Tuliowahi kuwa "madomo zege" tujuane hapa

Nikiwa nasoma Azania Sec school miaka hyo.

ilikuwa kuna sehem tunakaa kwa ndani baina ya Azania sec na jangwani sec kama maskani baada ya masomo..

Eneo hilo warembo wa jangwani sec walikuwa hawakauki kukatiza hapo mara kwa mara.

Kipindi hicho ndy balehe imepamba Moto,

Na najifunza kutongoza,

- lakini domo zege,,
-Ulimi kilo 50 uzito..
-Udenda jagi zima..
Domo zege.

Siku hiyo alipita mtoto mmoja mkali Sana wa jangwani sec,,
Mtoto kapiga skirt Safi na soksi nyeupe Safi
Anawaka hatari.
Kipindi hicho dent wa secondary ni mrembo kweli.
Amekamilika kila idara.
Na kipindi hicho jangwani sec ndy shule ya sec iliyokuwa inaongoza kwa watoto wakali .

Kwa kujitutumua nikamuita yule mrembo denti.

"Dada samahani kidogo."
Nilipayuka kwa sauti mbele ya jamaa zngu.

Bila kutegemea yule denti alisimama pale pale.,

"Akasema nakusikiliza"

Dah!!
Nikaanza kulazimisha mrembo aje pale tulipo na washikaji wengine.
.
Yule denti akaja hadi pale nilipo,
Huku akionyesha kunishangaa Sana..

Basi jinsi yule denti alivyokuwa mrembo.
Na alipokuja pale kunifata Mimi,

Watu wote walihamishia macho kwangu na denti kujuwa Mimi nitaongea nn?

Dent..uliniita?
Unasemaje?

Mimi; dah nahisi nimekufananisha sorry [emoji2][emoji2][emoji2]..

Denti:: uliniona wapi!?

Mimi;sorry nimekufananisha nitakukumbusha kesho nikikuona[emoji2][emoji2][emoji2].

Demu akabaki na mshangao.
Akaondoka zake.

Basi huku nyuma jamaa wanavunjika mbavu kwa kucheka.
. mwishowe kijiwe nikakiona kichungu.

Domo zege ni zaidi ya ufala [emoji2][emoji2][emoji2].
Sikutegemea kama yule mrembo angekuja pale kunifata Mimi.

Sent from my M2101K7BG using JamiiForums mobile app
 
ila mara nyingi ukimpenda manzi kwa dhati basi mara nyingi unakuwa domo zege kwake.
 
Poleni sana wakulungwa kwa kadhia hizo za udomo zege.
 
Hahaha
 
nlimkula enzi hizo tukapotezana after skuli then tukaja kukutana miaka mingi baadae kwe michongo ya maisha akawa muhimu sana aisee kiasi siwez andika equation ya maisha yangu bila yeye
Hongera
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…