"Tume Huru" Maana Yake ni Nini?

"Tume Huru" Maana Yake ni Nini?

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Leo nimesome sehemu kuwa wabunge wamepinga ripoti ya mto Mara wanataka iundwe "tume huru." Kila mara tumekuwa tunasikia watu wakilalamika kuwa inatakiwa tume huru ya uchaguzi. Ninavyoelewa, tume kikundi cha watu walioteuliwa kufanya shughuli fulani kulingana na hadidu za rejea wanazopewa na chombo kinachowateua. Sasa ninaposikia watu wakisema tume huru, huwa nashindwa kuelewa kwani tume yoyote huunda na chombo fulani na wanapewa hadidu za rejea, kwa hiyo uhuru walionao unabanwa na hadidu za rejea.

Je tunataka tume ambayo inajiandikia hadidu zake za rejea?

Inawezekana sana kuwa watu tunatumia neno "tume huru" kiurahisi tu lakini kwa makosa.

Mafundi wa kiswahili nawapa mada hapaya kuijadili, jeTume Huru ikoje?
 
Leo nimesome sehemu kuwa wabunge wamepinga ripoti ya mto Mara wanataka iundwe "tume huru." Kila mara tumekuwa tunsikia watu wakilalamika kuwa inatakiwa tume hurur ya uchaguzi. Ninavyoelewa, tume kikundi cha watu walioteuliwa kufanya shughuli fulani kulingana na hadidu za rejea wanazopewa na chombo kinachowateua. Sasa ninaposikia watu wakisema tume huru, huwa nashindwa kuelewa kwani tume yoyote huunda na chombo fulani na wanapewa hadidu za rejea, kwa hiyo uhuru walionao unabanwa na hadidu za rejea. Je tunataka tume ambayo inajiandikia hadidu zake za rejea?

Inawezekana sana kuwa watu tunatumia neno "tume huru" kiurahisi tu lakini kwa makosa.

Mafundi wa kiswahili nawapa mada hapaya kuijadili, jeTume Huru ikoje?
Labda pengine isiyofungamana na upande wowote wa kimamlaka, kisiasa,kichama au pengine watu kutoka nje wasio na mgongano wa kimaslahi upande huu na huu
 
Labda pengine isiyofungamana na uapnde wowote wa kimamlaka, kisiasa,kichama au pengine watu kutoka nje wasio na mgongano wa kimaslahi upande huu na huu
Henda, lakini sidhani kama kweli kuna mtanzania atakayekubalika kuwa hajafungamana na upande wowote. Mara nyingi watanzania tumekuwa na tabia ya kumpima hakimu kwa kulingana na hukumu anayotoa. Ikiwa hukumu haitufrahishi, tunesema amefungamana na serikali, na anapotoa hukuma inayopingana na serikali tunafurahi hata kama hakimu mweneywe ni yule yule.
 
Henda, lakini sidhani kama kweli kuna mtanzania atakayekubalika kuwa hajafungamana na upande wowote. Mara nyingi watanzania tumekuwa na tabia ya kumpima hakimu kwa kulingana na hukumu anayotoa. Ikiwa hukumu haitufrahishi, tunesema amefungamana na serikali, na anapotoa hukuma inayopingana na serikali tunafurahi hata kama hakimu mweneywe ni yule yule.
Na ndio changamoto inapokuja hapo sasa
 
Back
Top Bottom