Tuliowahi kutembea kwa sababu ya kukosa nauli tukutane hapa

Na nyingine ambayo nayo sitasahau ni kipindi nasoma Itaga Seminary, iko Tabora mbali sana na mji! Tulipigwa suspension na washkaji zangu kadhaa miaka hiyo, na taarifa zilikuwa zinakwenda Jimboni mjini, wazazi wanapewa taarifa wanakuwa wanawasubiri hapo jimboni mletwe toka huko shule wakabidhiwe, sasa mzee wangu mimi alivyokuwa bandidu akaongea na Padri ambaye kesho yake ndo angetupeleka hapo jimboni kuwa aniache njiani kama adhabu, dah lile padri bhana kesho yake tumepanda 'MIVA' nashangaa ananichomoa peke yangu hapo ananambia baba yako amesema utembee mpaka mjini na utamkuta yeye anakusubiri...daah sikuamini kabisa ila jamaa akachochea ndinga na mabegi yangu na masela zangu huko ndani wakasepa! Aisee nilitembea siku ile sitasahau, na nilimchukia sana mzee wangu, na njia ile ilikuwa hatari sana miaka hiyo haina magari wala wanavijiji wengi njiani, nimetembea kama masaa mawili nakutana na jamaa ana baiskeli na mkaa, akanipandisha nyuma juu ya mkaa, napo nikawa mzigo tena kwake maana njia ina mchanga kiasi akanishusha kama baada ya kilomita moja tu hivi, nikatembea tena kidogo nikaona yule padri ameamua kuja kunifuata tu! Tunafika jimboni nako dingi hayuko kawaambia ashasikiliza kesi yangu yeye kasepa na mabegi niende home kwa mguu, kwa wanaoelewa kutoka Tabora mjini mpaka maeneo ya Cheyo A maanina! Nakumbuka pia na mama aligombana sana na mzee ile nimefika home! Kwa adhabu ile Nilikoma utundu na ujinga shule! Nilikuja mshukuru mzee baada ya matokeo ya form two kutoka mwaka huo huo! Maana kwa utundu ule nisingetoboa hakika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Reactions: Cyb
Unanunua bando unaingia jf unapost alafu unasema huna nauli ?

Unataka huruma za watu ama ? Kwa maneno mengine umeomba hela indirect, pambana mkuu , khs kutembea Ni mazoezi

Sent using Jamii Forums mobile app
HUJAELEWA ANACHOTAKA KUTUSHIRIKISHA HAPA....SOMA VIZURI POST USIKURUPUKE!! NYINYI NDIYO MLIKUWA MNAFELI MITIHANI KWA KUTOKUSOMA VIZURI MASWALI!!!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Alikunyoosha aisee...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wazee wakatili ha ha ha ha ha
 
Mimi sikuwai kutembea umbali mrefu sema kipindi niko chuo nilikua nimepanga geto kinondoni sasa nikawa nna tabia ya kuja SANAA hapa palipo na makao makuu ya bank ya NMB posta hapa mitaa ya serena palikua na bar inabamba sana enzi hizo sasa nikala vyombo hadi nikabakiwa na elfu tano ukicheki kadi za ATM nimeziacha geto nilikua nahofia kutembea nazo ntazipoteza basi ile elfu tano kwenda kuwaomba jamaa wa text wanipeleke geto wakagoma enzi hizo bajaj au bodaboda hamna mwaka 2008. Basi nikaenda kutulia zangu pale LAS VEGAS kasino nasubili pakuche nipande daladala aisee usiku nilipigwa na baridi balaaa na usingizi kibao na wale malaya pale mara wapigane yani kero tupu tangu ziku iyo niliapa sitafanya ujinga ule.Ilikua ndio first time kukesha usiku kwenye baridi kama vile aisee madereva texi wa usiku wanatafuta hela kwa nguvu sana alafu wao wako confortable wanakula fegi tu
 
Acha utani Posta-buguruni karibu mno haikutakiwa hata kuanzisha uzi,

Mimi nilitembea toka posta mpaka chamanzi kwa mapunda, kuna dada mmoja msenge ndo aliesababisha.
Hela nlikuanayo 2000 yule dada ana renew chip maana nlipoteza chip kuna hela mule nlikua naitaka(kumbe line ukii renew huwezi kutumia huduma za kifeza mpaka masaa sijui mangapi yapite mi nilikua sijui, maana alinmbia ntaitumia line muda uleule hela ya nauli nikaitumia ku renew mbona nilijuta)
nikafika mbagala hoi nilikua nna mkeka nikaenda meridian kuumulika timu zote zimechana ikabidi nimalizie safari.
Watumwa na wenyewe walikua wasenge sasa sijui waliwezaje kutembea kutoka dar mpaka Congo?
 
Nakumbuka nilitembea Km 16 aiseee... [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Toka Kambini Jeshini Mgambo mpala Kabukuu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mwaka juzi nilienda kariakooo kutengeneza simu ikamaliza ela yote na simu haikutengeneza na sikua na msaada wowote..nikawa sina namna nikapiga amza kanuni kutoka kariakoo mpka kimara ni mwendo wa masaa mtatu nilitoka saa kumi nikafika saa moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nilitembea kutoka kkoo hadi Gongo la Mboto kisa GEROGE BUSH foleni zimebana balaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watumwa walikua wanatishwa ukuu mwenzako anapigwa risasi pembeni hapo akizingua we unazani unaweza kuleta fyoko
 
Kipindi niko field MUHAS ...Muhimbili hospital mpaka ubungo nikapanda daladala mpaka kimara..ningemalizia tuu sema giza lilikuwa limeingia na kesho natakiwa kazin..

Sent using Jamii Forums mobile app
ulikua na upungufu wa nauli ama uliamua tu kufanya zoezi mkuu?maana kama ulitembea mpk Ubungo afu ukapanda gari tena😛 . by then kulikua na daladala za Muhimbili - Mbezi, si ungepanda hizo tu
 
Nishawa kupoteza naulii kipindi hich niko arusha nilitoka sanawari hadi ngaramtoniii duu sitasahauuuuu nanyoosha barabara kama mwendawazimu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…