Uchaguzi 2020 Tume Huru ya uchaguzi au Uwazi katika mchakato wa uchaguzi

Uchaguzi 2020 Tume Huru ya uchaguzi au Uwazi katika mchakato wa uchaguzi

EZZ CHEZZ

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
1,230
Reaction score
1,352
Hello JF,

Kwanza ni-declare interest: Mimi ni muumini wa kile kinachowezekana hata kama hakifurahishi kuliko kile kinachofurahisha lakini hakiwezekani.

Kutokana na muundo wa tume huru unavyopaswa kuwa, nachelea kuamini kuwa kuna siku chama tawala kitakuja ridhia ipatikane! Muundo wake kwa vyovyote vile utakuwa kiama kwa chama kinachotawala sasa.

Mf. Ikiwa kila chama kitakuwa na mjumbe mmoja kwenye "bodi", upinzani utakuwa na " wajumbe" wengi kuliko chama tawala ambacho kitashindwa kuipelekesha tume kwa maslahi yake. Sidhani kuwa kuna siku watakubali hilo litokee.

Bali "uwazi katika mchakato wa uchaguzi" ndiyo kitu kinaweza piganiwa na kupatikana kwa kuzingatia mazingira ya demokrasia finyu tuliyopo. Hivyo basi napendekeza vyama vikuu vya upinzani kushinikiza mabadiliko ya sheria ya uchaguzi ili kuwe na transparency wakati wote wa zoezi hilo.

Hiki kitu kiliwezekana "kiasi fulani" mwaka 2010. Baada ya serikali kununua "super computer" kwa ajili ya "kukusanya na kuhesabu" kura, iliviita vyama vyote shiriki kuukagua "siku mbili kabla". Mtambo ulibainika kuwa na " kasoro" kwenye ujumuishi wa matokeo, (hii kasoro ilikuja kumgharimu mgombea wa chadema kwa kura zake kugawanyika kwenda kwa wagombea wengine: Lipumba alipata kura ambazo hakupigiwa). Hii ni kwa mujibu wa gazeti la MwanaHalisi.

Kwa wakati ule niliwalaumu chadema (wapinzani halisi kwa wakati ule). Kwani baada ya kila chama kupeleka "IT" wawili kikagua mtambo na kubaini una shida, ni mtu mmoja pekee aliyepigia kelele suala hilo; mgombea wao Slaa, ambaye alipotoa kauli siku mbili kabla ya uchaguzi kuwa ccm wamevuruga uchaguzi, hivyo ufutwe na mchakato uanze upya alionekana hayawani.

Viongozi wa chams walikuwa bize kupigania ubunge kwenye majimbo yao na kumwacha solemba akilia na NEC.

Lengo la huu mfano ni kuonesha kuwa kinachowezakana (kwenye mazingira tuliyopo ya demokrasia hafifu) ni kuisukuma serikali ikubali mchakato wa uchaguzi uwe wa wazi. Ingawa najua kwa wafuasi wa "tume huru" hili halivutii.

Bali tume huru haiwezi kupatikana abadani (rejea kauli ya hivi karibuni ya katibu mkuu wa chama tawala). Sasa ni afadhali kupata kidogo kinachowezekana na kuangalia namna kinavyoweza kutumika kuleta mabadiliko kuliko kusubiria kikubwa ambacho hakitawahi kuja.

Tujadili.
 
Kwahiyo viongozi wetu wa upinzani ambao ndio tunawategemea kwa mawazo mbadala ni kwamba hawako sahihi katika hili la kudai tume huru? Ni kwamba hawajui kuwa haliwezekani au wanajua ila wanatupumbaza tu?
 
Tume huru ya uchaguzi itakuwa na Uwazi katika mchakato wa uchaguzi mathalan matokeo ya kura za Urais yatabandikwa vituoni wananchi wataweza kujumlisha wenyewe na kujiridhisha.
 
Kwanza ni-declare interest: Mimi ni muumini wa kile kinachowezekana hata kama hakifurahishi kuliko kile kinachofurahisha lakini hakiwezekani.

Bali "uwazi katika mchakato wa uchaguzi" ndiyo kitu kinaweza piganiwa na kupatikana kwa kuzingatia mazingira ya demokrasia finyu tuliyopo. Hivyo basi napendekeza vyama vikuu vya upinzani kushinikiza mabadiliko ya sheria ya uchaguzi ili kuwe na transparency wakati wote wa zoezi hilo.

kinachowezakana (kwenye mazingira tuliyopo ya demokrasia hafifu) ni kuisukuma serikali ikubali mchakato wa uchaguzi uwe wa wazi. Ingawa najua kwa wafuasi wa "tume huru" hili halivutii.

Bali tume huru haiwezi kupatikana abadani (rejea kauli ya hivi karibuni ya katibu mkuu wa chama tawala). Sasa ni afadhali kupata kidogo kinachowezekana na kuangalia namna kinavyoweza kutumika kuleta mabadiliko kuliko kusubiria kikubwa ambacho hakitawahi kuja.

Tujadili.
Mkuu Izo Chezi, this is very objective, tunapoelekea kwenye uchaguzi Mkuu, watu kama nyinyi ambao ni wakweli na very objective ndio mnalisaidia taifa kwa kuueleza ukweli mchungu.

Kwa muda huu tuliobakiwa nao, ukweli ni bora kufanya kile kidogo kinachowezekana kuliko kutaka kikubwa ambacho hakiwezekani.

Kwenye uchaguzi, usawa wa haki na transparency kwenye kupiga kura ndio kila kitu.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda NEC, inaeleza wazi kuwa NEC ni independent institution, lakini kwa vile uteuzi wa viongozi wote wa NEC kuanzia Mwenyekiti, Mkurungenzi wa Uchaguzi, Makamishna, Wasimamizi wote wa uchaguzi unafanywa na mtu mmoja ambaye na yeye ni mgombea wa chama kimoja, it's expected watalipa fadhila, na mteuzi atateua makada wa chama chake, hivyo the only way ya kupata uchaguzi huru na wa haki ni kupitia maximum transparency.

Kwavile kura zinapigwa vituoni na kuhesabiwa vituoni, na matokeo yote kubandikwa vituoni, then kupitia maendeleo ya kitechnolojia, mawakala wa vyama vyote wawe na smart phones ambazo wata scan matokeo na kutuma makao makuu ya kata zao, majimbo yao na makao makuu ya vyama vyao.

Kila chama kiruhusiwe kufanya independent tallying, kwa kutumia scanned copies za vituoni, sio kwa lengo la kutangaza matokeo bali for tracking and prooving hivyo matokeo ya udiwani ya NEC, lazima ya tally na matokeo yenu, yasipo tally you have a proof.

The same ifanyike kwenye ubunge hadi urais.
P
 
Ni wazo zuri lakIni ili tuongeze uwazi inabidi turuke viunzi viwili muhimu ambavyo ndo vikwazo vya demokrasia nchini.

1. Jeshi la polisi: Lazima tuminimize militarization of the electoral process, hii ikiwa ni pamoja na kuwakataza polisi kuzunguka na magari ya washawasha na ving'ora kabla ya uchaguzi. Watu hawajawahi kufikiria juu ya haili lakini matendo haya huwa yanasababisha watu wasiende kupiga kura kwa kuwa wanaona zoezi lenyewe ni hatari kumbe linatakiwa liwe ni jambo la kawaida la kumpata kiongozi.

2. Wakurugenzi wa halmashauri: Wakurugenzi wa halmashauri ambao ni wateule wa rais aliyeko madarakani wasisimamie uchaguzi hata kidogo. Kiwepo chombo kingine ambacho kitaaminiwa na vyama vyote, hii itaongeza uwazi na kupunguza vurugu katika chaguzi zetu. Haiingii akilini kwamba mteule wa rais akavitendea haki vyama vingine hata kama ameapa kutenda haki. Mara nyingi wakurugenzi huwa hata kama wanataka kutenda haki huwa wanapewa mashinikizo na wakuu wa wilaya na mikoa ambao mara nyingi ni makada wa CCM.
 
Binafsi naona hata ikipatikana hakuna jipya kwa upinzani huu ,Kwan CCM wana mapandikizi wengi sana kwenye hvi vyama vya upinzani mfano sasa hvi wapo wanaodai na wengine hawana hata mpango na wengine waliitwa huko magogoni Sijui wamepewa maagizo gani.Lakn Hawa wote ni waponzani na wanaonekana hawana umoja kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usitegemee uwazi wowote bila kuwa na Tume huru....

Tume huru si option tena brasa kaka!! Ni lazima ili kulinda maamizi ya wengi kupitia sanduku la kura kuheshimiwa.

Kwa CCM huu ni msumari katikati ya utosi...hawana namna!!
 
Hello JF,

Kwanza ni-declare interest: Mimi ni muumini wa kile kinachowezekana hata kama hakifurahishi kuliko kile kinachofurahisha lakini hakiwezekani.

Kutokana na muundo wa tume huru unavyopaswa kuwa, nachelea kuamini kuwa kuna siku chama tawala kitakuja ridhia ipatikane! Muundo wake kwa vyovyote vile utakuwa kiama kwa chama kinachotawala sasa.

Mf. Ikiwa kila chama kitakuwa na mjumbe mmoja kwenye "bodi", upinzani utakuwa na " wajumbe" wengi kuliko chama tawala ambacho kitashindwa kuipelekesha tume kwa maslahi yake. Sidhani kuwa kuna siku watakubali hilo litokee.

Bali "uwazi katika mchakato wa uchaguzi" ndiyo kitu kinaweza piganiwa na kupatikana kwa kuzingatia mazingira ya demokrasia finyu tuliyopo. Hivyo basi napendekeza vyama vikuu vya upinzani kushinikiza mabadiliko ya sheria ya uchaguzi ili kuwe na transparency wakati wote wa zoezi hilo.

Hiki kitu kiliwezekana "kiasi fulani" mwaka 2010. Baada ya serikali kununua "super computer" kwa ajili ya "kukusanya na kuhesabu" kura, iliviita vyama vyote shiriki kuukagua "siku mbili kabla". Mtambo ulibainika kuwa na " kasoro" kwenye ujumuishi wa matokeo, (hii kasoro ilikuja kumgharimu mgombea wa chadema kwa kura zake kugawanyika kwenda kwa wagombea wengine: Lipumba alipata kura ambazo hakupigiwa). Hii ni kwa mujibu wa gazeti la MwanaHalisi.

Kwa wakati ule niliwalaumu chadema (wapinzani halisi kwa wakati ule). Kwani baada ya kila chama kupeleka "IT" wawili kikagua mtambo na kubaini una shida, ni mtu mmoja pekee aliyepigia kelele suala hilo; mgombea wao Slaa, ambaye alipotoa kauli siku mbili kabla ya uchaguzi kuwa ccm wamevuruga uchaguzi, hivyo ufutwe na mchakato uanze upya alionekana hayawani.

Viongozi wa chams walikuwa bize kupigania ubunge kwenye majimbo yao na kumwacha solemba akilia na NEC.

Lengo la huu mfano ni kuonesha kuwa kinachowezakana (kwenye mazingira tuliyopo ya demokrasia hafifu) ni kuisukuma serikali ikubali mchakato wa uchaguzi uwe wa wazi. Ingawa najua kwa wafuasi wa "tume huru" hili halivutii.

Bali tume huru haiwezi kupatikana abadani (rejea kauli ya hivi karibuni ya katibu mkuu wa chama tawala). Sasa ni afadhali kupata kidogo kinachowezekana na kuangalia namna kinavyoweza kutumika kuleta mabadiliko kuliko kusubiria kikubwa ambacho hakitawahi kuja.

Tujadili.
ili kuwepo uwazi kwenye uchaguzi, nilazima pawe na combo huru chausimamizi (tume huru) kimuundo na kiutendaji. Na hii tume isiwe kwa ajili ya vyama vya siasa Bali kwa ajili ya wananchi maana ndio wa naotaka kuona kura zao ziaheshimiwa na kuthaminiwa.
 
Kwahiyo viongozi wetu wa upinzani ambao ndio tunawategemea kwa mawazo mbadala ni kwamba hawako sahihi katika hili la kudai tume huru? Ni kwamba hawajui kuwa haliwezekani au wanajua ila wanatupumbaza tu?
Hakuna aliyesema hawako sahihi katika kudai tume huru. Ni maoni tu na mtazamo kuwa suala.la tume huru haliwezekani kwa sasa achilia mbali utata juu ya upatikanaji wake!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Angalizo tu, tume huru isiwe na wawakilishi wa vyama vya siasa CCM inauwezo kumiliki 90% ya vyama. Kwanza tuna hitaji tuwe na katiba bora, tuwe na mifumo na taasis huru.

Sent using Jamii Forums mobile app
Well said. Huo ni miongoni mwa utata wa tume huru. Mjumbe kama Mrema, je atakuwa mwakilishi wa chama chake au mwakilishi wa ccm?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tume huru ya uchaguzi itakuwa na Uwazi katika mchakato wa uchaguzi mathalan matokeo ya kura za Urais yatabandikwa vituoni wananchi wataweza kujumlisha wenyewe na kujiridhisha.
Tatizo ni kuwa chama tawala hiki hakiwezi kuangalia serikali iliyo chini yake itupatie tume huru. Rejea kauli ya Dr. Bashiru.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Izo Chezi, this is very objective, tunapoelekea kwenye uchaguzi Mkuu, watu kama nyinyi ambao ni wakweli na very objective ndio mnalisaidia taifa kwa kuueleza ukweli mchungu.

Kwa muda huu tuliobakiwa nao, ukweli ni bora kufanya kile kidogo kinachowezekana kuliko kutaka kikubwa ambacho hakiwezekani.

Kwenye uchaguzi, usawa wa haki na transparency kwenye kupiga kura ndio kila kitu.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda NEC, inaeleza wazi kuwa NEC ni independent institution, lakini kwa vile uteuzi wa viongozi wote wa NEC kuanzia Mwenyekiti, Mkurungenzi wa Uchaguzi, Makamishna, Wasimamizi wote wa uchaguzi unafanywa na mtu mmoja ambaye na yeye ni mgombea wa chama kimoja, it's expected watalipa fadhila, na mteuzi atateua makada wa chama chake, hivyo the only way ya kupata uchaguzi huru na wa haki ni kupitia maximum transparency.

Kwavile kura zinapigwa vituoni na kuhesabiwa vituoni, na matokeo yote kubandikwa vituoni, then kupitia maendeleo ya kitechnolojia, mawakala wa vyama vyote wawe na smart phones ambazo wata scan matokeo na kutuma makao makuu ya kata zao, majimbo yao na makao makuu ya vyama vyao.

Kila chama kiruhusiwe kufanya independent tallying, kwa kutumia scanned copies za vituoni, sio kwa lengo la kutangaza matokeo bali for tracking and prooving hivyo matokeo ya udiwani ya NEC, lazima ya tally na matokeo yenu, yasipo tally you have a proof.

The same ifanyike kwenye ubunge hadi urais.
P
Yap, hii ndiyo kitu inaweza kutupatia viongozi tutakaowachagua. Ingawa vyama vyetu vya upinzani navyo vina udhaifu mkubwa sana kwenye kujumuisha matokeo yao. Chadema kwa mfano, 2010 hawakuwa na matokeo kabisa wakitarajia wema wa serikali/ccm. Kuja 2015 wakawa na "laptops za kujumlishia matokeo!"

Kwenye ulimwengu huu wa kisasa na wa kutafutana, ya nini kujumlisha matokeo "manually kwa excel" ilhali unaweza kuyapata papo hapo kwa kutumia "applications ikiwamo excel hiyo hiyo?".

Chama kinaweza kuandaa app ambayo kila wakala/kata wata-upload matokeo yao pamoja na evidence za kuya-support (scanned images za fomu za matokeo) na application ikawa na live/up-to-date scores kama kwa wenzetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama siyo tishio la mabeberu wa Zito na aki na Pompeo uchaguzi huu tungeambiwa tukae mita 200 na Mkurugenzi ndo atajumlisha kura ofisini kwake.
Ila sanduku likiwekwa kati kura zikahesabiwa kweupe Kuna rangi fulani haitaonekana.
 
Kama siyo tishio la mabeberu wa Zito na aki na Pompeo uchaguzi huu tungeambiwa tukae mita 200 na Mkurugenzi ndo atajumlisha kura ofisini kwake.
Ila sanduku likiwekwa kati kura zikahesabiwa kweupe Kuna rangi fulani haitaonekana.
Miaka yote tumekuwa tukilalamika wizi wa kura unaofanywa na ccm,hao mabeberu walikuwa hawatusikii au?
 
Ni wazo zuri lakIni ili tuongeze uwazi inabidi turuke viunzi viwili muhimu ambavyo ndo vikwazo vya demokrasia nchini.

1. Jeshi la polisi: Lazima tuminimize militarization of the electoral process, hii ikiwa ni pamoja na kuwakataza polisi kuzunguka na magari ya washawasha na ving'ora kabla ya uchaguzi. Watu hawajawahi kufikiria juu ya haili lakini matendo haya huwa yanasababisha watu wasiende kupiga kura kwa kuwa wanaona zoezi lenyewe ni hatari kumbe linatakiwa liwe ni jambo la kawaida la kumpata kiongozi.

2. Wakurugenzi wa halmashauri: Wakurugenzi wa halmashauri ambao ni wateule wa rais aliyeko madarakani wasisimamie uchaguzi hata kidogo. Kiwepo chombo kingine ambacho kitaaminiwa na vyama vyote, hii itaongeza uwazi na kupunguza vurugu katika chaguzi zetu. Haiingii akilini kwamba mteule wa rais akavitendea haki vyama vingine hata kama ameapa kutenda haki. Mara nyingi wakurugenzi huwa hata kama wanataka kutenda haki huwa wanapewa mashinikizo na wakuu wa wilaya na mikoa ambao mara nyingi ni makada wa CCM.
Yeah hivi ni vihunzi hasa. Ijapokuwa sina tumaini ikiwa vinaweza epukika before 2020".

Tatizo kubwa la jeshi letu la Polisi ni muundo wake ambao unakinzana na msingi wa uwepo wake. Polisi wanapaswa kuwepo kwa ajili ya usalama wa raia na si kudhibiti raia kama ilivyo kwetu.

Pia tatizo kubwa la hawa wakurugenzi.ni namna wanavyopatikana. Hawa kimsingi wangepaswa kuwa wateule wa mkuu wa wilaya ambaye "amechaguliwa na wananchi" na si kuteuliwa na "mwenyekiti" wa chama tawala kama ilivyo sasa.

Hivyo basi, ninadhani vihunzi hivi vyote viwili vingetatuliwa kwa kubadili mfumo wa TAMISEMI ambapo viongozi wakuu wa wilaya/mkoa wachaguliwe na wananchi. Kila wilaya/mkoa uwe na "idara yake" ya jeshi la polisi (kama marekani). Mkuu wa wilaya/mkoa (governor?) ndiye ateue mkuu wa polisi.

Au,

Ikiwa hatuwezi kufumua muundo wetu wa TAMISEMI basi angalau Polisi iwe chombo huru ambacho ma-commissioner wake hawatateuliwa bali kugombea nafasi zao na kufanyiwa vetting na tume ya utumishi. Rejea namna Jaji mkuu wa Kenya anavyopatikana.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yanayowezekana kufanyika sasa kwa muda uliobaki
1. Mabadiriko ya sheria matokeo ya uchaguzi wa Urais yahojiwe mahakamani kama kuna dosari kubwa zilizo jitokeza
2. Utaratibu wa kila chama kuhesabu / kujumulisha matokeo ya mgombea nafasi ya Rais uruhusiwe
3. Mgombea huru aruhusiwe . Nadhani hili lilishapitishwa na Mahakama!?

Mipango ya muda mrefu; Maandalizi yaanze sasa
1. Mabadriko ya sheria husika; za tume ya uchaguzi, vyama vya siasa, katiba, utumishi wa umma (serikali za mitaa) na nyinginezo ili kuruhusu yafutayo;
2. NEC - tume ya uchaguzi isiwe chini ya Serikali ijiendeshe yenyewe
3. NEC ijitegemee kibajeti - utaratibu huru ufanyike kubaini vyanzo vyake vya fedha
4. Viongozi wa Tume wasiteuliwe na Rais. Waajiliwe kwa utaratibu mazi na usiotegemea muhimili mwingine
5. Iwapo viongozi watateuliwa na Rais basi utaratibu na kinga kwa watumishi ya NEC uwepo walau kama ilivyo kwa Mahakama - japo napo siyo huru kinadharia.
6. Tume ihusishe wawakilishi wa vyama vyote vyenye wawakilishi na ISIWE kwa uwiano wa wabunge!
 
Mkuu Izo Chezi, this is very objective, tunapoelekea kwenye uchaguzi Mkuu, watu kama nyinyi ambao ni wakweli na very objective ndio mnalisaidia taifa kwa kuueleza ukweli mchungu.

Kwa muda huu tuliobakiwa nao, ukweli ni bora kufanya kile kidogo kinachowezekana kuliko kutaka kikubwa ambacho hakiwezekani.

Kwenye uchaguzi, usawa wa haki na transparency kwenye kupiga kura ndio kila kitu.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda NEC, inaeleza wazi kuwa NEC ni independent institution, lakini kwa vile uteuzi wa viongozi wote wa NEC kuanzia Mwenyekiti, Mkurungenzi wa Uchaguzi, Makamishna, Wasimamizi wote wa uchaguzi unafanywa na mtu mmoja ambaye na yeye ni mgombea wa chama kimoja, it's expected watalipa fadhila, na mteuzi atateua makada wa chama chake, hivyo the only way ya kupata uchaguzi huru na wa haki ni kupitia maximum transparency.

Kwavile kura zinapigwa vituoni na kuhesabiwa vituoni, na matokeo yote kubandikwa vituoni, then kupitia maendeleo ya kitechnolojia, mawakala wa vyama vyote wawe na smart phones ambazo wata scan matokeo na kutuma makao makuu ya kata zao, majimbo yao na makao makuu ya vyama vyao.

Kila chama kiruhusiwe kufanya independent tallying, kwa kutumia scanned copies za vituoni, sio kwa lengo la kutangaza matokeo bali for tracking and prooving hivyo matokeo ya udiwani ya NEC, lazima ya tally na matokeo yenu, yasipo tally you have a proof.

The same ifanyike kwenye ubunge hadi urais.
P
Very good, simple and somehow effective means to the free,fair&peacefull General Election. But I'm 100%sure CCM will never allow that.
They know the results will not be on their side.Wanaogopa vitu vya uwazi na ukweli kuliko CoVid-19.
 
Yawezekana mifumo ya kitaasisi kuwa huru

Je mifumo ya kifikra ya watendaji wa taasis nayo ni huru ?
Kwahiyo viongozi wetu wa upinzani ambao ndio tunawategemea kwa mawazo mbadala ni kwamba hawako sahihi katika hili la kudai tume huru? Ni kwamba hawajui kuwa haliwezekani au wanajua ila wanatupumbaza tu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom