mpaka Mwembe Yanga moja kwa moja mpaka Temeke Mwisho ile siku siwezi kuisahau

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kuziendekeza dhiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii itakuwa chai..tigo pesa imeanza mwaka 2010, mpesa imeanza mwaka 2009
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unasema Posta mpaka Buguruni? Tehe tehe, niulize mimi, nilipiga ngondi kutoka Tukuyu mpaka Uyole narudi nyumbani Dar es salaam kwa miguu. Jua linachomoza mpaka linazama mi niko njiani natembea sina hata hela ya kula. Nikifika Uyole usiku nikakutana na wasamalia wakanikaribisha chakula na ulabu. Sikukataa nilikula na kunywa nilivyolewa ndio ikawa nauli yangu. Nilirukia roli nikajificha kwenye magunia ya viazi wakaja kunishtukia alfajiri tushafika Mikumi, wakaona waniache tu mpaka Chalinze na hela ya kula wakanipa. We acha tu.
 
Duuh tukuyu mpaka uyole?? khaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mlimani city pale kituoni mpaka Serengeti kituo Cha gari za tandika.
2012 tulienda kulipia course ya computer na shosti wangu, tumetoka tukasema twende Mwenge. Kufika kule Hali ya hewa ikabadilika ilinyesha mvua magari hamna tukarudi Hadi itv watu kibao tukarudi Mwenge tukapanda za ubungo foleni haisogei kufika Mliman tukashuka twende kwa mguu Ubungo nako Hali mbaya, Buguruni hapatamaniki watu tumesogea gari tukapata ya tandika Mwenzangu alikua anaishia temeke mie mpaka mbagala ndani ndani. Toka saa 11jion nimefika saa Saba kasoro usiku. Mshua akaniseeema nimetoka kwa wanaume na chakula nikanyimwa, Kesho muguu imetoa Kama malenge lenge unyayoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2014 Niliibiwa bag dogo mchana kweupe soko la mitumba Krokon Arusha, kila kitu kilikuwa humo wallet na simu, nilitembea kwa mguu kutoka hapo Krokon mpaka Tengeru mdogo mdogo nilipokuwa ndo nakaa! Aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mi nshapiga tokea Krokon mpaka Tengeru, nilifika kule nikaumwa na kesho sikutoka miguu imevimba mzee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…