Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Kwa wiki karibu yote iliyopita huko visiwani Zanzibar, tume huru ya taifa ya uchaguzi ilikuwa kwenye mchakato mzito wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na namna ya kuhamisha taarifa zao iwapo mwananchi atahitaji.
Baadhi ya sehemu na tawala ambazo tume ilipita kwa ajili kutoa elimu huko visiwani Zanzibar ni pamoja na Majimbo ya Donge na Mahonda Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Unguja na majimbo ya Mtoni, Welezo, Mfenesini, Mwera na Bububu yaliyopo Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.
Soma pia: Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutekeleza uboreshaji wa daftari la wapiga kura kisiwani Zanzibar kuanza Oktoba 7 hadi 13, 2024
Tume ilipita kwenye maeneo hayo na mengine mengi ambapo ilitumia magari ya matangazo na vyombo vy habari vya huko visiwani Zanzibar kwa ajili y kuwapa wananchi elimu kuhusu namna ya kujiandikisha.
Siku ya leo Oktoba 7 Tume itaanza rasmi kuwaandikisha wananchi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ambapo zoezi hilo linategemea kumalizika Oktoba 13 mwaka huu
Zoezi hilo litahusisha mikoa mitano ya Zanzibar na vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Kwa hiyo kama huko Zanzibar, tafadhalini sana nendeni mkajiandikishe ili uweze kutimiza haki yako ya kikatiba.
Kwa wiki karibu yote iliyopita huko visiwani Zanzibar, tume huru ya taifa ya uchaguzi ilikuwa kwenye mchakato mzito wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na namna ya kuhamisha taarifa zao iwapo mwananchi atahitaji.
Baadhi ya sehemu na tawala ambazo tume ilipita kwa ajili kutoa elimu huko visiwani Zanzibar ni pamoja na Majimbo ya Donge na Mahonda Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Unguja na majimbo ya Mtoni, Welezo, Mfenesini, Mwera na Bububu yaliyopo Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.
Soma pia: Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutekeleza uboreshaji wa daftari la wapiga kura kisiwani Zanzibar kuanza Oktoba 7 hadi 13, 2024
Tume ilipita kwenye maeneo hayo na mengine mengi ambapo ilitumia magari ya matangazo na vyombo vy habari vya huko visiwani Zanzibar kwa ajili y kuwapa wananchi elimu kuhusu namna ya kujiandikisha.
Siku ya leo Oktoba 7 Tume itaanza rasmi kuwaandikisha wananchi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ambapo zoezi hilo linategemea kumalizika Oktoba 13 mwaka huu
Zoezi hilo litahusisha mikoa mitano ya Zanzibar na vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Kwa hiyo kama huko Zanzibar, tafadhalini sana nendeni mkajiandikishe ili uweze kutimiza haki yako ya kikatiba.