Tough lady
Senior Member
- Jul 24, 2013
- 151
- 183
Naandika habari hii ili kuwasaidia hata wadogo zetu na ndugu zetu wajue uozo uliopo Tumaini University Dar es salaam,ni chuo ambacho kwanza mazingira yake hayafai kuitwa chuo kikuu, mtu ajaribu kwenda Mwenge barabara ya Coca cola ajionee mazingira tunayosomea, lecture rooms ni jengo la mabati limetengwa kwa ceiling boards, computer room ina computer ila zinazofanya kazi si zaidi ya computer 10, mnaweza kukaa semester ikafika nusu bila lecturer, wakimpata anafundisha miezi 2 halafu mnaambiwa semester tayari kwa somo hilo, hii imewapata sana watu wa education mfano katika course ya Geography na Educational media and technology.Unaweza kuamini haya mambo yanatokea katika chuo ambacho ada yake ni shilingi 2,500,000 kwa mwaka?, miaka 3 ada ya Tumaini dsm ni shilingi 7,500,000.Hayo ni baadhi ya kero za Tumaini university Dsmkwa ufupi.<br>Tatizo sugu zaidi lililonituma kuandika leo hii ni tatizo la hela ya mkopo toka HESLB.Kama unasoma Tumaini kwa kutegemea hela ya mkopo unakuwa umekwisha, hela ya mkopo Tumaini huwa inatoka wiki 2 hadi 3 baada ya vyuo vingine kupokea hela hizo, tatizo zaidi ni hela za field. Mwaka jana wanafunzi wa education walilipwa shilingi 480,000 badala ya 620,000, kwa maelezo kuwa eti hawakuwa kwenye bajeti ya bodi kwani uongozi haukuonyesha kama kuna field wakati huo, na hizo hela zilipatikana baada ya vikao vingi sana na loan officer wa kipindi hicho...<br>Sasa, mwaka huu, mpaka sasa hivi, wanafunzi wote wa Tumaini university Dsm, hatujapata hela ya field, na wakati huo field imeanza tangu tarehe 15 july.Wakati tunafunga, tuliambiwa kuwa hela haijaja toka loan board hivo tukapewa karatasi yenye majina tukajaza namba za account ili hela itakapofika toka loan board watuingizie hela kwa kuhakiki account zetu kupitia karatasi tuliyosaini.Cha ajabu, jumatatu iliyopita, tukatumiwa ujumbe kuwa watu tuliopo Dsm tufike chuoni kwa ajili ya kusaini na kuhakiki namba za akaunti kwenye hela ya field, walioweza wakafika wakasaini, cha ajabu, mpaka leo hii, hakuna hela ya field iliyoingia, na je kwa waliopo mkoani, chuo kinafikiria wataishi vipi na wako field?, na kwanini tusipewe hela zetu kwa kuwa tulishaacha akaunti namba wakati wa kuondoka chuo?,hivi sasa kila mtu anasema la kwake, hatuna wa kumuuliza maana hata serikali ya wanafunzi haijulikani kama ipo au haipo, ulifanyika uchaguzi wa serikali, ukapingwa na mgombea aliyeshindwa, kuanzia hapo hatuelewi kinachoendelea.Naandika hivi kwa niaba ya wanafunzi wenzangu, tunaumia sana, naomba wanasiasa na viongozi wa dini waingilie kati, hiki chuo wanadai ni cha dini, lakini wanafunzi tunanyanyaswa tofauti na dini inavotaka watu watende,..kuna mengi sana hapo chuoni, nategemea pia kuanzisha page facebook itakayoeleza uozo wote wa Tumaini, na hiyo page itasaidia wanafunzi wengi kutoa dukuduku lao,nitapost jina la page pindi niianzishapo.<br>Ni hayo tu kwa leo, naomba jamii itusaidie wanafunzi wa Tumaini, na nawaasa ndugu zangu, ukiamua kujiunga Tumaini Dsm, ujitayarishe kuwa na roho yenye kusononeka kwa miaka yote utakayosoma hapo.